Mambo ya kuzingatia unapotangaza biashara mtandaoni

Mambo ya kuzingatia unapotangaza biashara mtandaoni

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
20210305_103604_0000.png


MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTANGAZA BIASHARA MTANDAONI

Jifunze na uitambue hadhira yako unayoilenga

Ikiwa huijui hadhira yako ni ipi, huwezi kuipa kile inachotaka, na kisha nayo haitakupa kile unachotaka.

Wafahamu kwa umri wao, wanaishi wapi, wanazungumza lugha gani na wapo katika hatua gani ya maisha (mwanafunzi, mzazi, mstaafu)

Chagua ni mitandao ipi utumie na ipi ya kupuuza

Tafiti idadi ya watu wanaotumia mitandao hiyo. Hii itakusaidia kuamua ni mitandao gani utumie na ipi ya kuachana nayo.

Fahamu washindani wako; Kwa sababu ikiwa hutafanya hivyo, watapata nguvu. Pia, kujifunza kutoka kwenye kile wanachofanya, itakusaidia kuamua ni nini unapaswa na kipi hupaswi kufanya.

Jua ni kina nani, wako wapi, wanafanya nini, walifanya nini hapo awali, kama wanaleta vitisho vyovyote kwenye biashara yako, wako mitandao gani, hadhira yao ni kubwa na wanachapisha mara ngapi
 
Upvote 1
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom