Mamlaka zinazohusika ziangalie Mbwa wanaozagaa Mitaani bila uangalizi maalum, wanaweza kuwahatarishi kwa Watu

Mamlaka zinazohusika ziangalie Mbwa wanaozagaa Mitaani bila uangalizi maalum, wanaweza kuwahatarishi kwa Watu

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257


Imekuwa kawaida kuona wanyama mbalimbali hasa wale ambao wanaonekana hawana madhara ya mara kwa mara kwa Watu wakiwa mitaani hawana muelekeo, lakini inapotokea Wanyama hao wanaanza kusababisha madhara ndipo ambapo Mamlaka zinaibuka kuanza kuchukua hatua.

Mfano huku mitaa ya kwetu huku Dodoma kumekuwa na ongezeko la mbwa wanaozunguka wakionekana kutokuwa na wamiliki kwa baadhi ya mitaa ikiwemo Mtaa wa Relini.

Ni mbwa ambao wamekuwa na tabia ya kukaa kwenye njia wanazopita mitaani muda mwingi, na wakati mwingine wamekuwa na tabia ya kukimbiza Watu wanaopita kwenye njia hizo.

Wiki iliyopita majira ya saa moja asubuhi, nikiwa ndani nilisikia sauti mtoto akilia sana, baada ya kutoka nje na kuzunguka nje ya nyumba nilimkuta mtoto wa jirani ndiye anayelia baada ya kukimbizwa na mbwa wawili, hali iliyosababisha kudondoka na kuumia mgongo, huku watu wakiwakimbiza mbwa wale.

Si huyu tu, mmoja wa madereva bodaboda anasema mbwa hao wamekuwa na tabia hiyo kwa Watu wanaopita, naye ni miongoni mwa waliopitia adha hiyo wakati fulani. Kuna kipindi hapa waliwapiga risasi mbwa, ila kuna mbwa jike alibaki ndiye aliwazaa hawa mbwa.

Ni zaidi ya mbwa Watano hupenda kukaa njia majira ya asubuhi na jioni. Nitoe wito kwa Mamlaka mbalimbali zinazohusika zichukue hatua mapema kabla ya madhara hayajatokea kwa Watu.

Ni jambo la nadra kuona katika Nchi za wenzetu zilizoendelea kuona Mbwa wakiwa mitaani hawana muongozo kwa kuwa, inapotokea hawana chanjo wakimng'ata mtu wanaweza kusababisha magonjwa lakini pia uwepo wao sehemu mbalimbali kama wana vijidudu au magonjwa wanaweza kuwa na athari kubwa.
 
Matumizi mabaya ya mtandao shida ndogo za mtaani kwako unashindwa kumpelekea mwenyekiti wa mtaa, mtendaji wa mtaa afisa Mifugo wa mtaa na wakat mwingne mna diwan, mna mkurugenzi wa mji hao wote umeshindwa kwenda kuwashitakia ad ulete habari ndogo hii kwa jamii nzima ya watanzania

Ama ujui ofisi za kata kuna kila kitengo pale nenda ukashitaki utapata msaada
 
Waende Iringa walete wahehe Dodoma,week moja tu jiji linakuwa safi
 
Ujumbe huu ungekuwa umeandikwa na mtu aliyeko Dar,,,, tungesikia mengi.
 
Inatuma ujumbe kuwa ulinzi umeimarika Dodoma au wizi majumbani umepungua, mbwa hawana thamani kwa sasa.
 
Back
Top Bottom