Manara na Simba yake

Mamserenger

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2019
Posts
1,156
Reaction score
2,092
Wale wana wa Msimbazi poleni sana kwa kipigo pale kwa Mkapa.

Kuondoka kwa Haji Manara kweli kunaonesha kabisa kuna Nguzo moja imevunjika pale Msimbazi.
Namkumbuka sana Manara mechi kama hizi kabla hazija anza week moja kabla zinapigiwa promo sana.

Manara alikuwa anazitangaza na sisi mashabiki kweli tulikuwa tunajaa uwanjani.

Lakini sasa hivi tumewaleta wamasishaji hawa kina Mwijaku na mwenzie Mziwanda mechi hazija anza badala kuwa amasisha watu kuwatia Morali wachezaji wao wanakuja na kuponda watangulizi na hata kutoa Lugha na ahadi za kufedhea. Wao wanazani Brand ya Simba imejengwa kwa mdomo mwingi na ahadi za kisengerenyuma.

Any way hata Babra CEO wa Simba nae huwa ana hulka za kimwanamke hasa kuchagua wale wa pashaji ambao kwakweli asee sio watu wa ma hala pale.Wanaongozwa tuu na hulka za Mipasho Majungu na upuuzi.CEO Akiamini Simba ikiwa na pesa za kutosha.Basi makombe yote mpaka ya Ligi atachukua yeye.

Kwa Sasa Simba hatuna tena ule umoja wa Viongozi wachezaji pamoja na Mashabiki chanzo kikubwa ni ile Press ya Manara kueleza ukweli alio kuwa anafanyiwa pale Simba na ma boss wakubwa ambao huwezi kuwa dhania kabisa.Na yeye akiondoka lihali bado anaipenda Simba.

Sasa wale wanazi walio itunza Simba na walio pambania hawapo wamekaa pembeni

Simba ya Sasa ni ya Kina Mwijaku na Badra Mo
Hakika tusha potea kwenye ramani yoteee

Ila narudia tena Sumu ni ile Press ya Manara kufunua uwozo wote alio kuwa anafanyiwa na Ma Boss wake Mo pamoja na Badra.

Asansteni
Mamserenger

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Skia nikwambie, baada ya Mwamedi kushindwa kumpa mimba babla , akaona ampe Simba.

#ova
 
Manara hana lolote!! Angekuwa na lolote angeenda na hilo lolote yanga na tungeliona!! Ameangukia pua mechi ya kwanza tu ya mchujo!!
 
Manara hana lolote!! Angekuwa na lolote angeenda na hilo lolote yanga na tungeliona!! Ameangukia pua mechi ya kwanza tu ya mchujo!!
Yanga hawakuwa na mpango wa kucheza CAFCL. Lengo ni kuchukua kombe la ligi kuu msimu huu hapa nyumbani.
 
Manara hana lolote!! Angekuwa na lolote angeenda na hilo lolote yanga na tungeliona!! Ameangukia pua mechi ya kwanza tu ya mchujo!!
Kweli unacho kiona.

Ila Manara tangy aondoke Simba mpaka asaivi hatueleweki kufikia hatua ya kuwaamini kina Mwijaku.

Manara kwa kuhamasisha kwake aliweza kuwaunganisha mashabiki wachezaji na viongozi.Mechi kama hizi ilikuwa Do or Die
 
Kwani mashabiki hawajajaa maana caf walitaka 15000 tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…