Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
-
- #121
Mpangie mwana chumba, ajitenge na mamaye,
hadi apate mchumba, hapa si wewe ni yeye,
tajitenga na ushamba, ka meno na kiseyeye,
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ATAPATAPA.
tashibisha vya mlevi, tumbole kuning'inia,
wala huu si uchimvi, wahenga wanatambua,
ngadu wala sii mwivi, mwendowe tu sio nia,
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ATAPATAPA.
Mgema atapatapa, zamu imemuwadia,
eti harufu ya papa, ndio anasingizia?
kitaa anajitapa, kama jaji rugazia!
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ANATAPATAPA.
kakongorokea mediko, kaponzewa na mwanao!
simchumie viboko, akageuka kideo,
ambebe kwa mbeleko, kama mbege kwa kileo.
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ANATAPATAPA.
Kaditama wa aama! sumari nagongomeka,
mwanao kwake mama, utumbo umeungika,
takulaje vya shirima, mwanao macho tumbuka?
KUZIZOA SIFA KWA MWANA, MTUNZE NA MAMAYE. RutashubanyumaLast edited by jogi; Yesterday at 23:31.
Haswaaaaa, Makubalioano hayo hayo ndio niliataka kuongelea, siku hizi wasichana wachache sana wa umri wa over 20 wanaweza kujishtukia wana mimba bila kuua na kushindwa kufanya maamuzi ya kibinafsi zaidi.
Hivyo huo wa kwenu nahisi ulikuwa ni uamuzi wa watu wawili wazima, wenye utashi (uliokufa kwa muda) mkaamua kufanya mlilofanya.
Lakini kwa kuwa maamuzi yenu hayakusimama kwenye kweli, hayo ndio matokeo yake.
Kwa kawaida, maisha tangu vizazi vingi kiasi vilivyopita, mtoto anatakiwa azaliwe kwenye mazingira ya familia yenye baba mwanaume na mama mwanamke, wenye misimamo thabiti ya familia, hawajui kila kitu, lakini wamechagua kumsaidia Mungu na ulimwengu, kuongeza kizazi cha binaadamu, na kulea mtu ambaye atakuwa tegemeo la viumbe.
Shorkcut zilizopo siku hizi, hakuna wa kuzicontrol, ila ni wewe na utashi wako,
Na ujue sheria ya mungu ilvyo ya ajabu, kwa mtazamo wa kawaida, ni ngumu, ila kwa undani ni rahisi na shortcut kuliko zingine zote.
Hapa sisemei Dini,
Mtu yoyote akifuata utashi wake wa ndani, bila kuwa mnafiki, mbinafsi, huwezi kufanya maamuzi kama hayo. Kamwe!!!
Ila kwa udhaifu wetu, mara kwa mara tunarudia makosa yale yale.
Makovu lazima yawe machoni mwako, lazima ujifunze kuishi na matokeo ya makosa yako.
Yeye, dada, sitaki kumgusia, sitaki kuficha makosa yako kwa ajili ya makosa ya mtu mwingine, asingekuwa yeye angekuwa mwiningine, ila wewe uko hapa. Next time nadhani utaamua vingine, na pia wadogo zako, sidhani kama unaweza kuwashauri kuwa its okay kufanya maamuzi kama yako. (that is a good thing to the future generation)
Kaunga kisasi siyo chako hata siku moja..........Mwachie Muumba
jogi naona unashusha tenza za mahaba kiustadi sana..............hongera
mkuu, kama ni kweli kuwa vitu havina thamani isipokuwa tumevipa, i-paint upya picha ya mapenzi yenu, ujanja hauwi moja kwa moja na ujinga haumng'ang'anii asiyeutaka.
naamini umeingia ndani ya beti na vina vya shairi langu!!!!
I know Rutashubanyuma, but Muumba sometimes hutumia watu katika kuleta baraka na pia kuadhibu! Anyway since we are talking about Muumba now; l am sure He will see you thru, kwani hawezi kuruhusu majaribu ambayo anajua huwezi kuyakabili.
Kaunga..........hiyo kwenye nyekundu naona umeibandua kutoka 1 Corintians 10:13........."No temptation has overtaken you except such as is common to man; but God is faithful, who will not allow you to be tempted beyond what you are able, but with the temptation will also make the way of escape, that you may be able to bear."
So! Tubarikiwe sana.
[MENTION]Du uko juu ki verse za biblia. Me huwa siwezi kumbuka ni kitabu gani licha ya mstari. Here is another one, nipe reference yake: .....Itakuwa ni siku za mwisho, nitawamwagia watu wote roho yangu, wana wenu na binti zenu watatabiri, na watoto wenu wataona maono na wazee wenu wataota ndoto..... ninataka nikabishane kwenye thread moja hivi! Rutashubanyuma
Du uko juu ki verse za biblia. Me huwa siwezi kumbuka ni kitabu gani licha ya mstari. Here is another one, nipe reference yake: .....Itakuwa ni siku za mwisho, nitawamwagia watu wote roho yangu, wana wenu na binti zenu watatabiri, na watoto wenu wataona maono na wazee wenu wataota ndoto..... ninataka nikabishane kwenye thread moja hivi! Rutashubanyuma
kwa hiyo Haika baada ya hiyo hotuba wanishauri nifanyaje maana maji tayari yamekwisha kumwagika?