Mambo manne yatakayokusaidia kudili na mambo usiyoyatarajia

Mambo manne yatakayokusaidia kudili na mambo usiyoyatarajia

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241128_173703_Google.jpg

Kama wanadanamu hatuwezi kuishi kila siku kwa namna moja au kuwa na furaha muda wote au kuwa na mambo mazuri siku zote, bali kuna nyakati ambazo tunakutana na mambo ambayo hatuyatarajii kabisa

Sasa haya mambo ambayo hatuyatarajii ingawa tunajua yanaweza kutokea muda wowote ule basi nakuletea mambo manne ambayo ukikutana na hali hiyo basi uweze kudili nayo

Screenshot_20241128_173905_Google.jpg

Mosi,kukiri kwanza jambo fulani lisilo kupendeza limetokea, inaweza kuwa ajali, maradhi, kufukuzwa kazi, kuachwa nakadhalika, kukiri kwamba umetokewa na jambo hilo ni njia ya kukupa utulivu

Mbili,kukubali hali hiyo kwamba imetokea au imekutokea,kitendo hiki ni njia ya kiroho ambayo itakusaidia kutoka kwenye machungu na maumivu na kukupeleka kwenye utulivu wa nafsi, kubali kwamba wewe ni HIV positive kwa maana ishatokea tayar huwezi kubadili hali hiyo cha kufanya ni kuikubali hali hiyo

Kubali kwamba mahusiano yamefika mwisho umeachwa kwahiyo ipokee hiyo hali kama ilivyo, kubali kazi umeachishwa ndo ishatokea sasa huwezi kurudisha siku nyuma, kwa kukubali hali hiyo hapo utapata utulivu na amani, usitafute mchawi we kubali tu kwamba ishatokea

Tatu, kubali kuingia katika mazingira mapya ili uondokane na hali iliyo kutokea au unafuu upatikane, hapa weka igo yako pembeni, ulikuwa na kazi nzuri sana sasa imeisha, acha kuishi kama mambo safi hapa ishi kutokana na mazingira ulinayo sasa, paki ndinga pembeni usiingie kwe mikopo ili uendeshe gari ambalo sasa huwezi kulihudumia, nenda kituo chukua dala dala fresh tu

Nne,hatua hii ndio nyepesi hasa baada ya kuzikubali hatua hizo tatu zilizo pita, nayo ni kufanya kwa vitendo sasa,ni wakati wa kukung'uka suruali au sketi na kusimama na kusonga mbele kwa vitendo, hapa sahau huzuni zote,ondoa maumivu yote na songa mbele, wanasema majaliwa yakifunga mlango wa mafanikio basi matumaini hufungua milango mipya ya mafanikio.

Ni hayo tu!
 
N jambo la kuamua tu kutotoka nje ya ndoa, amua sasa? Unaendelea tu na mambo ya hovyo, twamuitaji Mungu!

Hayo uliyosema hapo ni sahihi, ila sio rahisi Kama unavyozungumza! Ni project haswa!
 
Duh yaani kukubali nimefukuzwa kazi itoshe kunipa faraja , utulivu wa nafsi na amani? hapo ndipo pagumu, hapo sijapaelewa kwakweli, mbona kama vile ukikubali ndipo maumivu yanaongezeka.
 
Duh yaani kukubali nimefukuzwa kazi itoshe kunipa faraja , utulivu wa nafsi na amani? hapo ndipo pagumu, hapo sijapaelewa kwakweli, mbona kama vile ukikubali ndipo maumivu yanaongezeka.
Ukikubali maana yake unafungua milango ya kusonga mbele na kutafuta malisho mapya,usipokubali ndio uchawi unaanzia hapo

Utataka kumjua mchawi wako nani aliyesababisha ufukuzwe kazi,au utabakia na stress kwanini wamekufukuza kazi?

Lkn kukubali huo ukweli kunakupa nafasi ya kusonga mbele na hutapoteza mda kuwaza na kulalamika kwanini wewe na si mtu mwingine?
 
Back
Top Bottom