Mambo ya kuzingatia unapoagiza bidhaa Mtandaoni

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124


Chunguza Maelezo ya Bidhaa. Chukua muda kusoma na kuelewa yaliyomo kwenye bidhaa unayotaka kununua. Usidanganyike na picha zilizohaririwa vizuri zinazoweza kupotosha muonekano halisi wa kitu hicho.

Linganisha bei za Bidhaa zinazofanana, lengo lako ni kununua bidhaa bora kwa bei nzuri.

Soma uchambuzi wa bidhaa, njia rahisi ya kupata bidhaa bora ni kupitia hakiki za bidhaa. Uliza watumiaji wengine ili kujiridhisha kuhusu ubora wa bidhaa hiyo.

Fahamu sera za mchakato wa ununuzi wa vitu kwa wauzaji wako. Baadhi ya wafanyabiashara huwa na sera kandamizi kwa wateja, mfano wengine huwa hawaruhusu kurudisha vitu kama vile vifaa vya elektroniki na bidhaa nyingine zinapokuwa zimefunguliwa.
 
Upvote 1
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…