JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Meneja Ukaguzi wa Kampuni ya Lake Oil, Ali Sharif amesema magari yao yana mfumo wa GPS ambapo kuna mfumo wa kuziona popote zilipo, waliona zimeingia sehemu wasizozifahamu wakaanza kuzifuatilia, zilipofika Songwe wakazifanyia ukaguzi na kubaini hali hiyo.
“Magari mawili tumeyakamata tunayo hapa na mawili tumeshayazuia yapo Mbeya,” anasema Sharif.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Omari Mgumba aliyekuwepo katika kituo hicho anasema: “Chemba zote za mafuta zimejaa vipodozi, tutaendelea kushikilia mzigo na madereva watuhumiwa, gari tutaziachia kwa kuwa wahusika wameonesha hawafurahishwi na kitu hiki na wametoa ushirikiano.”
Baadhi ya madereva wa magari makubwa ya mizigo wamedai kuwa wenzao wamefanya hivyo kutokana na malipo madogo wanayoyapata kutoka kwa waajiri wao.
Chanzo: ITV