RIGHT MARKER
Senior Member
- Apr 30, 2018
- 129
- 473
Mambo 13 ya busara
1. Ufikapo mahali ambako umealikwa usiketi kwenye kiti kabla ya kukaribishwa na mwenyeji wako.
2. Kama unakula mbele ya watu wengine usipende kuvutana na nyama ambayo ni ngumu. Nyama ngumu achana nayo.
3. Uendapo kwenye usaili wa ajira (kazi) usivae suruali bila mkanda huku ukiwa umechomeka shati. Pia usivae viatu ambavyo havina kamba.
4. Ukialikwa kwenye sherehe yoyote kula kwanza nyumbani kwako kabla ya kwenda kwenye sherehe.
5. Ukialikwa kwenye sherehe yoyote usinywe kilevi ambacho hujawahi kunywa (Usijifunze kunywa pombe eneo hilo).
6. Kama umeongozana na mtu ambaye mnaheshimiana (mama, baba, mke, mume, mkwe, kaka, dada, kiongozi, n.k) halafu umekutana na mtu ambaye mnafahamiana kidogo na mbaya zaidi umemsahau; usimuulize mliwahi kuonana wapi au kukutana wapi. Tafuta wakati mwingine ukiwa pekee yako umuulize.
7. Mtu unayemuheshimu usimpe salamu ya mkono kabla hajaanza kukupa yeye.
8. Kama mkuu (kiongozi) wako wa kazi atahitaji muende kwenye mualiko alioalikwa, usivae nguo (suits) ya kiwango cha juu kuliko ya mwenyeji (kiongozi) wako.
9. Usiongeze maneno mengine tofauti na maneno yaliyosemwa na kiongozi (mkuu) wako wa kazi, au msemaji wa eneo lako la kazi bila ruhusa yake.
10. Usimkosoe mkubwa wako mbele ya wageni wake. Tafuta wakati mwingine wa kumkumbusha kile alichokosea.
11. Ufikapo kwenye sherehe chukua chakula kinachokutosha. Usibebe chakula ambacho huna uhakika wa kukimaliza.
12. Kama unakunywa chai na mkate mbele ya watu wengine usiloweke mkate kwenye chai - hata kama hiyo ndo staili yako ya unywaji wa chai na mkate ukiwa kwako.
13. Usipende kusifia mambo ya mwanamke mwingine (kama vile urembo, n.k) mbele ya mkeo, sifa ambazo mkeo hana.....Usipende kusifu mambo ya mwanaume mwingine mbele ya mumeo (mambo ambayo mumeo hana).
~ Ongeza jambo lingine la Busara...
Right Marker
Dar es salaam
Oktoba 1, 2024
1. Ufikapo mahali ambako umealikwa usiketi kwenye kiti kabla ya kukaribishwa na mwenyeji wako.
2. Kama unakula mbele ya watu wengine usipende kuvutana na nyama ambayo ni ngumu. Nyama ngumu achana nayo.
3. Uendapo kwenye usaili wa ajira (kazi) usivae suruali bila mkanda huku ukiwa umechomeka shati. Pia usivae viatu ambavyo havina kamba.
4. Ukialikwa kwenye sherehe yoyote kula kwanza nyumbani kwako kabla ya kwenda kwenye sherehe.
5. Ukialikwa kwenye sherehe yoyote usinywe kilevi ambacho hujawahi kunywa (Usijifunze kunywa pombe eneo hilo).
6. Kama umeongozana na mtu ambaye mnaheshimiana (mama, baba, mke, mume, mkwe, kaka, dada, kiongozi, n.k) halafu umekutana na mtu ambaye mnafahamiana kidogo na mbaya zaidi umemsahau; usimuulize mliwahi kuonana wapi au kukutana wapi. Tafuta wakati mwingine ukiwa pekee yako umuulize.
7. Mtu unayemuheshimu usimpe salamu ya mkono kabla hajaanza kukupa yeye.
8. Kama mkuu (kiongozi) wako wa kazi atahitaji muende kwenye mualiko alioalikwa, usivae nguo (suits) ya kiwango cha juu kuliko ya mwenyeji (kiongozi) wako.
9. Usiongeze maneno mengine tofauti na maneno yaliyosemwa na kiongozi (mkuu) wako wa kazi, au msemaji wa eneo lako la kazi bila ruhusa yake.
10. Usimkosoe mkubwa wako mbele ya wageni wake. Tafuta wakati mwingine wa kumkumbusha kile alichokosea.
11. Ufikapo kwenye sherehe chukua chakula kinachokutosha. Usibebe chakula ambacho huna uhakika wa kukimaliza.
12. Kama unakunywa chai na mkate mbele ya watu wengine usiloweke mkate kwenye chai - hata kama hiyo ndo staili yako ya unywaji wa chai na mkate ukiwa kwako.
13. Usipende kusifia mambo ya mwanamke mwingine (kama vile urembo, n.k) mbele ya mkeo, sifa ambazo mkeo hana.....Usipende kusifu mambo ya mwanaume mwingine mbele ya mumeo (mambo ambayo mumeo hana).
~ Ongeza jambo lingine la Busara...
Right Marker
Dar es salaam
Oktoba 1, 2024