Mamlaka ya Ngorongoro badilisheli hili kwa Watalii

Mamlaka ya Ngorongoro badilisheli hili kwa Watalii

Hassanjk

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2023
Posts
333
Reaction score
689
Ili mgeni aweze kulala ndani ya eneo (mbuga) ya Ngorongoro kuna ada ya Serikali anatakiwa kulipa ambayo huitwa Camping fees (GRR).

Wanachofanya mamlaka ya Ngorongoro; Mgeni hata kama amelipia camping fees ya siku tano; akishindwa kuingia Ngorongoro kwa siku ya kwanza; mfano akaja siku ya pili hata kama ametoa taarifa; Hawamruhusu hadi alipe upya siku zote tano. Ukiuliza una ambiwa System hairuhusu kubadilisha

Watalii wanaona kama huu ni WIZI WA WAZI WAZI kwani hata kama Mamlaka hawajali changamoto za mtalii (kuumwa, kukosa ndege nk) wangemruhusu basi atumie camping ya siku zilizobakia tofauti na iliyo sasa

1. Naamini watu wa mamlaka wana elimu ya utalii (World Tourism Geography) mfano; Naamini wanajua kuwa hapo jirani tu Botswana kuna Caldera nzuri sana kuliko hii ya kwetu (Okavango Delta) na ipo well managed bila kuwa na longo longo...na watalii kule ni wengi sana....na hakuna purkushani. Mtalii akikumbana na hii kadhia hutusema vibaya akirudi kwao na kufanya malengo ya Mama kufikisha watalii Milioni tano kubakia ndoto tu......

2. Hapa kwetu Mtalii aliyelipa hela yake yote Mamlaka ; Kama atapata changamoto kama kuugua au ndege yake ya International kuchekewa siku moja, Muendesha watalii hadi kichwa kinauma; atadaije mgeni alipe tena hela ambayo haijatumika?

3. Nyongeza;
Kila mgeni anayelala ndani ya mamlaka lazima alipe kiingilio na malazi; najiuliza tu, hizi hela za Camping wanazopora kwa watalii waliopata changamoto, huwa zina wekwa kundi gani?

4. Pendekezo;
Mgeni akipata changamoto yoyote ya kumfanya ashindwe kuingia ndani ya mamlaka (ngorongoro); aruhusiwe kuitumia hela yake (camping) ndani ya siku 30.
 
Ni kweli kabisa.
NCAA wanaendesha biashara ya utalii kibabe sana.
Sijui wamesomea wapi?
Naona ubabaishaji mwingi sana.
Amendment ni kitu cha kawaida kwenye utalii.
 
Mgeni akienda Zimbabwe au Zambia harafu akaja Tanzania ni wachache sana wanaorudi hasa kwa madudu ya Ngorongoro ila Wasomi wetu wa Ngorongoro hawayaoni kabisaa..
 
Back
Top Bottom