Mambo yasiyonipendeza na kuvutia sana Marekani

Mambo yasiyonipendeza na kuvutia sana Marekani

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
1. Biashara holela ya bunduki kwa raia
Hizi taarifa za kupigana sana risasi hovyo hovyo kila siku kwa sababu ya biashara holela ya silaha isiyo na udhabiti mpana kama mataifa mengine ya West na yaliyoendelea zinasikitisha na kutia doa sana Marekani. Kifo cha risasi kwa watoto ndicho chanzo kinachoongoza kwa sasa. Nafikiri sio sahihi kabisa, na ni wendawazimu wa hali ya juu kuruhusu bunduki za kila aina kuuzwa kama bidhaa nyingine ambapo mtu yeyote hata mwenye matatizo ya akili, umri mdogo au mhalifu anaweza kununua bunduki kirahisi kama bidhaa nyingine yoyote.

2. Wafahidhina/Conservatives hasa MAGA Republicans
Hawa watu nawaona wa ajabu sana katika sera na misimamo yao. Hawataki sheria zozote ngumu kuhusu umilikaji bunduki, hawapendi sana msaada wa serikali kwa watu masikini, ukiwa kinyume na Democrats wewe ni rafiki yao na wataungana na wewe, wamejaa conspiracy theories za kila aina. Ni tofauti sana na conservatives wengine wa West na nchi zilizoendelea ambao wana make sense kwa mambo mengi.

3. Ughali wa huduma za matibabu na dawa sekta ya afya
Marekani ni taifa ambalo gharama za kila matibabu ziko juu na dawa zinauzwa ghali sana tofauti na kwingine duniani. Sekta ya afya ni mojawapo ya sekta zenye mzozo mkali sana katika siasa za hii nchi .Upande mmoja wa Democrats wakitaka udhibiti, usaidizi na ufadhili zaidi wa serikali kupitia bima na sheria na upande mwingine wa Republicans ukitaka biashara huria zaidi ambapo makampuni ya dawa, bima, hospitali na wateja wao ndio watakuwa na maamuzi yao makubwa zaidi ya kibinafsi.
 
Huko mambo ni mazuri, changamoto ndogo ndogo za kawaida tu.
Vipi pia kuhusu msimamo wa Democrat na Republican kuhusu sekta ya afya ? Pia msimamo na mapendekezo ya raia wa kawaida ?
 
biden.PNG
 
1. Biashara holela ya bunduki kwa raia
Hizi taarifa za kupigana sana risasi hovyo hovyo kila siku kwa sababu ya biashara holela ya silaha isiyo na udhabiti mpana kama mataifa mengine ya West na yaliyoendelea zinasikitisha na kutika doa sana Marekani. Kifo cha risasi kwa watoto ndicho chanzo kinachoongoza kwa sasa. Nafikiri sio sahihi kabisa, na ni wendawazimu wa hali ya juu kuruhusu bunduki za kila aina kuuzwa kama bidhaa nyingine ambapo mtu yeyote hata mwenye matatizo ya akili, umri mdogo au mhalifu anaweza kununua bunduki kirahisi kama bidhaa nyingine yoyote.

2. Wafahidhina/Conservatives hasa MAGA Republicans
Hawa watu nawaona wa ajabu sana katika sera na misimamo yao. Hawataki sheria zozote ngumu kuhusu umilikaji bunduki, hawapendi sana msaada wa serikali kwa watu masikini, ukiwa kinyume na Democrats wewe ni rafiki yao na wataungana na wewe, wamejaa conspiracy theories za kila aina. Ni tofauti sana na conservatives wengine wa West na nchi zilizoendelea ambao wana make sense kwa mambo mengi.

3. Ughali wa huduma za matibabu na dawa sekta ya afya
Marekani ni taifa ambalo gharama za kila matibabu ziko juu na dawa zinauzwa ghali sana tofauti na kwingine duniani. Sekta ya afya ni mojawapo ya sekta zenye mzozo mkali sana katika siasa za hii nchi .Upande mmoja wa Democrats wakitaka udhibiti, usaidizi na ufadhili zaidi wa serikali kupitia bima na sheria na upande mwingine wa Republicans ukitaka biashara huria zaidi ambapo makampuni ya dawa, bima, hospitali na wateja wao ndio watakuwa na maamuzi yao makubwa zaidi ya kibinafsi.
Hiyo ya kumiliki bunduki naunga mkono, Marekani ni taifa flan Kila mtu anajiona mbabe na muhuni kuliko mwenzake pia uhalifu mwingi.
 
Shida ya marekani ni matajiri wakubwa na wenye ushawishi kwenye siasa za marekani sababu lazima tukumbuke kuw idadi kubwa ya watu ni watu weupe na asili ya marekani imejengwa na capitalist wakubwa na walienda marekani ili kupata faida zaidi kwenye biashara zao. Kuna mambo ambayo yanaleta sana migogoro na mwngine yatakuja kuleta sana migogoro mbeleni maana saivi yanakuja polepole kwenye maisha ya wananchi wa kawaida.

