Mamlaka zinapotumika kukandamiza watu

Mamlaka zinapotumika kukandamiza watu

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kuna hiki kinachoitwa ungamo. Kwamba mtuhumiwa wa wizi, ugaidi, mauaji nk; kwamba kwa hiari yake aliungama. Kutokea hapo mtu au watu wakahukumiwa kunyongwa au hata kufungwa.

Kesi hii:

Maelezo kukiri kosa yalivyowaunganisha washtakiwa-11

Ni mwendelezo wa maungamo uchwara kama hayo kupewa umuhimu.

Hivi ni kwa kumdanganya nani vile?

Tuliwasikia akina Adamoo walivyolazimishwa kuweka sahihi zao kwenye yaliyoitwa maungamo. Bila shaka huku ndiko walikopotelea kina Lijenje

Kwanini haya maungamo viini macho yanaendekezwa tu na hata kuwa sasa ndiyo haswa ulio uthipitisho wa tuhuma zenyewe?

Kulikoni kutokutumika ushahidi wenye kuaminika kama ule wa ma CCTV, mienendo ya simu yenye kutumia teknolojia nk, zenye kueleweka hata kwao mabeberu? Kwanini ni nia ya serikali kuona kuwa haki za watu zinapotea tu pasipo na kujali?

Kwani ufwedhuli maana yake nini?

Kulikuwa na maslahi gani kwenye kuwabambikizia akina Adamoo maelezo ya uongo Ili kupata kuwatia hatiani kiharamu? Kuna maslahi gani kwenye kuwabambikizia watuhumiwa wowote maungamo yasiyokuwa ya kweli?

Tunahitaji nchi ambapo sekta zote za utawala zitakuwa ni wezeshi. Tunahitaji haki. Hatuhitaji sekta kandamizi.

Mifano iko mingi. Fikiria pia Polisi, TRA, LATRA, EWURA, NIDA, TANROADS, Uhamiaji, nk nk.

Ni wapi kuna nafuu?
 
Hiki kiapo kuwepo kisheria wakati mwingine hutumika vibaya, naona kuna wakati mamlaka husika huamua kutumia excessive force kwa kuwalazimisha watuhumiwa wakubali makosa yao ili kuokoa muda, ni kama kinazibana mamlaka kisheria.

Hili hufanyika kwa sababu pia, kama watuhumiwa wataonekana kukaa mahabusu muda mrefu kabla ya ushahidi kukamilika ili wapelekwe mahakamani, basi jamii itaanza kupiga kelele wanashikiliwa kinyume cha sheria.

Hapo unakuta ndio kiini cha chimbuko la watuhumiwa kulazimishwa kukiri makosa kinyume na mapenzi yao, suluhisho la hili naona panahitajika watu kukaa chini.

Waangalie ni njia gani nzuri ya kuwafanya watuhumiwa wakiri makosa kwa mapenzi yao bila kushurutishwa kwa vitisho au vipigo, lakini pia, at the same time, wasikae muda muda mrefu mahabusu kinyume cha sheria.
 
Hiki kiapo kuwepo kisheria wakati mwingine hutumika vibaya, naona kuna wakati mamlaka husika huamua kutumia excessive force kwa kuwalazimisha watuhumiwa wakubali makosa yao ili kuokoa muda, ni kama kinazibana mamlaka kisheria.

Hili hufanyika kwa sababu pia, kama watuhumiwa wataonekana kukaa mahabusu muda mrefu kabla ya ushahidi kukamilika ili wapelekwe mahakamani, basi jamii itaanza kupiga kelele wanashikiliwa kinyume cha sheria.

Hapo unakuta ndio kiini cha chimbuko la watuhumiwa kulazimishwa kukiri makosa kinyume na mapenzi yao, suluhisho la hili naona panahitajika watu kukaa chini.

Waangalie ni njia gani nzuri ya kuwafanya watuhumiwa wakiri makosa kwa mapenzi yao bila kushurutishwa kwa vitisho au vipigo, lakini pia, at the same time, wasikae muda muda mrefu mahabusu kinyume cha sheria.

Hayupo mhalifu au mtuhumiwa mtu mzima anayeweza kuungama eti kwa kufanya uhalifu.

Maungamo yote tunayoyasikia ni maungamo viini macho ambayo takribani watuhumiwa wote huyakana mahakamani.

Ajabu na kweli ni kuwa takribani maungamo yote hukubaliwa kama halali na mahakama za kwetu.

Nani asiyejua uwepo wa vifo, vipigo vikali achilia mbali mateso na vitisho kwenyekuwataka watuhumiwa kukubaliana na tuhuma Ili yaishe?

Yupo kwenye rekodi bwana yule akumtamkia mtuhumiwa: "safari hii hauchomoki."

Ushahidi magumashi yakiwamo maungamo uchwara, unastahili kupigwa vita sasa hata kama ni wazi kuwa hautakuwa na nafasi kwenye serikali za watu, zozote zijazo.
 
