Maumivu chini ya kitovu au kitovuni kwa mama mjamzito si jambo geni bali huwatokea wengi tu, sio jambo la kuogofya sana na wakati mwingine huwa inashauriwa kupata medical attention.
Nini sababu?
Kawaida mimba inapokuwa huwa inasababisha ngozi na nyama za misuli ya tumbo kuvutika hii hupelekea maumivu.
Wakati mwingine husababishwa na ukuaji wa mfuko wa mtoto/mji wa mimba 'uterus', hivyo mfuko huu hukandamiza sehemu ya kitovu na kusababisha maumivu. Mwanamke hupata aina hii ya maumivu wakati wa trimester ya kwanza ya ujauzito.
Mwanamke mwenye kupata aina hii ya mkandamizo utokeao ndani, ile sehemu ambayo hupatwa na mkandamizo huu huwa 'sensitive' na wakati mwingine huwasha pale inapogusana na nguo. Aina hii ya maumivu kwa kwaida huitwa "Umbilical Hernia" yaani kitovu kinatokeza kwa nje kama uvimbe hivi, hivyo ni vyema uonane na daktari wa masuala ya uzazi.