Umiliki wa silaha umeshakuwa janga kwa taifa ni sawa na mraibu wa madawa au pombe yanakuaribu ila bado unatamani kuyatumia makampuni ya silaha yanailetea serikali pesa nyingi na yanapata faida kubwa sana ni jambo la kushangaza sana kwamba ata pale mauaji ya wanafunzi mashuleni yanapotokea suluhisho wanalikuja nalo serekali za majimbo ni kurahisisha umilikiji wa silaha ata zile ambazo ni za kivita apo ndyo uone vile makampuni ya silaha yanaushawishi kwenye siasa za marekani obama alishindwa, Biden kwenye sera za kampeni alinadi ataweka sheria ngumu naona naye kashindwa

Swala la afya ni zimwi likukulalo ambalo alishibi makampuni ya dawa na hospitali zinasingizia tafiti zinatumia pesa nyingi ila ni kama nayo zinataka kujipatia pesa kwenye mgongo wa tafiti wataalamu wanasema kidonge cha maumivu kinauzwa ghali sana marekani kuliko taifa lolote duniani, Obama alijitaidi kuongeza kodi kwa matajiri ili watu wa vipato vya kati wapate bima kwa wingi ila naona Trump alivyoingia akaona ni biashara kichaa akaitoa yote ni katika kuwafever matajiri wafaidike na uwekezaji wao

Zimwi lingine linalokuja kwa kasi ni kwenye sekta ya elimu uko naisi miaka mi5 mbeleni wanafunzi wengi watakuwa wanaanza kazi wakiwa na madeni lukuki kutoka kwenye mikopo ya elimu wanayoipata elimu ni gharama sana marekani mtu wa kipato cha chini hawezi mudu kumsomesha mwanae elimu ya juu bila mkopo na mkopo nawo ni mkubwa kuliko kawaida maana kwa mwaka kwa vyuo vya kawaida inawza mkost mwanafunz si chini ya dola30k icho ni kiwango cha chini

Zimwi lingine linalikuja polepole lakin kwakasi ni upande wa vyakula saivi vyakula vya fast food vinagharama nafuu kuliko vyakula vya kujipikia matunda mbogamboga ziko juu kuliko kawaida miaka10 mbeleni naisi tutakuwa tunaongelea mengine

Shida ya marekani si kingine ila ni sababu ya mfumo wao ulivyoo capitalist ni watu wanaoitaji faida zaidi na zaidi kuwagusa kwenye biashra zao ni kujitafutia matatizo hasa kwa chama kilichopo madarakani
 
Umilikaji bunduki kwa raia ni jambo linalopendelewa na Republicans zaidi sio Serikali. Democrats siku zote huwa wanataka udhibiti mkubwa wa silaha ila hawajawahi kupata uungwaji mkono kutoka Republicans kupitisha sheria kali za udhibiti, hata majimbo yanayolegeza sheria na kuruhusu hadi watu kutembea na bunduki za kivita wazi barabarani ni ya Deep red states ya Republicans.
Shida ya marekani ni matajiri wakubwa na wenye ushawishi kwenye siasa za marekani sababu lazima tukumbuke kuw idadi kubwa ya watu ni watu weupe na asili ya marekani imejengwa na capitalist wakubwa na walienda marekani ili kupata faida zaidi kwenye biashara zao. Kuna mambo ambayo yanaleta sana migogoro na mwngine yatakuja kuleta sana migogoro mbeleni maana saivi yanakuja polepole kwenye maisha ya wananchi wa kawaida.

Umiliki wa silaha umeshakuwa janga kwa taifa ni sawa na mraibu wa madawa au pombe yanakuaribu ila bado unatamani kuyatumia makampuni ya silaha yanailetea serikali pesa nyingi na yanapata faida kubwa sana ni jambo la kushangaza sana kwamba ata pale mauaji ya wanafunzi mashuleni yanapotokea suluhisho wanalikuja nalo serekali za majimbo ni kurahisisha umilikiji wa silaha ata zile ambazo ni za kivita apo ndyo uone vile makampuni ya silaha yanaushawishi kwenye siasa za marekani obama alishindwa, Biden kwenye sera za kampeni alinadi ataweka sheria ngumu naona naye kashindwa

Swala la afya ni zimwi likukulalo ambalo alishibi makampuni ya dawa na hospitali zinasingizia tafiti zinatumia pesa nyingi ila ni kama nayo zinataka kujipatia pesa kwenye mgongo wa tafiti wataalamu wanasema kidonge cha maumivu kinauzwa ghali sana marekani kuliko taifa lolote duniani, Obama alijitaidi kuongeza kodi kwa matajiri ili watu wa vipato vya kati wapate bima kwa wingi ila naona Trump alivyoingia akaona ni biashara kichaa akaitoa yote ni katika kuwafever matajiri wafaidike na uwekezaji wao

