Mambo Gani ya kujiandaa kwa walimu kabla ya kwenda JKT

Joined
Dec 8, 2013
Posts
94
Reaction score
10
wajamvi poleni na majukumu ya hapa na pale. Naomba mwenye Details kuhusu mambo ya kujiandaa kwa wale wanaokwena jkt kwa mujibu wa sheria atudokeze hapa.

Nawasilisha
 
Kwanza ndugu fungua moyo wako maana huku si mchezo.Mambo muhimu ni;
1.Raba pair 2
2.Track suit 2
3.Nguo za kwendea mjini ukipata pass
4.Tranka
5.Daftari(counter book)kwa ajili ya mafunzo ya darasani.
6.Hela ni muhimu kwa matumizi yako.
N.B.Hayo ni muhimu sababu nguo,raba na fedha huwa zinachelewa kufika.Karibu sana JKT,hiki chombo ni kitamu.
 
Mswaki, pakti ya sukari, pafyum, sindano na uzi wa kushonea nguo, chanuo, boxer mbili pamoja na pakiti kumi za dume kondom.
 
Vp wadau kama afya mgogoro inakuwaje hasa kwa waalim wa kike?utaajiriwa bila kupita huko jkt?p'mwenye ufaham anijuze.



Afya ikiwa mgogoro utakuwa excluded kwenye 'fatiki' badala yake utakuwa assigned tasks laini laini
 
Hebu nijue ndgu.mimi nimemaliza mwaka jana chuo na nilikuwa shule binafsi.Nataka wiki ijayo nipeleke maombi wizarani ili niajiriwe next yeae.vp na mm hyo jkt inanihusu au ndo ajira hakuna?kwa tuliomaliza miaka ya nyuma ualimu ila tunataka kuingia serikalini inakuwaje katika hilo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…