Mama Samia ni wakati sasa wa kuweka Legacy yako mwenyewe

Mama Samia ni wakati sasa wa kuweka Legacy yako mwenyewe

Mr Sir1

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2018
Posts
1,749
Reaction score
7,945
Inawezekana ikawa bado mapema kumhukumu moja kwa moja ila kubwa linalomuangusha Mama ni kutaka kupendwa na kutekeleza kwa wakati mmoja. Kama kiongozi inapaswa ajue wapi pakubembeleza mahaba na wapi pa kuweka sura ya mbuzi.

Katika jaribio la kujionyesha yeye ni tofauti na mtangulizi wake, anaishia kuwa muungwana kupita kiasi. Magufuli alifanya makosa mengi mno ikiwemo kutokuwa na utu lakini haimaanishi Mama ajifanye muungwana sana ili aonekane bora mwisho wa siku watampiga na hata asijue kapigwa na nini.

Kama Mama anahitaji hasa kuweka legacy yake, angeanza na Baraza la Mawaziri. ilipaswa alifumue lote. Aweke watu ambao kawateua yeye, ambao watakuwa answerable kwake yeye na sio kuendelea na teuzi za Magufuli.

Maana kuna baadhi ya wateule wanahisi kuwa mama hana mamlaka juu yao kwa vile sio yeye aliewateua. Kuna baadhi wanaamini kuna waliokaribu na Mama ambao wana sauti kuliko mama. Kuepukana na hili angeanza upya na watu wapya. Tofauti na hapo daima atatazamwa kwa mlinganisho na Magufuli ama kumithilishwa na Magufuli kabisa.

Ili aonekane yeye kama yeye, aepuke sana kujiweka na magroup kidhahiri kabisa. Mfano kuhusishwa kwake na Kikwete kushawapa wakosoaji wake pa kuanzia. Ambapo ni kumlinganisha na Kikwete. Ina maanisha kila alifanyalo watu washalipa hatma kuwa litakuwa kama la Kikwete.

Mama aanze kusimama kama Samia. Sio muendelazaji wa Magufuli ama mshauriwa na Kikwete.

La mwisho, japo ana nia njema ya kurejesha uhusiano wa kimataifa; angetulia kidogo na hivi visafari vya hapa na pale, awaache wasaidizi wake. Maana japo safari zake zinaweza kuwa na tija, mbeleni zitatumiwa kama bakora ya kusema hakukaa nyumbani alikuwa busy na safari kama Kikwete.
 
kwa hiyo kubadili baraza la mawaziri ni "legacy" au hujua maana ya legacy
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Mama ndio kwanza ana mwezi mmoja na ushee, kila siku kelele.

Muacheni mama apumzike afanye kazi zake.
 
Miluzi imekua mingi kupita kiasi, Watanzania tutulieni tusimyumbishe rais wetu.
 
Uzuri wa Tanzania kila mtu mshauri na mtaalam wa kila jambo isipokuwa yale yanayowahusu wenyewe tu. Muacheni mama wa watu afanye kazi, hata akiharibu si kwamba atakuwa ndie wa kwanza.
 
Uzuri wa Tanzania kila mtu mshauri na mtaalam wa kila jambo isipokuwa yale yanayowahusu wenyewe tu. Muacheni mama wa watu afanye kazi, hata akiharibu si kwamba atakuwa ndie wa kwanza.
So imekuwa ni nchi ya majaribio
 
11 May 2021

Wakili wa Mahakama Kuu, Peter Madeleka akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mjadala wa kisheria na masuala ya usimamiaji ya haki za watu.

#LIVE: A-Z WAKILI ALIYEFUNGWA KWA UHUJUMU UCHUMI AFUNGUKA BAADA YA KUACHIWA HURU


Source : MwanaHALISI TV
 
Imekuwa ni desturi kwa chadema kujiona wana haki ya kukosoa tu!

Kwa muda mrefu uhuru wa habari kichwani mwa Chadema unamanisha ni kutukana na kukosoa wengine ila wao kukosolewa hapana.

Ukiwakosoa chadema watakuita ni dikteta ila wao wakikukosoa wanaita ni uhuru wa habari!

Kitendo cha Chadema kuanzisha kampeni ya kuunfollow Clouds kisa tu wamehoji watu wanaowakosoa siyo haki kabisa na ni unyumbu na uzwazwa wa hali juu kwenye chama hicho.

Jiulize kama Lema ambaye hana cheo chochote anaishi kwa kulelewa na wanaume wenzake huko Ulaya anaweza kuanzisha kampeni ya kipuuzi namna hiyo kisa tu dikteta Mbowe amekosolewa, vipi Lema angekuwa rais wa nchi angechukua hatua gani kwa clouds na wakosoaji wa mienendo ya Chadema?

Bila shaka chadema wanaohubiri demokrasia na uhuru wa kutoa maoni hawana chembe hata tone la uvumilivu pindi wanapokosolewa.
CHADEMA wametokea wapi hapa?
 
Legacy Pekee anayoweza kuiacha ni kusafiri na kuomba Mikopo/Misaada kwa Wingi kama awamu ya 4, labda na Kuvaa Magauni Mazuri
 
Back
Top Bottom