MAMBO HAYA 10 TUYAEPUKE KWANI HULETA MARADHI MENGI KWA BINADAMU

Mkuu hiyo condition inaitwa bilateral headache utakuwa unaumwa macho mcheki dokta pale AAR posta yuko vizuri hebu kacheki mapema
...nilishamcheki Dr. sio dsm ni Mt. Meru hospital Arusha,nikapewa miwani...sasa tatizo linalojitokeza ni kwamba ninakuwa nategemea sana miwani,yani siku nikiamua kutokuvaa miwani natamani pawe na mawingu ya mvua muda wote,mwanga wa jua unaniumiza macho mpk naota ndita usoni kwa sababu ya kubana macho!
 
Pole sana mkuu
 
Mkuu hujawasahau kwa bahati mbaya tu... Ni kuwa havina madhara ukitumia kiasi


HAYA NI BAADHI TU YA MADHARA YA POMBE KIFYA.ACHA KUNYWA POMBE UIMARISHE AFYA YAKO.Pombe za aina zote zina kemikali ambazo baadhi ya hizo kemikali huwa ni sumu mwilini,hivyo kuacha athari ya kiafya kwa mtumiaji.Pombe inaweza ikamdhuru mtumiaji kwa kumsababishia madhara yafuatayo:

1.Vidonda vya tumbo.
2.Kansa ya utumbo.
3.Kusinyaa kwa Ini.
4.Kansa ya Ini.
5.Kansa ya umio(oesophagus)
6.Vindonda kwenye mapafu.
7.Utapiamlo hasa wale wanaokunywa huku lishe duni.
8.Matatizo ya ganzi miguuni na mikononi(Peripheral Neuropathy).
9.Kisukari.
10.Figo kushindwa kufanya kazi.(Renal failure)
11.Kansa ya figo
12.Kukosa au upungufu wa hamu ya tendo la ndoa.(Loss of Libido)
13.Upungufu wa nguvu za kiume.
14.Kuongeza kasi kwa baadhi ya magonjwa hata kama unatumia dawa kama vile Kifua Kikuu,Kansa,Kisukari,Shinikizo la damu la kupanda.n.k
15.Kukosa hamu ya kula.(Anorexia)
16.Kutovyonzwa vyema kwa chakula(Malabosorption)
17.Ugonjwa wa kongosho.(Pancreatis).
18.Magonjwa ya moyo.
19.Mwili kutetema(Tremors)
20.Kichaa cha pombe(mtu hawezi kufanya kazi bila ya pombe,au anakuwa kama mgonjwa lakini akipewa pombe tu anakuwa mzima)
 
Usimeze Vidonge vya kizungu vina madhara baadae ukivizoea sana. Kula punje 12 za Lozi unapo jisikia unaumwa na kichwa au waweza kunywa maji ya Uvuguvugu glasi 2 kichwa hapo hapo kitapona.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…