Mamlaka za vyombo vya majini Zanzibar na Bara, msipochukua tahadhari Watanzania watalia hapo mbele

Mamlaka za vyombo vya majini Zanzibar na Bara, msipochukua tahadhari Watanzania watalia hapo mbele

Ze burner

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
514
Reaction score
83
Leo tarehe 20.12.2020 muda huu naandika nikiwa katika chombo cha Zan Fast Ferry (Zanzibar 2) tulitaraji kuondoka majira ya saa 10.15 jioni kwa mujibu wa ticket zetu ila katika hali isiyotarajiwa tumeondoka saa 10.55 jioni baada ya kupigwa na joto kali hatqri huku watoto wakipiga kelele kwa maumivu ya joto hilo.

Cha kushangaza saa, kabla ya chombo hicho kuondoka alikuja mmoja kati ya watumishi wa kampuni hiyo akiwa ndani ya uniform ya tshirt na kutangaza yafuatayo "naomba niwaeleza kwamba madust ya taka yapo mbele hiyo ni vema kuacha boti ikiwa hali ya usafi" Mpaka hapo nilimuona jamaa ana akili kweli hadi alipokuja na tangazo la pili "mnajui boti ya Kilimanjaro imetangulia kuondoka ila siyo tatizo, japo tuchelewa kidogo ndani ya dakika 15 tutakua tumeipita" hapa kwa kweli kanipoteza.

Badala ya kuomba msamaha kwa kutuchelewesha kwa takriban dakika 40 anakuja kusema "japokua tumechelewa kidog" halafu angalau angekua na lengo la kuomba radhi kama ilivyo kwa waungwana anakuja anasema " hakuna shida Kilimanjaro tutaipita ndani dakika 15" abiria wote tuliomsikia tukaanza minongono kama kwamba hakuna aliyemwelewa kabisa.

Kwa kitendo cha kuchelewa sina tatizo nacho yaweza kuwa xilikuwepo sababu za msingi japo wao hawakuzisema. Tatizo ni zile kauli za kushindana wakati hatukua ktk mashindano. Leo tumefika salama ila naamini iko siku Mungu aepushie mbali tutakuja alaumiana km vile hakuna aliyekua akijua ama akiona kinachoendelea.

Nqshauri, km ilivyo kwa mamlaka ya Latra kuweka time table ya kutoka na kuingia mabasi kwenye vituo mbali mbali, ni Vyema pia mamlaka husika ziweke ratiba ya kuondoka na kufika kuliko kutegemea uwexo wa chombo husika kuamua muda wa kufika.
 
Hizi Zan Ferries ingekua huku nchi kavu tungezifananisha na SAULI, au KISBO KANGI LUGOLA. Boti zinamwage moto balaa.

Cha muhimu zile safety rules zote wazizingatie tu.
 
Huduma kwa wateja kwa hp Tz... Bado Ina changamoto kubwa.

Wengi wanaongea na wateja kauli zao Ni mbovu kupita kuvumilika, ubunifu hakuna...
 
Sasa kwanini msimuulize,hizo mbio za kuipita boti ya Kilimanjaro zina umuhimu gani?.na kwanini muingie katika mashindano yasiyowahusu?
 
Hizi Zan Ferries ingekua huku nchi kavu tungezifananisha na SAULI, au KISBO KANGI LUGOLA. Boti zinamwage moto balaa.

Cha muhimu zile safety rules zote wazizingatie tu.
Hizi Zan Ferries ingekua huku nchi kavu tungezifananisha na SAULI, au KISBO KANGI LUGOLA. Boti zinamwage moto balaa.

