"Mambo kwa soksi"

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Hakika kifo cha mkongwe wa muziki nchini Dkt. Remmy Ongara kitakuwa kimewashtua watu wengi.

Leo hapa nimekuwa nikisikiliza nyimbo zake nyingi tu. Na katika pekua pekua yangu nikakutana na mkanda wa kaseti wenye wimbo wa "mambo kwa soksi" uliokuwa ukizungumzia matumizi ya kinga ya mipira ya kiume wakati wa kufanya mapenzi.

Wimbo huu ulipingwa sana hadi kufikia redio Tanzania kukataa kuupiga na kanda zake zikawa zinauzwa kinyemela kwenye soko la giza.

Sasa hivi matangazo ya kinga ya mipira yako kila sehemu. Iwe mabango, magazetini, redioni, kwenye tv, na sehemu nyingine nyingi.

Kwa maono yangu Dkt.Remmy aliona mbali sana kuliko hata watawala wetu wa wakati huo. Alichopingiwa enzi hizo ndicho kinachofanyika hivi sasa. Kweli mtu huhitaji shahada kuwa na busara.
 
Huwa najiuliza ni kwa nini alinyimwa uraia wa Tz?
 
Mhhh Kevin tena! .......Haya bwana
 
Huwa najiuliza ni kwa nini alinyimwa uraia wa Tz?

Kuna wimbo alimwimbia Mrema....enzi za NCCR...labda ulimponza....
Ila nadhani alipewa baadae?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…