Mambo ya ajira online

Mambo ya ajira online

Samtee

Member
Joined
May 2, 2018
Posts
89
Reaction score
118
Aisee kwanza habari za asubui, niwapeni mikasa ya ili jambo la kuomba ajira mtandaoni.

Kumbuka hapa siongelei ajira portal wala Taesa wala makampuni yenye kutangaza kazi.

Naongelea ile mtu kapost kuna nafasi ya ajira ameweka namba umtafute labda whatsapp au sms.
Jumlisha na wale wa kutoa connection. Aiseee tuwe makini mno tena haswa kwa watoto wa kike.

Yaani mtu unamtafuta kazi ukiiulizia imeungwa ungwa basi unaamua kwenda/kuichukua maana shida ni nyingi alafu huko kwenye iyo kazi sasa.

Ushauri mtu akikupa kazi huku au kokote lakini huoni io kampuni mahali kwenye mtandao achana nayo.
Ukimwomba mwajiri taarifa za kampuni na anakula chenga achana nayo.

Kama ni mkoani tafuta mtu unae mjua aende hapo kwanza au akutafutie taarifa za hapo mahali kabla hujaenda.
Ukiacha kufanya yote aya basi ukienda kuwa mdadisi.

Kwa sababu watu wanauzwa, watu wanabambikiwa makesi, watu wanapotezwa kikubwa uchafu ni mwingi.
 
Huo ujinga sifanyi, kama Tangazo halina jina na info za kampuni situmi CV, kama ni uhuni hivi, wanaweza kuchukua info za referee kutapeli.
 
Hivi kwanini wanataka certified copies badala ya cheti original?

Kuna sababu yoyote ya kitaalamu?
 
Back
Top Bottom