Mamlaka yafuta makanisa matano Kenya

Mamlaka yafuta makanisa matano Kenya

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Mamlaka nchini Kenya zimeyafuta Makanisa matano likiwemo kanisa la Mshukiwa aliyewachochea zaidi ya Waumini wake 400 kufunga hadi kufa.

Msajili wa Mashirika nchini humo katika notisi iliyowekwa kwenye gazeti la Taifa amesema leseni ya Muhubiri Paul Nthenge Mackenzie wa kanisa la Good News International Ministries ilifutiliwa mbali kuanzia Mei 19 huku kutokula kukionekana ndicho chanzo kikuu cha sehemu kubwa ya hao Watu 400 waliofariki Kanisani kwake japo ripoti za upasuaji zinaonyesha wengine wakiwemo Watoto walinyongwa, kupigwa au kubanwa pumzi hadi kufa.

Mamlaka zimeyafutilia mbali Makanisa mengine 4 pia likiwemo la New Life Prayer Centre and Church lake mhubiri Ezekiel Odero ambaye amehusishwa na Mackenzie na sasa anachunguzwa kwa mashtaka kadhaa yakiwemo mauaji, itikadi kali na utakatishaji fedha.
 
Hivi kuna KKKT ya Kenya huko?
Waanze na hao.
 
Going to church and mosque is a wastage of time and Money.

Saidieni wenye shida mbalimbali hiyo inatosha.
Sisi Waislam hatufuati matamanio ya nafsi zetu. Sisi tumejisalimisha kwa Mola Muumba wa Kila Kitu. Na kwa kuwa tumejisalimisha kwake, hivyo tutamuabudu Mola kama anavyotaka Yeye na sio kama tunavyotaka sisi.

Mwisho, najua umeweka mosque hapo ili u balance, ndio maana hata nikikuuliza kwenda mosque kunapotezaje muda na pesa hutoweza kunijibu.
 
Sisi Waislam hatufuati matamanio ya nafsi zetu. Sisi tumejisalimisha kwa Mola Muumba wa Kila Kitu.
Wewe African na Uislam wapi na wapi?? Dini za wazungu na waarabu unazifanya kuwa zako?? Africans had their own ways of life before the coming of white men.
 
Wewe African na Uislam wapi na wapi?? Dini za wazungu na waarabu unazifanya kuwa zako?? Africans had their own ways of life before the coming of white men.
Kwanza Uislam haukuja kwa ajili ya wazungu au waarabu peke yao.

Pili, Uislam ndio Dini ya asili kwa MwanaAdamu. Dini ya asili ya wazungu, waafrika na waarabu na wengineo. Hivyo muafrika kurudi katika Uislam, ni amerudi katika asili yake.
 
Kwanza Uislam haukuja kwa ajili ya wazungu au waarabu peke yao.

Pili, Uislam ndio Dini ya asili kwa MwanaAdamu. Dini ya asili ya wazungu, waafrika na waarabu na wengineo. Hivyo muafrika kurudi katika Uislam, ni amerudi katika asili yake.
Brainwashed.
 
Kwanza Uislam haukuja kwa ajili ya wazungu au waarabu peke yao.

Pili, Uislam ndio Dini ya asili kwa MwanaAdamu. Dini ya asili ya wazungu, waafrika na waarabu na wengineo. Hivyo muafrika kurudi katika Uislam, ni amerudi katika asili yake.
Ni ujinga kusema Uislam ni dini ya asili, hata kwa wakristo it's clear ukristo ulikua wa wayahudi sema tu walivyomkataa Yesu ndio akasema ihubiriwe kwa Kila mtu ila hata ukisoma bible it's obvious ukristo ni huko uyahudini. Same to Islam, ni wa mashariki ya kati na ndio maana hizo dini zinaitwa Abrahamic religions maana ni za mashariki ya kati hapo.

Kama zilikua zetu Toka mwanzo kwanini hakuna nabii muafrika au story yoyote ya Uislam wa kiafrika??

Punguza kujikomba kwenye vitu vya waarabu unakifanya chako.
 
Back
Top Bottom