Uchaguzi 2020 Mambo 6 yenye matumaini kutoka kwa Mgombea urais Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Mambo 6 yenye matumaini kutoka kwa Mgombea urais Tundu Lissu

PAZIA 3

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
1,102
Reaction score
1,919
Wasalaam,

Ikiwa ni kipindi cha kutafuta wadhamini kwa Wagombea urais, wala siyo kipindi cha kampeni, wagombea urais wanajaribu tu kuongea yale matamanio yao maana hawaruhusiwi kunadi ilani zao, ila utakuta watu wanasema, wapinzani wanamshambulia Magufuli wala hawasemi watafanya wakishinda uchunguzi, ni kujifariji kwamba hamuelewi kinachozungumzwa na wapinzani wa Magufuli. Hapa nimekuwekea Mambo 6 yanayoonekana kwa mgombea urais Tundu Lisu mpaka sasa.

1. Maneno yake yanapoza roho za wastaafu wengi viongozi kutambuliwa juhudi zao, wanavumilia mengi Ila roho zao zinaumizwa pale inapoonekana hawakufanya kitu wakati ndio waliomwinua mheshimiwa.

2. Maneno ya TL yanaumiza sana vyombo vya habari visivyomtendea haki kwa kuogopa serikali, ujue ukweli huwa unaumiza roho ila inabaki kugugumia moyoni, najua hata media zinatamani Lissu ashinde vipate kupumua.

3. Maneno ya Lissu na siasa zake zimeibua watu wapya waliokuwa wameachana na siasa, Ila CCM imeelekeza vijana wake kujibu mapigo harakaharaka huku mitandaoni kuziba au kuzuia upepo wa Tundu Lissu.

4. Siasa za Lissu zinawagusa moja kwa moja wapenda haki wote. Hawa ukiwauliza nani wanapenda awe Rais watakwambia Lissu, ila watasema hatoweza kulingana na siasa za Magufuli na CCM, kwamba Lissu ataishia kuwatamanisha ila hatopewa nchi.

5. Lissu anasikilizwa sana na wanadiplomasia wengi nchini ikiwemo mabalozi wetu, pamoja na kuwa wao ni sehemu ya serikali, ila huko waliko mambo wanayoyaona nchi zile nitofauti kabisa na Mambo yaliyo nchini mwao.

6. Siasa za Lissu zinawagusa watu wote hata kama hajawahi kujenga hata hospitali moja nchini, kumnyanyapaa mtu unayemlisha haifanyi akuheshimu.

Hayo ni baadhi tu Mambo machache niliyoyaona na yanayowafanya wapinzani wake Lissu kuzidi kumshambulia kwa kejeli ali khari akizidi kujizolea umaalufu mkubwa kuliko wakati wowote.

Lisu akishinda ni furaha kwa wote, ila Magufuri akishinda, vijana hasa wanachuo watalia maana atakuwa na hasira zaidi kwa watakaoonyesha mapenzi ya wazi kwa wapinzani, kutukanwa na kusimangwa itakuwa sehemu ya maisha yao, huo ndo uhalisia japo maendeleo ya miundombinu yanazidi kuonekana.
 
CCM cha pombe jana walipigwa daflau, nilikutana nao jana asubuhi kwenye supu sehemu fulani Dodoma. an inner team ya 2020 campaign for cha pombe, wamejiaminisha kwamba Tundu Lissu atawachanganya wananchi na mambo yake ya kisheria ambayo ni technical na wananchi hawayaelewi na kwamba mgombea wao anaongea lugha inayoeleweka na kuclick haraka sana kwa Wananchi.

Sasa jana Lissu kawafumania walevi hawa, na walikuwa wamelewa kwelikweli japo nasikia cha pombe mwenyewe pombe haziwezi.
Kwanza Cha pombe analazimika kubadili siasa zake zenye mawaidha ya kuwadharirisha wanawake wa Tanzania, hasa baada ya lissu kutoa tafsiri ya maneno ayapendayo cha pombe. ataweza?

