Elections 2010 Manabii Wa Uongo

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2010
Posts
10,827
Reaction score
4,176
Hakika mambo yote yatapita lakini Neno litasimama.

Imeandikwa "Siku za mwisho wataibuka manabii wa uongo"

Hivi karibuni, kwenye moja ya mikutano ya kampeni ya JK aliibuka msanii mmoja na kujitambulisha kuwa yeye ni Mchungaji na kuanza kujinasibu mbele ya kipaza sauti na kamera za TBC kuwa JK ni Chaguo la Mungu. Hatudanganyiki.

Kama hiyo haitoshi, hivi leo, Mchungaji Sylvester Gamanywa (na Sheikh mmoja) ameingia katika orodha ya watu wanaotumiwana JK kwa kuwasihi watu wasichague mtu kwa hisia za udini.

Swali:

Hawa manabii wa uongo (Gamanywa na wenzake wanaojipendekeza), wameuona Waraka wa Waislamu? Wasitughilibu. Tumechoka.

Nitamchagua Slaa kwa hisia zozote.

Wala sihitaji Mchungaji kunielekeza kuwa JK hafai tena kuiongoza Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…