Mama Salma Kikwete awataka wakazi wa Mkoa wa Lindi kuipigia kura ya ndiyo katiba pendekezwa

Hivi kweli imegusa maeneo yote? Rasimu hii na ya tume ya Warioba ipi imegusa maeneo mengi?
 
Uyu mama kapata wapi ruhusa ya kuwafundisha wanaume wapigeje kura??

aaah asitufanye sisi wajinga. aende zake akampikie mmewe
 
Kwani lazima rais aongee kwa niaba ya chama? Makamu m/kiti, katibu mkuu, katibu mwenezi na viongozi wengine wa chama wasio na madaraka yeyote wana kazi gani? Yeye kama mwenyekiti tunakubali akae kwenye vikao vya chama wakubaliane watakavyokubaliana ila hizi kazi za PR awaachie hao wengine.
 
Nimewasikia kwa hoja zenu. Wengine mna hoja wengine mna misisimko. Asiyemjua First Lady huyu naye hajitambui. Halafu wewe unayeleta kipindi cha Mama Maria Nyerere na kipindi cha sasa unakosea sana. Unalinganisha vitu wiwili tofauti. Siku hizi kuna uwazi, trasparency, kipindi kile cha Mama huyo hapakuwa na transparency sana na uhuru wa kujieleza ulidhibitiwa sana. Women Empowerment haikuwepo kipindi kile jaribu kujua na kufuatilia historia. Halafu ninyi sijui mnaishi sayari gani! Katiba Inayopendekezwa iliandikwa na Watanzania si Wana CCM kama unavyodai. Ni CCM na Vyama karibu vyote vya upinzani ikiwemo UKAWA. TLP, UDP, CCJ, CUF, CHADEMA, NLD na vingine vingi vilishiriki katika kuandika Katiba hiyo hata NCCR- Mageuzi nao walihusika. UKAWA baadhi yao walisusa hatua fulani lakini mwanzo walijadili kwa kina na kutoa mapendekezo yao. Wewe unasema ni Katiba ya CCM inabidi upimwe macho na masikio inawezekana hata mjadala hukuuona au kuusikia. Tujitokeze kwa wingi kujiandikisha na hatimaye tuipigie kura Katiba Inayopendekezwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…