Mama wa Lugumi afariki kwa mshituko wa "tuhuma" za mwanae

Mama wa Lugumi afariki kwa mshituko wa "tuhuma" za mwanae

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,880
Breaking News : Mama wa Said Lugumu afariki dunia akiwa njiani kuja Dar kwa matubabu zaidi ,alipata tatizo la moyo baada ya tuhuma za kutisha za ufisadi kwa mwanae . Mr Lugumi kwa sasa yuko njiani kuelekea Mwanza kuandaa maazishi . Mungu amlaze marehemu mahali pema peponi , Amin!

Akielezea kwa msisitizo,mtangazaji wa Clouds Radio Ephraim Kibonde anasema Mama wa Said Lugumi alikuwa ktk mipango ya kuletwa Dsm kwa matibabu zaidi mara baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya,hali hii imesababishwa na maneno katika magazeti na vyombo mbalimbali vya habari juu ya "tuhuma" za Lugumi na mitambo ya Finger print

Chanzo:Clouds Radio
 
Bwana alitoa na bwana ametwaa , bila shaka mama yetu alikuwa mdau wa Jf .
 
SIP dear mom, ila naona chumvi imeongezwa vya kutosha kwenye hii habari.......
Cardiac failure is fatal...everybody knows that
 
Hao Clouds wamekuwa Madaktari sasa? Inakuwaje watangaze hivyo,je wao wamethibitisha vipi kama hicho ni chanzo. Yani uhai wa mtu wanafanya siasa?
 
Kumbe wizi hausaidii! Mapesa yote hayo halafu unafiwa!!!

Kumbe hata Said mwenyewe atakufa na kuacha kila kitu! Ooh Mwana acha wizi
 
Billion 30+ zote hizo , hata India ameshindwa kupelekwa na mwanae fisadi papa?
 
Kumbe wizi hausaidii! Mapesa yote hayo halafu unafiwa!!!

Kumbe hata Said mwenyewe atakufa na kuacha kila kitu! Ooh Mwana acha wizi

Dhuruma ni dhuruma. PESA alizochukuwa Lugumi zimewauwa Watanzania wengi kwa kukosa huduma muhim. Hizo fedha zingtumiwa kutowa huduma kwa Watanzania wote. Binadam lazima tujuwe hapa duniani tunapita tu na ni vizuri kutenda mema na haki. Hata ukiwa na pesa has a za wizi utaishi kwa wasiwasi. Pesa usizozitolea jasho zitakutowa damu.
 
Back
Top Bottom