Zimwi lingine linalokuja kwa kasi ni kwenye sekta ya elimu uko naisi miaka mi5 mbeleni wanafunzi wengi watakuwa wanaanza kazi wakiwa na madeni lukuki kutoka kwenye mikopo ya elimu wanayoipata elimu ni gharama sana marekani mtu wa kipato cha chini hawezi mudu kumsomesha mwanae elimu ya juu bila mkopo na mkopo nawo ni mkubwa kuliko kawaida maana kwa mwaka kwa vyuo vya kawaida inawza mkost mwanafunz si chini ya dola30k icho ni kiwango cha chini

Zimwi lingine linalikuja polepole lakin kwakasi ni upande wa vyakula saivi vyakula vya fast food vinagharama nafuu kuliko vyakula vya kujipikia matunda mbogamboga ziko juu kuliko kawaida miaka10 mbeleni naisi tutakuwa tunaongelea mengine

Shida ya marekani si kingine ila ni sababu ya mfumo wao ulivyoo capitalist ni watu wanaoitaji faida zaidi na zaidi kuwagusa kwenye biashra zao ni kujitafutia matatizo hasa kwa chama kilichopo madarakani
 
Ni vigumu kuelewa hili ila nafikiri kwenye Afya na silaha kuna fursa za masilahi makubwa sana kwa makundi mengi mbalimbali yaliyo kimaslahi kuliko katika elimu na usafiri.
Huko kwenye elimu na usafirishaji serikali iliweza vipi kufanikiwa ila kwenye afya imekuwa mtihani ?
 
Ni vigumu kuelewa hili ila nafikiri kwenye Afya na silaha kuna fursa za masilahi makubwa sana kwa makundi mengi mbalimbali yaliyo kimaslahi kuliko katika elimu na usafiri.
Ishu ya silaha ni ngumu sana na ata kama wataweka sheria ngumu bado umiliki wa silaha bila vibali itachukua nafasi
Republican inaongozwa na mabwanyenye sera zao nyingi ni kuwapendelea wao ata misimamo yao ni ile ya mlengo wa kutotaka mabadiliko mapya sababu yanawabe a wao na viwanda vingi vya silaha ni vyao.
Soko la silaha kwa mtu mmojammoja imeleta faida kwao sana kuacha ili soko ni hasara siyo rahisi kuliacha kirahisi
 
Asante sana Yoda na Aiba kwa kutupa elimu hii ya maisha ya USA na Changamoto zake. Kwa hiki kidogo lakini wengine sisi tumepata pakubwa. Big up sana.

Nadhani Diaspora wengine mliolowea huko jifunzeni hivi kutuhabarisha ndugu zenu tuzijue Siasa, Maisha na Changamoto za nchi mlizopo huku na SIO TU KUTURINGISHIA NA UJUAJI MWINGI
 
. Ughali wa huduma za matibabu na dawa sekta ya afya
Marekani ni taifa ambalo gharama za kila matibabu ziko juu na dawa zinauzwa ghali sana tofauti na kwingine duniani. Sekta ya afya ni mojawapo ya sekta zenye mzozo mkali sana katika siasa za hii nchi .Upande mmoja wa Democrats wakitaka udhibiti, usaidizi na ufadhili zaidi wa serikali kupitia bima na sheria na upande mwingine wa Republicans ukitaka biashara huria zaidi ambapo makampuni ya dawa, bima, hospitali na wateja wao ndio watakuwa na maamuzi yao makubwa zaidi ya kibinafsi.
Hua nachoka ilivo rahisi ku bail out taasisi za kifedha zilizofilisika kutokana na ulafi wa CEO's na wamiliki ila inakuwa ngumu kutoa bima ya afya kwa kila mmarekani
 
Sio kila Mmarekani anahitaji bima ya Afya ya Serikali. Labda ungesema kwa Wamarekani wanaohitaji.
Hua nachoka ilivo rahisi ku bail out taasisi za kifedha zilizofilisika kutokana na ulafi wa CEO's na wamiliki ila inakuwa ngumu kutoa bima ya afya kwa kila mmarekani
 
Ishu ya silaha ni ngumu sana na ata kama wataweka sheria ngumu bado umiliki wa silaha bila vibali itachukua nafasi
Republican inaongozwa na mabwanyenye sera zao nyingi ni kuwapendelea wao ata misimamo yao ni ile ya mlengo wa kutotaka mabadiliko mapya sababu yanawabe a wao na viwanda vingi vya silaha ni vyao.
Soko la silaha kwa mtu mmojammoja imeleta faida kwao sana kuacha ili soko ni hasara siyo rahisi kuliacha kirahisi
Inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom