Mambo ya Pesa; Kila tukio ni sherehe

Vinci Dayot Upamecano

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2020
Posts
524
Reaction score
1,288
Asalaam Aleykum warahmatullah wabarakatul, Ramadan Mubarak.

Penye hela nyingi hapaharibiki neno, kuna mshkaji wangu mmoja hiv ametusua bwana, sasa siku ya Jana Ijumaa alinipa mualiko kwenye Hafla fupi ya kumpongeza Binti yake wa miezi 10 kwa sasa, ameweza kutembea mwenyewe.

Kwanza sherehe ilikuwa sio baridii, Wageni walikuwa nyomi Ile mbayaa, yaani watu walikuwa ni wengi sana waliokwenda kusherehekea mtoto ameweza kutembea mwenyewe (na mimi pia ni miongoni mwao). Ilikuwa ni kama li'sherehe fulani hivi likubwa la harusi, Kuanzia muziki, vyakula, vinywaji, wageni, ukumbi, Maonyesho hadi Zawadi kumbe ni mtoto ameweza kutembea, wanangu tutafute mboga.

Jamaa ni kawaida yake tangu atusue (naongea kwa kumsifu sio kwamba nampiga madongo) amekuwa anafanya vi'event fulani hiv vyenye maudhui ya kawaida kwa gharama kubwa sana (pesa si ipo bwana). Jamaa anakwambia tangu anazaliwa mpaka mwaka juzi 2021 hakuwahi kufanyiwa Birthday Party, Sasa hiyo mwaka Jana alijifanyia Birthday Party ya kufuru, watu tulikula, kunywa na kusaza.

Mwaka Jana 2022 kafanya bonge moja la Party kuzindua nyumba yake, mwaka huohuo kamfanyia Party moja ya kutisha mtoto wa sister'ake kumpongeza kwa kuhitimu Nursery.

Bado una ule mtazamo wako kuwa "Pesa haiwezi kununua furaha"?
 
Mmmmmh
 
Masikitini akipata matako hulia mbwata.
 
Five years later......
 
Umekuja kumsifia mwanaume mwenzio ana pesa...kama mwanaume umri wako bado mdogo saana kifkra
 
Inaweza kununua
 
Chanzo cha hizo pesa.
Maana watu wa style hii wanapaswa kufanya hivyo ili kukuza utajiri wao.
Kadiri anavyofanya ndio anavyozidi kitoboa.
 
Umekuja kumsifia mwanaume mwenzio ana pesa...kama mwanaume umri wako bado mdogo saana kifkra
Una uhakika gani kama mimi Sina Pesa?, Chunga sana kijana

Kama una shida ni vema kuomba msaada sio unataka kumalizia hasira zako za umaskini kwa watu wenye hela.
 
Chanzo cha hizo pesa.
Maana watu wa style hii wanapaswa kufanya hivyo ili kukuza utajiri wao.
Kadiri anavyofanya ndio anavyozidi kitoboa.
Jamaa anatumia hela kwa namna fulani ya walakini, anyway Anajia yeye na Mungu wake.
 
Tumia Pesa ikuzoee bob
Bob, kuna kuwa na hela na kuna kuwa tajiri. Mtu yeyote anaweza kuwa na hela, lakini sio kila mtu anaweza kuwa tajiri.

Matendo ya huyu jamaa yanaonyesha ana pesa, lakini sio tajiri.
Utajiri ni discipline, utajiri ni lifestyle, utajiri ni kuinvest.

Utajiri ungekuwa hivyo u gesi kiasi Bakhresa anafanya party ya kuona paka wakinyanduana
 
Got you, Appreciate.

Tutafute hela na tuwe Matajiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…