Man Fongo: Ipo siku nitarudi uswahilini kuimba kwenye vigodoro.

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506


Msanii wa muziki singeli Man Fongo amesema anakumbuka alipoanzia muziki wake kwa kuimba nyimbo za vigodoro uswahili na ipo siku atarudi uswahilini kuwaimbia mashabiki zake.

Akiongea kupitia eNewz amesema singeli ni muziki wa watu masikini na watu wa hali ya chini na umetokea uswahilini.

Amesema anakumbuka mwanzo alipokuwa akiimba uswahilini alikuwa analipwa hela ndogo hadi elfu ishirini pia kulikuwa na misukosuko mingi ikiwemo kushikiwa mapanga na kuwekewa mawe aimbe hadi asubuhi.

Hata hivyo Man Fongo anasema zamani alipokuwa anaimba muziki wa singeli alikuwa anakuwa na watu mbalimbali wa uswahilini waliokuwa wakimfuata nyuma hali iliyopelekea mpaka watu kuhisi kwamba ni vijana wa panya road japo walikuwa mashabiki.

Mambo hayo amesema akiyakumbuka anatamani siku hiyo ifike arudi uswahilini na kuendeleza show zake za kwenye vigodoro.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…