Malumbano la hoja: Mchangiaji ashangaa jiji la Dar kuvunjwa kwa kisingizio cha kubana matumizi , ashangaa Chanika kuwa jiji magomeni kuwa nje ya jiji

Malumbano la hoja: Mchangiaji ashangaa jiji la Dar kuvunjwa kwa kisingizio cha kubana matumizi , ashangaa Chanika kuwa jiji magomeni kuwa nje ya jiji

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Akizungumza kwa kujiamini mmoja wa wachangiaji amepinga kuvunjwa kwa jiji kulikoleta mkanganyiko wa hadhi ya maeneo , kwa kutolea mfano wa Chanika kuwa jijini huku Magomeni , Kinondoni , Masaki , Temeke , Mwenge na Mbezi Beach kuwa nje ya jiji .

Ametoa plan ambayo kama ingefanyiwa kazi basi mkanganyiko huo usingekuwepo na bado matumizi yangeendelea kubanwa , amedai kwamba kama lengo lilikuwa ni kubana matumizi ilikuwa rahisi tu kubadili muundo wa Jiji ambapo amependekeza vikao vya jiji vingekuwa vya mameya wa manispaa zake kwa lengo la kujadili palikofikiwa kwenye mipango ya manispaa hizo , bado jiji lingeendelea kuwepo bila kuipromote Buguruni kwa Mnyamani na kuitupa Oysterbay .

Mwisho mchangiaji huyo amekiri kufahamu mamlaka ya Rais na amesema hapingi mipango yake
 
Vingunguti tope la mbuzi ni jiji lkn Mbezi beach ni Kijiji.
 
Nimeukutia mwishoni ila mjadala ulikuwa mzuri wachangiaji wamechangia kwa uwazi bila kumung'unya maneno. Hoja ya kijana wa UD ilikuwa nzuri ingawa meya kaijibu kisiasa kana kwamba watu hawajui hali ya serikali kuu kupoka vyanzo vyote vya mapato kisha yenyewe ndiyo igawe kutokana na mipango yake ambayo wakati mwingine siyo mipango ya eneo husika.

Meya yeye anajibu oooh sijui sisi bajeti yetu ni 60b hakuna anayetuingilia hoja ni hiyo 60b ni yako au mpk huruma ya kule fedha ilipo maana unaweza kusema ni 60b ila mwenye nazo kwa mipango yako kutooana na yake anakupa tu 20b.

Hii mbinu ya serikali kuu kupora fedha za halmashauri haikuwa sahihi kama suala lilikuwa ubadhirifu ilitakiwa ni kuimarisha tu vyombo vya usimamizi wa fedha na vile vya dola kama Takukuru, polisi na mahakama vifanye kazi vizuri kudeal na hao wabadhirifu ili halmashauri ziwe na uwezo wa kuhudumia maeneo yao kwa uharaka
 
Mi nadhani uduni wa baadhi ya maeneo kufanywa hoja ya kukejeri Ilala kuwa Jiji haina mashiko, hamjaona NAIROBI SLUMS?
 
Moderator nisaidie kumuweka kwenye Ignore list huyu kapuku
Mkuu usipaniki siasa n kupambana tu kwa hoja anakera lakn anakiamsha chama chetu kiache kuoanga n chama cha zaman TLP CUF tulianza nao lakn wanamajengo yao sisi tunakwma wap? Tumeshindwa wakt wa ruzuku tutaweza wakat huu mkuu

Viva chadema
 
Mleta mada unashidwa kuelewa kuwa hayo maneno mnayoyaona leo ya Chanika, Buguruni nk... Hayata fanana hivyo miaka 15-20 ijayo.
 
Back
Top Bottom