Pili, mi nilifikia hatua nikasahau kwamba tuna mabwawa mengine ya umeme. hahahahaha kumbe yapo manne nadhani hahahaha. kwa miaka mitano yote zimefanyika jitihada za kufuta historia, kuficha ukweli na kutukaririsha uongo, kwamba sasa ndio tunajenga bwawa la umeme, sasa ndio tunanunua ndege.

Kwamba tuna mabwawa mengi kuliko hili ambalo limeanza kujengwa, na tumeishanunua ndege nyingi kuliko hizi zilizopo yaani hadi nimechoka.

Kweli uongo haulipi.
 
Nchi ina zaidi ya miaka 59 hakuna maendeleo licha ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani, mda huu Tanzania ilipaswa iwe level ya America, German, UK, China, Japan, South korea, India, canada Oman na mataifa mengineyo Tajiri,

kama siyo CCM mda huu Tanzania ingekuwa G5 na ingekuwa na kura ya Veto, CCM wanachukua pesa za viwanda wanazitumia kudidimiza demokrasia kuwahujumu kuwadhoofisha chadema kuua upinzani kwa ujumla wakitaka warejeshe mfumo wa chama kimoja wapate kubadili katiba kama china ili Rais awe wa milele.
 
Mkuu tutake radhi polisi tafadhali, hiyo mentality mnayojaribu kuijenga itawagharimu kwa muda, hata sisi tunapenda na tunatamani sana kuona utawala wa kisheria ukichukua nafasi yake nchini, maelekezo yametujengea uadui na watanzania wenzetu, ndugu, jamaa na marafiki. Tunahitaji kurudi katika ethics za kazi, kanuni, sheria na taratibu, msitufokee sasa mnatuvunja moyo katika kujirudi kwetu.
Mkitaka muitwe police badala ya policcm, tendeni haki pasi kupendelea upande wowote.
Mkiendelea kutumika na CCM nasi tutaendelea kuwaita Policcm mpaka Yesu arudi .
 
Mkitaka muitwe police badala ya policcm, tendeni haki pasi kupendelea upande wowote.
Mkiendelea kutumika na CCM nasi tutaendelea kuwaita Policcm mpaka Yesu arudi .
Haki itatendeka tu mkuu, mimi, yeye na yule tulikataa kuandikisha namba za vitambulisho vya kupigia kura mwaka2015.

Mimi, yeye na yule tulikataa maelekezo ya kutawanya kikao cha ndani cha chama fulani.

Mimi, yeye na yule tulihamishwa posts na kupelekwa outposts ndani ndani vijijini hakuna umeme wala maji kwa vile tulikataa maagizo haram.

Mimi, yeye na yule tumetishiwa kufukuzwa kazi kwa vile tunaonekana wanasiasa pale tunapojaribu kuwaelekeza wenzetu kuhusu sheria, kanuni na taratibu za utendaji kama afisa polisi.

Mimi, yeye na yule tunavunjika moyo kuona watanzania tunaojaribu kuwatetea leo hii wanatujumuisha na kutuona wote ni wale wale, basi ngoja tu tuendelee kuwa policcm, hatubadiliki tena!
 
Haki itatendeka tu mkuu, mimi, yeye na yule tulikataa kuandikisha namba za vitambulisho vya kupigia kura mwaka2015...
Mkuu nakubaliana nawewe siyo askari wote wanapenda kinachofanyika ..umeongea suala ambalo wengi hawajawahi kujua kwanini mtu kama RPC wa geita kipindi hicho somebody konyo aliondolewa kwenye nafasi yake kwa kusimamia weledi wa kazi yake hope wewe unaweza kuwa miongoni mwa vijana wake
 
Tundu Antipas Lissu atazoa Umaarufu wa maneno ya kejeli lakini sio kuliongoza taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2020-2025
 
Tume ya uchaguzi wajiangalie sana. Haiwezekani watu wakamatwe na fomu zao zipotetwe ili maccm yapite bila kupingwa wakati upande wa ccm hakuna waliotolewa kwani wao ni watakatifu?
 
Back
Top Bottom