Cha muhimu zile safety rules zote wazizingatie tu.
Waliaza vzr wakidhani mbio zao ndo kila kitu ila leo ndo nimegundua kumbe hata abiria hawafurahishwi nqzo. Ni kwamba tu walichoka dharau za Azam na watu wake
 
Sasa kwanini msimuulize,hizo mbio za kuipita boti ya Kilimanjaro zina umuhimu gani?.na kwanini muingie katika mashindano yasiyowahusu?
Nilichokiona watu wote walimdharau kwa maneno yake ya kipuuxi wakabaki wakijadiliana wao kwa wao. Ingekua ni km kumuuliza kichaa
 
MKUU NATUMAINI UMEFIKA SALAMA KABISA,SWALI NI KWAMBA JE KILIMANJARO MLIIPITA?
 
anasema " hakuna shida kilimanjaro tutaipita ndani dakika 15" abiria wote tuliomsikia tukaanza minongono kama kwamba hakuna aliyemwelewa kabisa.
Engine Horsepower na knots speed kubwa ndiyo hupelekea kasi ya chombo na hii haimaanishi ni mwendo hatari.

Labda iwe bahari imechafuka, upepo mkali na mawimbi makubwa kupita kiasi ndipo nahodha wa chombo akaamua kukiondoa chombo bila kuzingatia hali ya bahari hapo ndipo tunaweza kusema ni hatari lakini suala la kukipita kasi chombo kingine wakati bahari ni shwari hilo silo tatizo la kiusalama ni nguvu ya engine horsepower na kasi ya knots ngapi chombo kinaweza kwenda.
 

World's Fastest Ship: Incat's Wave Piercing Catamaran


Built at Incat's shipyards in Hobart, Tasmania, this is the world's fastest ship. With a cargo of over 1,000 passengers and 150 cars, the 99-meter catamaran can travel at speeds of up to 58 knots or 107 km per hour. Its new owner, Buquebus Ferries, has named it 'Francisco' in honour of Argentinean-born Pope Francis.
Jul 2013
Built at Incat's shipyards in Hobart, Tasmania, this is the world's fastest ship. With a cargo of over 1,000 passengers and 150 cars, the 99-meter catamaran can travel at speeds of up to 58 knots or 107 km per hour. Its new owner, Buquebus Ferries, has named it 'Francisco' in honour of Argentinean-born Pope Francis.
 
Kwanini chombo cha baharini kinaweza kuwa na kasi ndogo ?

Why Ships are Slow?

marineinsight


Have you ever wondered why ships are so slow? There are several factors affecting the ship speed in the sea which makes the massive cargo ship slow. Two important factors which are explained in this video are Power to Weight Ratio and Ship Resistance. You will also learn how ship speed is calculated onboard ship and the unit of the ship speed. This video explains different techniques which are used today to measure the ship speed including the ship GPS system. We will also see how the ancient seafarers used to measure the speed of the ship without any electronic instruments, as done in today's world. Different types of ships have different service speeds. Bulk Carriers – 13 to 15 knots Container Ships – 16 to 24 knots Oil and chemical tankers – 13 to 17 knots RORO vessels – 16 to 22 knots Cruise Ships – 20 to 25 knots Different types of ships have different drafts, different cargo, different design and hence accordingly different service speed.

 
Changamoto za hali ya bahari, ukubwa wa mawimbi, kasi ya upepo unaovuma, kipimajoto cha hali ya hewa , msongamano wa vyombo vya baharini ktk eneo meli inapokatiza na mwendo wa chombo yote kwa umoja wake dhidi ya usalama wa jumla

 
Kwa kitendo cha kuchelewa sina tatizo nacho yaweza kuwa xilikuwepo sababu za msingi japo wao hawakuzisema.
Vyombo vya habari redio na televisheni viwe vinarusha utabiri mahususi kuhusu bahari na maziwa makuu ya Victoria, Tanganyika na Nyasa. Wenzetu hufanya hivyo ili kuwapa taarifa wasafiri na waendesha vyombo bahari / ziwani pamoja na wavuvi kuelewa usalama wao kila siku.

Utabiri hali ya bahari ukanda wa Marekani na visiwa vya Karibi.

 
Back
Top Bottom