Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Mamlaka nchini Kenya zimeyafuta Makanisa matano likiwemo kanisa la Mshukiwa aliyewachochea zaidi ya Waumini wake 400 kufunga hadi kufa.
Msajili wa Mashirika nchini humo katika notisi iliyowekwa kwenye gazeti la Taifa amesema leseni ya Muhubiri Paul Nthenge Mackenzie wa kanisa la Good News International Ministries ilifutiliwa mbali kuanzia Mei 19 huku kutokula kukionekana ndicho chanzo kikuu cha sehemu kubwa ya hao Watu 400 waliofariki Kanisani kwake japo ripoti za upasuaji zinaonyesha wengine wakiwemo Watoto walinyongwa, kupigwa au kubanwa pumzi hadi kufa.
Mamlaka zimeyafutilia mbali Makanisa mengine 4 pia likiwemo la New Life Prayer Centre and Church lake mhubiri Ezekiel Odero ambaye amehusishwa na Mackenzie na sasa anachunguzwa kwa mashtaka kadhaa yakiwemo mauaji, itikadi kali na utakatishaji fedha.
Msajili wa Mashirika nchini humo katika notisi iliyowekwa kwenye gazeti la Taifa amesema leseni ya Muhubiri Paul Nthenge Mackenzie wa kanisa la Good News International Ministries ilifutiliwa mbali kuanzia Mei 19 huku kutokula kukionekana ndicho chanzo kikuu cha sehemu kubwa ya hao Watu 400 waliofariki Kanisani kwake japo ripoti za upasuaji zinaonyesha wengine wakiwemo Watoto walinyongwa, kupigwa au kubanwa pumzi hadi kufa.
Mamlaka zimeyafutilia mbali Makanisa mengine 4 pia likiwemo la New Life Prayer Centre and Church lake mhubiri Ezekiel Odero ambaye amehusishwa na Mackenzie na sasa anachunguzwa kwa mashtaka kadhaa yakiwemo mauaji, itikadi kali na utakatishaji fedha.