Mambo yahusuyo Muungano kama yalivyotajwa kwenye Katiba

Mambo yahusuyo Muungano kama yalivyotajwa kwenye Katiba

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1608035071526.png

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ibara ya 4(3) imeeleza kuwa kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za umma Katika Jamuhuri ya muungano na kwa ajili ya madaraka juu ya shughuli hizo kutakuwa na mambo ya muungano ambayo yatafanywa kwa ushirikiano kati ya Tanzania bara na Zanzibar na pia kutakuwa na mambo yasiyo ya muungano.

Mambo yote ya muungano yameorodheshwa katika Nyongeza ya Kwanza ( First Schedule) katika katiba hiyo.
Mambo hayo ni kama ifuatavyo:-

1. Katiba ya Tanzania na serikali ya Jamhuri ya Muungano.

2. Mambo ya Nchi za nje

3. Ulinzi na usalama

4. Polisi

5. Mamlaka za Juu ya mambo
yanayohusika na hali za hatari

6. Uraia

7. Uhamiaji

8. Mikopo na Biashara ya Nchi za nje

9. Utumishi katika serikali ya Jamhuri ya muungano

10. Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa Forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha

11. Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta, na simu

12. Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo halali, mabenki na shughuli zote za mabenki, fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.

13. Leseni ya viwanda na takwimu

14. Elimu ya juu

15. Maliasili ya mafuta

16. Baraza la Taifa la Mitihani ya Tanzania

17. Usafiri na usafirishaji wa Anga

18. Utafiti

19. Utabiri wa Hali ya hewa

20. Takwimu

21. Mahakama ya Rufani

22. Uandikishaji wa vyama vya siasa na mambo mengine yanayohusiana navyo.

Hivyo, mambo mengine yote ambayo hayapo katika orodha hii sio mambo ya muungano, pande zote mbili ( Tanzania Bara na Zanzibar) zinaweza kuyaendesha tofauti.
Mfano wa Mambo yasiyo ya muungano ni pamoja na Ardhi na Mazingira.
 
Upvote 2
4. Polisi

Kumbe wale waliokuwa wanalalamika eti "mapolisi ya bara yamemwagwa Zenj kama ubwabwa wa Hashim Rungwe," hawajui kabisa Katiba!???
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom