Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Hali hiyo imeyeyusha kabisa ndoto za Klabu hiyo kwa wakati huu wa miaka ya hivi karibuni kuwa na uwanja wa kisasa ambao ulikusudiwa kujengwa katika eneo hilo.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa;
"Sijawahi kumdhihaki yeyote aliye katika mitihani coz siijui kesho yangu. Ila sitaacha kusema, Uwanja mliotutambia umeota mbawa, haya rudini bondeni mkahangaike na magugu maji", aliandika Manara.
Klabu ya Yanga ilikabidhiwa eneo hilo katika hafla iliyohudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba pamoja na Mke wa Rais wa kwanza wa Zanzibar hayati Sheikh Abeid Amani Karume, Mama Fatma Karume ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la wadhamini wa klabu hiyo ndiye aliyepokea eneo hilo.