Kuna hiki kinachoitwa ungamo. Kwamba mtuhumiwa wa wizi, ugaidi, mauaji nk; kwamba kwa hiari yake aliungama. Kutokea hapo mtu au watu wakahukumiwa kunyongwa au hata kufungwa.

Kesi hii:

Matajiri waliofadhili mauaji ya Lotter- 10

Ni mwendelezo wa maungamo uchwara kama hayo kupewa umuhimu.

Hivi ni kwa kumdanganya nani vile?

Tuliwasikia akina Adamoo walivyolazimishwa kuweka sahihi zao kwenye yaliyoitwa maungamo. Bila shaka huku ndiko walikopotelea kina Lijenje

Kwanini haya maungamo viini macho yanaendekezwa tu na hata kuwa sasa ndiyo haswa ulio uthipitisho wa tuhuma zenyewe?

Kulikoni kutokutumika ushahidi wenye kuaminika kama ule wa ma CCTV, mienendo ya simu yenye kutumia teknolojia nk, zenye kueleweka hata kwao mabeberu? Kwanini ni nia ya serikali kuona kuwa haki za watu zinapotea tu pasipo na kujali?

Kwani ufwedhuli maana yake nini?

Kulikuwa na maslahi gani kwenye kuwabambikizia akina Adamoo maelezo ya uongo Ili kupata kuwatia hatiani kiharamu? Kuna maslahi gani kwenye kuwabambikizia watuhumiwa wowote maungamo yasiyokuwa ya kweli?

Tunahitaji nchi ambapo sekta zote za utawala zitakuwa ni wezeshi. Tunahitaji haki. Hatuhitaji sekta kandamizi.

Mifano iko mingi. Fikiria pia Polisi, TRA, LATRA, EWURA, NIDA, TANROADS, Uhamiaji, nk nk.

Ni wapi kuna nafuu?
Hili tatizo ni kweli lipo. Kiini chake ni kuiga jambo bila kuwa na utamaduni wa jambo lenyewe. Kule Latin Amerika wenzetu walidhani kuwa wakiwa na Katiba na sheria kama za Marekani ni tosha kuwaletea maendeleo kama ilivyo Marekani. Baada ya muda waligundia kuwa Katiba na sheria lazima viendane na kiwango fulani cha ustaarabu unaoibeba Katiba na sheria mpya. Na ungamo la jinai hivyo hivyo. Kwa mfano, Marekani mtu akiungama kuwa kaua, hilo ungamo peke yake halitoshi kumtia hatiani. Vyombo vya usalama lazima vipitie ungamo lake na kupata ushahidi wa kimahakama; faida ya ungamo hapo ni kwamba mhusika atawaelekeza polisi kwenye ushahidi, kama silaha iliyotumika, iko wapi nk. ambao utaletwa mahakamani na kesi kuamliwa.
 
Hili tatizo ni kweli lipo. Kiini chake ni kuiga jambo bila kuwa na utamaduni wa jambo lenyewe. Kule Latin Amerika wenzetu walidhani kuwa wakiwa na Katiba na sheria kama za Marekani ni tosha kuwaletea maendeleo kama ilivyo Marekani. Baada ya muda waligundia kuwa Katiba na sheria lazima viendane na kiwango fulani cha ustaarabu unaoibeba Katiba na sheria mpya. Na ungamo la jinai hivyo hivyo. Kwa mfano, Marekani mtu akiungama kuwa kaua, hilo ungamo peke yake halitoshi kumtia hatiani. Vyombo vya usalama lazima vipitie ungamo lake na kupata ushahidi wa kimahakama; faida ya ungamo hapo ni kwamba mhusika atawaelekeza polisi kwenye ushahidi, kama silaha iliyotumika, iko wapi nk. ambao utaletwa mahakamani na kesi kuamliwa.

Faida ya ungamo haipo kwani hakuna ungamo la hiari bali ni zao la vipigo na mateso ambayo mahakamani mtuhumiwa huyakana.

Tuliambiwa mmoja wa watuhumiwa pale Lau madukani alikiri kukutwa na silaha (Luger A5340) na kete kadhaa za madawa ya kulevya lakini bado alikana kata kata mahakamani.

Kumbuka mahakama ililikibali ungamo hilo kama ushahidi halali dhidi yake hali mtuhumiwa mwenyewe akilikana.

Kwa mwendelezo huu ni sahihi kudhani mamlaka zimejiwekea namna ya kuhalalisha hatma bila ya kujali ukweli. Kwamba mamlaka zikiamua kwa lolote hata kama ni la kidhwalimu mwananchi hutoboi.

Kimsingi ni kuwa mamlaka kama hizi hazitufai na pia hatuzitaki.
 
Kuna hiki kinachoitwa ungamo. Kwamba mtuhumiwa wa wizi, ugaidi, mauaji nk; kwamba kwa hiari yake aliungama. Kutokea hapo mtu au watu wakahukumiwa kunyongwa au hata kufungwa.

Kesi hii:

Matajiri waliofadhili mauaji ya Lotter- 10

Ni mwendelezo wa maungamo uchwara kama hayo kupewa umuhimu.

Hivi ni kwa kumdanganya nani vile?

