KERO Mamlaka za Serikali za Mitaa Chanika (Dar) zimeshindwa kusimamia ukusanyaji taka katika mitaa ya Gogo, Bondeni na Polisi

KERO Mamlaka za Serikali za Mitaa Chanika (Dar) zimeshindwa kusimamia ukusanyaji taka katika mitaa ya Gogo, Bondeni na Polisi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kwa takribani miezi mitano, Mzabuni aliyechukua tenda ya Ukusanyaji taka katika Mitaa ya Chanika ya Gogo, Bondeni na Polisi wameshindwa jukumu hilo, hakuna taarifa rasmi au maelezo kutoka Serikali za Mtaa kuhusiana na jambo hili!

Mzabuni huyu alijisifu sana kipindi alipokuwa akichukua tenda hii na kusababisha vijana waliokuwa wakifanya kazi hiyo awali kuondolewa, kwani Mzabuni huyu alijitangaza kama mtu mwenye pesa, vitendea kazi na uzoefu.

Matokeo yake ni takriban miezi mitano na pesa akichukua lakini utendaji umekuwa wa kiwango cha chini. Tunaomba Serikali iingilie kati jambo hili kunusuru afya zetu.

IMG-20241225-WA0030.jpg
 
Back
Top Bottom