Mambo ya kutisha yanayoendelea nchini ni ishara kuwa nchi yetu ipo katika laana kwa sababu imetiwa unajisi na damu za wasio na hatia

Mambo ya kutisha yanayoendelea nchini ni ishara kuwa nchi yetu ipo katika laana kwa sababu imetiwa unajisi na damu za wasio na hatia

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Matukio ya kutisha na ya kishetani, kama yale ya utekaji wa watu na kuwapoteza, watoto wadogo kuuawa, kutawaliwa na watu wenye mioyo ya ukatili wa kupindukia, uovu kupewa heshima dhidi ya wema, ni ishara kuwa, yamkini nchi yetu ipo katika laana kwa sababu imetiwa unajisi na damu za wasio na hatia. Jambo la kujiuliza, tumefikaje hapa? Laana hii imetokana na nini?

Kwa wanaoamini uwepo wa Mungu wetu, muweza wa yote na mkuu wa kila kitu, wanaweza kurejea katika mafundisho ya kiimani na Biblia Takatifu kuhusiana na uovu wa umwagaji wa damu za wasio na hatia.

Hesabu 35:33:  "Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu"

Nchi hii kuna watu wengi wamepotea na kuuawa tena bila hatia. Tunaambiwa damu za wasio na hatia zikimwagwa zinaitia nchi nzima unajisi.

Mkumbuke matukio ya watu kutekwa na kuuawa hapo awali yalikuwa machache sana, lakini sasa yameongezeka maradufu kiasi cha baadhi ya watu, hasa wenye mamlaka, kututaka tuyaone kuwa ni matukio ya kawaida. Yaani tusione ajabu mtu kutekwa na kupotezwa au hata kutekwa na kuuawa na kisha mwili wake kutupwa porini Katavi na kwingineko ukaliwe na wanyama.

Ndiyo maana watawala huwezi kuwasikia wakitoa sauti kuonesha kuhuzunishwa na matukio haya ya kishetani. Ukiona wanaongelewa basi mpaka wawe wameulizwa.

Pia soma: Kuua ni laana hata vitabu vya vidini vimesema hivyo, usikubali kubebeshwa dhambi hiyo
 
Matukio ya kutisha na ya kishetan, kama yale ya utekaji wa watu na kuwapoteza, watoto wadogo kuuawa, kutawaliwa na watu wenye mioyo ya ukatili wa kupindukia...
Hakika.

Taifa Zima inabidi liingie Kwenye maombi Kwa Mungu, Ili atuepushe na hii laana ya kutekana na kuuwana😎
 
Leo Kwa taarifaa ya habar nimesikia Kuna mgangaa kakamatwa sijui wapi huko kazika watu wengi tu uku amewakalisha na inasemekana walizikwa wakiwa hai ktk maiti zilizofukuliwa zimekutwa maiti za watoto wadogo pia ...

Km taifaa tuna safari ndefu sana
 
Leo Kwa taarifaa ya habar nimesikia Kuna mgangaa kakamatwa sijui wapi huko kazika watu wengi tu uku amewakalisha na inasemekana walizikwa wakiwa hai ktk maiti zilizofukuliwa zimekutwa maiti za watoto wadogo pia ...

Km taifaa tuna safari ndefu sana
Hii laana bila kuukata mnyororo wake, tutaendelea kuishi katika laana. Itakuwa ni nchi ya mauji wakati wote.
 
Matukio ya kutisha na ya kishetani, kama yale ya utekaji wa watu na kuwapoteza, watoto wadogo kuuawa, kutawaliwa na
Wanasiasa wanafanya ufedhuli wao kwa njia hii mbele ya uchaguzi mkuu kwani njia ya ajali za magari imeshajulikana na watu.
 
Kwa mujibu wa Jasusi
Evarist Chachali kwenye kitabu chake cha Shushu (Afisa Usalama wa Taifa) ni nani na anafanya nini ?
Kazi yake ni kuhakikisha kuzuia kila aina ya tukio limalosababisha ukosefu wa usalama kwa Taifa lake au Wananchi wake. Sasa Mimi nashangaa hawa Usalama wa Taifa wanafanya nini hasa ? Hawanusi hatari zao haya matukio ya Utekaji, Mauaji ya raia wake ? Na hawa Watekaji na Wauaji ambao wanajitambulisha kwa utambulisho wa Polisi ni wakina nani hasa ?
Najiuliza mwenyewe maswali hapa.
Kazi ya Usalama wa Taifa ni ipi sasa ? Taifa lolote lile ni watu na Watu ndio hivyo wanatekwa, wanapotea na wanakutwa wameuwawa.
Ifikie wakati Vyombo vya Ulinzi na Usalama vitangulize mbele Usalama wa raia wake kwanza maana huko kwengine kwenye rasilimali za Taifa zimekuwa ni za Wachache ambao ni Wanasiasa. Basi mtuhakikishie Usalama wetu.
 
Hesabu 35:33:  "Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu"
Hawatakuelewa kamwe
 
Matukio ya kutisha na ya kishetani, kama yale ya utekaji wa watu na kuwapoteza, watoto wadogo kuuawa, kutawaliwa na watu wenye mioyo ya ukatili wa kupindukia, uovu kupewa heshima dhidi ya wema, ni ishara kuwa, yamkini nchi yetu ipo katika laana kwa sababu imetiwa unajisi na damu za wasio na hatia. Jambo la kujiuliza, tumefikaje hapa? Laana hii imetokana na nini?

Kwa wanaoamini uwepo wa Mungu wetu, muweza wa yote na mkuu wa kila kitu, wanaweza kurejea katika mafundisho ya kiimani na Biblia Takatifu kuhusiana na uovu wa umwagaji wa damu za wasio na hatia.

Hesabu 35:33:  "Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu"

Nchi hii kuna watu wengi wamepotea na kuuawa tena bila hatia. Tunaambiwa damu za wasio na hatia zikimwagwa zinaitia nchi nzima unajisi.

Mkumbuke matukio ya watu kutekwa na kuuawa hapo awali yalikuwa machache sana, lakini sasa yameongezeka maradufu kiasi cha baadhi ya watu, hasa wenye mamlaka, kututaka tuyaone kuwa ni matukio ya kawaida. Yaani tusione ajabu mtu kutekwa na kupotezwa au hata kutekwa na kuuawa na kisha mwili wake kutupwa porini Katavi na kwingineko ukaliwe na wanyama.

Ndiyo maana watawala huwezi kuwasikia wakitoa sauti kuonesha kuhuzunishwa na matukio haya ya kishetani. Ukiona wanaongelewa basi mpaka wawe wameulizwa.

Pia soma: Kuua ni laana hata vitabu vya vidini vimesema hivyo, usikubali kubebeshwa dhambi hiyo
nyie ni wambea Sana mlisema Magufuli aliteka watu lkn leo hayupo mnaletq ujinga wenu tunajua ujambazi wenu wachaga
 
Hali mbaya sana.

Halafu na mimi kuna mjinga mmoja nataka nimteke mjinga yule anataka kunizoea
 
Back
Top Bottom