Nimewasikia kwa hoja zenu. Wengine mna hoja wengine mna misisimko. Asiyemjua First Lady huyu naye hajitambui. Halafu wewe unayeleta kipindi cha Mama Maria Nyerere na kipindi cha sasa unakosea sana. Unalinganisha vitu wiwili tofauti. Siku hizi kuna uwazi, trasparency, kipindi kile cha Mama huyo hapakuwa na transparency sana na uhuru wa kujieleza ulidhibitiwa sana. Women Empowerment haikuwepo kipindi kile jaribu kujua na kufuatilia historia. Halafu ninyi sijui mnaishi sayari gani! Katiba Inayopendekezwa iliandikwa na Watanzania si Wana CCM kama unavyodai. Ni CCM na Vyama karibu vyote vya upinzani ikiwemo UKAWA. TLP, UDP, CCJ, CUF, CHADEMA, NLD na vingine vingi vilishiriki katika kuandika Katiba hiyo hata NCCR- Mageuzi nao walihusika. UKAWA baadhi yao walisusa hatua fulani lakini mwanzo walijadili kwa kina na kutoa mapendekezo yao. Wewe unasema ni Katiba ya CCM inabidi upimwe macho na masikio inawezekana hata mjadala hukuuona au kuusikia. Tujitokeze kwa wingi kujiandikisha na hatimaye tuipigie kura Katiba Inayopendekezwa.