GwaB
JF-Expert Member
- Mar 19, 2014
- 4,291
- 5,786
Mapato ya nchi hutegemea ukusanyaji wa kodi kutoka kwa wingi wa watu binafsi au kutoka kwenye faida ya mashirika na makampuni yaliyojiandikisha kwa lengo la kufanya biashara. Kwa miaka mingi sana Tanzania imekuwa ikitegemea kodi zinazokusanywa kutoka kwa wafanyakazi walioko kwenye mfumo ulio rasmi na baadhi ya wafanyabiashara wachache binafsi. Ni hivi karibuni tu kumekuwa na mwelekeo wa kupanua wigo wa walipa kodi kwa kuihusisha sekta isiyo rasmi ili ichangie ipasavyo katika mapato ya nchi.
Pamoja na nia njema ya serikali kuongeza idadi ya walipa kodi kwa kuruhusu watu kufanya biashara ni vyema serikali ikapitia upya huu mfumo wa utoaji leseni na vibali hasa kwenye biashara za kitaaluma. Kwa hali ya kawaida biashara zisizohitaji vibali hulipa ada kwa ajili ya leseni ya kufanya biashara ambayo iko kwenye TSH 70,000 kwa mwaka. Kwa biashara zinazohitaji vibali vya kitaaluma, pamoja na kulipia TSH 70,000 za leseni bado mfanyabiashara anatakiwa kulipia TSH 50,000 kwa ajili ya kibali cha kufanya biashara za kitaaluma.
Kwa mfano nilioutoa hapo juu, inaonyesha wazi kuwa mfanyabiashara anayewekeza kwenye biashara zinazohitaji vibali vya kitaaluma gharama zake zinakua juu zaidi na kupunguza kiwango cha uwekezaji kwenye mradi husika. Tozo na ada ya vibali ni kikwazo katika biashara napendekeza ufanyike utaratibu wa mamlaka za udhibiti kuchukua mgao kwenye leseni kuu za biashara.
Mamlaka za udhibiti huundwa kwa sheria zinazotungwa kwenye bunge letu, pamoja na uundwaji wake huo ni muhimu kuangalia kama mwelekeo wa sheria za usimamizi ziwe na lengo la kuwezesha biashara kushamiri na baadaye kulipa kodi na sio kukwamisha biashara zinazoanzishwa kwa gharama kubwa.
Pamoja na nia njema ya serikali kuongeza idadi ya walipa kodi kwa kuruhusu watu kufanya biashara ni vyema serikali ikapitia upya huu mfumo wa utoaji leseni na vibali hasa kwenye biashara za kitaaluma. Kwa hali ya kawaida biashara zisizohitaji vibali hulipa ada kwa ajili ya leseni ya kufanya biashara ambayo iko kwenye TSH 70,000 kwa mwaka. Kwa biashara zinazohitaji vibali vya kitaaluma, pamoja na kulipia TSH 70,000 za leseni bado mfanyabiashara anatakiwa kulipia TSH 50,000 kwa ajili ya kibali cha kufanya biashara za kitaaluma.
Kwa mfano nilioutoa hapo juu, inaonyesha wazi kuwa mfanyabiashara anayewekeza kwenye biashara zinazohitaji vibali vya kitaaluma gharama zake zinakua juu zaidi na kupunguza kiwango cha uwekezaji kwenye mradi husika. Tozo na ada ya vibali ni kikwazo katika biashara napendekeza ufanyike utaratibu wa mamlaka za udhibiti kuchukua mgao kwenye leseni kuu za biashara.
Mamlaka za udhibiti huundwa kwa sheria zinazotungwa kwenye bunge letu, pamoja na uundwaji wake huo ni muhimu kuangalia kama mwelekeo wa sheria za usimamizi ziwe na lengo la kuwezesha biashara kushamiri na baadaye kulipa kodi na sio kukwamisha biashara zinazoanzishwa kwa gharama kubwa.