BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
Miezi kadhaa iliyopita kuliibuka Watu waliokuwa wanakamata magari Jijini Dar es Salaam kwa wale ambao hawakuwa wamelipia ada za maegesho.
Kuliibuka usumbufu mkubwa kwa kuwa watu waliokuwa wakikamatwa walikutwa na madeni ya miaka ya nyuma ambayo hata wengine hawayajui au hawayakumbuki.
Mamlaka zikajitokeza kufafanua kuwa madeni hayo hayakulipwa kwa sababu za kimfumo, sikumbuki vizuri wao wenyewe wanajua walichokisema, hoja yangu ni kuwa usumbufu huo unaendelea na wahusika wengi hawajui madeni yao hali inayosababisha usumbufu kwa kiasi kikubwa.
Kwa sasa nimesikia kuwa mfumo huo wa madeni upo chini ya TAMISEMI, kama ni kweli kwa nini wasitume ujumbe kwa wale wanaodaiwa kwenye namba za simu kwa wahusika wenye magari.
Inawezekana wasifikiwe wote kwa kuwa wengine walishabadilisha namba za simu, waliuza magari, au hawana tena hayo magari kwa namna yoyote, lakini hii tabia ya kumsapraizi mtu kumwambia anadaiwa kisha ukamtaka alipe papo kwa hapo, haijakaa sawa.
Juzi nimekamatwa maeneo flani na hao wanaotoza malipo ya parking wakaniambia nilipe elfu 50 na kama sina salio basi niendelee kubaki nao hadi jioni, hivi hii ni sawa?
Hapo mimi nina nafuu kuna mwamba aliambiwa anadaiwa zaidi ya 200,000 akatakiwa kuilipa papo hapo, akasema hiyo gari aliinunua kwa mtu hakujua kama ina deni kubwa hivyo.
Hivyo, wito wangu kwa Serikali kutafuta namna ya kuwafikishia ujumbe wanaodaiwa hata kama ni kwa njia ya sms kwa kuwa madeni ni ya miaka ya nyumba, sio rahisi mtu kukumbuka na kuwa na gari haimaanishi wewe unatakiwa kutembea na hela nyingi muda wote.
Pia soma:
~ Wanaohusika kudai fedha za ‘parking’ kwa kusimamisha magari barabarani, wamekuwa kero kwa Wananchi!
~ TAMISEMI: Mfumo wa kusoma madeni ya parking ulipata hitilafu ukashindwa kutuma ujumbe kwa wenye magari
Kuliibuka usumbufu mkubwa kwa kuwa watu waliokuwa wakikamatwa walikutwa na madeni ya miaka ya nyuma ambayo hata wengine hawayajui au hawayakumbuki.
Mamlaka zikajitokeza kufafanua kuwa madeni hayo hayakulipwa kwa sababu za kimfumo, sikumbuki vizuri wao wenyewe wanajua walichokisema, hoja yangu ni kuwa usumbufu huo unaendelea na wahusika wengi hawajui madeni yao hali inayosababisha usumbufu kwa kiasi kikubwa.
Kwa sasa nimesikia kuwa mfumo huo wa madeni upo chini ya TAMISEMI, kama ni kweli kwa nini wasitume ujumbe kwa wale wanaodaiwa kwenye namba za simu kwa wahusika wenye magari.
Inawezekana wasifikiwe wote kwa kuwa wengine walishabadilisha namba za simu, waliuza magari, au hawana tena hayo magari kwa namna yoyote, lakini hii tabia ya kumsapraizi mtu kumwambia anadaiwa kisha ukamtaka alipe papo kwa hapo, haijakaa sawa.
Juzi nimekamatwa maeneo flani na hao wanaotoza malipo ya parking wakaniambia nilipe elfu 50 na kama sina salio basi niendelee kubaki nao hadi jioni, hivi hii ni sawa?
Hapo mimi nina nafuu kuna mwamba aliambiwa anadaiwa zaidi ya 200,000 akatakiwa kuilipa papo hapo, akasema hiyo gari aliinunua kwa mtu hakujua kama ina deni kubwa hivyo.
Hivyo, wito wangu kwa Serikali kutafuta namna ya kuwafikishia ujumbe wanaodaiwa hata kama ni kwa njia ya sms kwa kuwa madeni ni ya miaka ya nyumba, sio rahisi mtu kukumbuka na kuwa na gari haimaanishi wewe unatakiwa kutembea na hela nyingi muda wote.
Pia soma:
~ Wanaohusika kudai fedha za ‘parking’ kwa kusimamisha magari barabarani, wamekuwa kero kwa Wananchi!
~ TAMISEMI: Mfumo wa kusoma madeni ya parking ulipata hitilafu ukashindwa kutuma ujumbe kwa wenye magari