Tuliwasikia akina Adamoo walivyolazimishwa kuweka sahihi zao kwenye yaliyoitwa maungamo. Bila shaka huku ndiko walikopotelea kina Lijenje

Kwanini haya maungamo viini macho yanaendekezwa tu na hata kuwa sasa ndiyo haswa ulio uthipitisho wa tuhuma zenyewe?

Kulikoni kutokutumika ushahidi wenye kuaminika kama ule wa ma CCTV, mienendo ya simu yenye kutumia teknolojia nk, zenye kueleweka hata kwao mabeberu? Kwanini ni nia ya serikali kuona kuwa haki za watu zinapotea tu pasipo na kujali?

Kwani ufwedhuli maana yake nini?

Kulikuwa na maslahi gani kwenye kuwabambikizia akina Adamoo maelezo ya uongo Ili kupata kuwatia hatiani kiharamu? Kuna maslahi gani kwenye kuwabambikizia watuhumiwa wowote maungamo yasiyokuwa ya kweli?

Tunahitaji nchi ambapo sekta zote za utawala zitakuwa ni wezeshi. Tunahitaji haki. Hatuhitaji sekta kandamizi.

Mifano iko mingi. Fikiria pia Polisi, TRA, LATRA, EWURA, NIDA, TANROADS, Uhamiaji, nk nk.

Ni wapi kuna nafuu?
Eti mtu anakiri kwa hiari akiwa polisi akifika mahakamani kwanini akane? hata mahakimu huwa ni wajinga sn
 
Faida ya ungamo haipo kwani hakuna ungamo la hiari bali ni zao la vipigo na mateso ambayo mahakamani mtuhumiwa huyakana.

Tuliambiwa mmoja wa watuhumiwa pale Lau madukani alikiri kukutwa na silaha (Luger A5340) na kete kadhaa za madawa ya kulevya lakini bado alikana kata kata mahakamani.

Kumbuka mahakama ililikibali ungamo hilo kama ushahidi halali dhidi yake hali mtuhumiwa mwenyewe akilikana.

Kwa mwendelezo huu ni sahihi kudhani mamlaka zimejiwekea namna ya kuhalalisha hatma bila ya kujali ukweli. Kwamba mamlaka zikiamua kwa lolote hata kama ni la kidhwalimu mwananchi hutoboi.

Kimsingi ni kuwa mamlaka kama hizi hazitufai na pia hatuzitaki.
Hakuna ungamo zaidi ya vipigo
 
Hili tatizo ni kweli lipo. Kiini chake ni kuiga jambo bila kuwa na utamaduni wa jambo lenyewe. Kule Latin Amerika wenzetu walidhani kuwa wakiwa na Katiba na sheria kama za Marekani ni tosha kuwaletea maendeleo kama ilivyo Marekani. Baada ya muda waligundia kuwa Katiba na sheria lazima viendane na kiwango fulani cha ustaarabu unaoibeba Katiba na sheria mpya. Na ungamo la jinai hivyo hivyo. Kwa mfano, Marekani mtu akiungama kuwa kaua, hilo ungamo peke yake halitoshi kumtia hatiani. Vyombo vya usalama lazima vipitie ungamo lake na kupata ushahidi wa kimahakama; faida ya ungamo hapo ni kwamba mhusika atawaelekeza polisi kwenye ushahidi, kama silaha iliyotumika, iko wapi nk. ambao utaletwa mahakamani na kesi kuamliwa.
Huku watu wanabambikwa unaweza kuwekewa hata bomu nyumbani kwako? angalia walipeleka kichwa cha binadamu kwa Professor Arusha tena mtoto wake ni wakili wakapewa milioni 90, je bado utawaamini hao polisi?
 
Hayupo mhalifu au mtuhumiwa mtu mzima anayeweza kuungama eti kwa kufanya uhalifu.

Maungamo yote tunayoyasikia ni maungamo viini macho ambayo takribani watuhumiwa wote huyakana mahakamani.

Ajabu na kweli ni kuwa takribani maungamo yote hukubaliwa kama halali na mahakama za kwetu.

Nani asiyejua uwepo wa vifo, vipigo vikali achilia mbali mateso na vitisho kwenyekuwataka watuhumiwa kukubaliana na tuhuma Ili yaishe?

Yupo kwenye rekodi bwana yule akumtamkia mtuhumiwa: "safari hii hauchomoki."

Ushahidi magumashi yakiwamo maungamo uchwara, unastahili kupigwa vita sasa hata kama ni wazi kuwa hautakuwa na nafasi kwenye serikali za watu, zozote zijazo.
Tuna polisi ya hovyo kabisa hapa Tanzania
 
Tuna polisi ya hovyo kabisa hapa Tanzania

Tuna mamlaka za hovyo sana. NInakazia:

"Mifano iko mingi. Fikiria pia Polisi, TRA, LATRA, EWURA, NIDA, TANROADS, Uhamiaji, nk nk.

Ni wapi kuna nafuu?"

Ubora wetu ni kwenye upuusi zaidi si katika lolote lenye tija:

 
Back
Top Bottom