Mama Mbilinyi na Mama Kabendera kukata rufaa kwa hakimu Mkuu

Daisy Llilies

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2019
Posts
1,017
Reaction score
2,158
Habari tulizozipokea sasa hivi ni kuwa, wakina Mama hawa wawili wameondoka duniani kwa uchungu mkubwa kutokana na hujuma walizofanyiwa vijana wao. Vijana wao wote wawili waliwekwa gerezani mmoja akiwa amemaliza kutumikia kifungo.

Baada ya mauti ya mzazi wake ilifahamika pia kuwa Sugu alifungwa bila makosa. Leo hii mama zao wako kwa hakimu wa haki asiyepokea rushwa wala kufanya kazi kwa amri kutoka juu. Wanaomba hukumu ya haki itendeke.

Pamoja na Mama Kabendera kumuombea msamaha mtoto wake, sauti yake haikusikilizwa.

Tunawatakia Kheri ya Mwaka Mpya kutoka Radio Mbao.
 
Vijana wa upinzani bana sasa mtakufuru, kwa hiyo mlitaka yeye tu ndo asamehewe wengine wasisamehewe sio?! Na kwa mujibu wenu vijana wenye haki ni hao tu?
Anyway nawatakia Heri ya mwaka mpya makamanda.
Msisahau haya maneno ya wahenga;-
"Mchuma janga hula na nduguze"
 
Hizo ni siasa za maji taka wazazi wangapi wamekufa pasipo watoto wao kuachiwa bwana,yeye ni nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…