- Thread starter
-
- #21
Ukifikiri hivi unafikiri formulaic, inside the box of orthodoxy. Ni kama unasema hakuna ndoa zisizo stable na hakuna mahusiano nje ya ndoa yaliyo stable.
In some instances, watu wanakuwa na mahusiano mazuri tu kabla ya ndoa, wakishaoana wanaanza kujisahau na kujiona wako entitled, vituko. Wanakosa mapenzi wanabaki wamefungwa na ndoa tu na wanaishi pamoja kwa kuona aibu ya talaka.
Lakini kama watu hawana kizingiti cha ndoa, wakiwa pamoja unajua kwamba wamekuwa pamoja kwa sababu wanataka kuwa pamoja, si kwa sababu wanashurutishwa na ndoa au orthodoxy yoyote.
Kuhusu wanawake kuchupachupa naona umeshindwa kunisoma kabisa kama umenisoma kama namaanisha wanachupachupa bila sababu.
Inawezekana labda wewe hujanielewa! Unapoulaumu mfumo dume ( kuwa mwanamke analaaniwa kuchupachupa na mwanammeanasifiwa) huku hujuwi kuwa pengine kwa hili la kuchupachupa hata wanawake wenyewe hawalipendi. Na ndio maana nikakwambia ulishawahi kufanya utafiti kujuwa kuwa hili la wanawake kuchupachupa nao wanataka waitwe"Vikike" kama wanavyoitwa wanaume vidume?