Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
Manchester hoi kwa Liverpool
LONDON, Uingereza
KOCHA wa Liverpool, Rafael Benitez amepata ushindi wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu dhidi ya Manchester United, kwa bao la dakika za mwisho la Ryan Babel aliyetokea benchi.
Mechi hiyo iliyochezwa jana Uwanja wa Anfield na kuhudhuriwa na mashabiki 44,192 ilimalizika kwa wenyeji Liverpool kuibuka na ushindi wa mabao 2-1
Carlos Tevez aliwashitua Liverpool baada ya dakika tatu tangu filimbi ya kuanzisha pambano hilo ilipolia akimalizia wavuni pasi ya Dimitar Berbatov.
Makosa yaliyofanywa na kipa wa Manchester United, Edwin van der Sar ya kupangua ovyo dakika ya 26 yaliipatia Liverpool bao baada ya mpira huo kumgonga mguuni beki Wes Brown na kujaa wavuni.
Bao lililoifanya Liverpool iondoke na pointi zote tatu lilifungwa dakika ya 76 na Babel kwa shuti la mguu wa kulia ndani ya eneo la penelti baada ya kupata pasi ya Dirk Kuyt.
Vidic alitolewa nje dakika ya 89 baada ya kuoneshwa kadi ya pili ya njano kwa kumchezea rafu Xabi Alonso.
Huo ni ushindi wa kwanza kwa Benitez dhidi ya Manchester United tangu alipoanza kuifundisha Liverpool mwaka 2004 na ulipatikana bila Steven Gerrard na Fernando Torres ambao hawakuwemo katika kikosi kilichoanza mechi hiyo. line-up.
Liverpool: Jose Reina, Alvaro Arbeloa, Martin Skrtel, Jamie Carragher, Fabio Aurelio, Yossi Benayoun/Steven Gerrard, Xabi Alonso, Javier Mascherano/Sami Hyypia, Albert Riera/Ryan Babel, Dirk Kuyt na Robbie Keane.
Manchester: Edwin Van der Sar, Wes Brown, Rio Ferdinand, Nemanja Vidic, Patrick Evra, Wayne Rooney, Paul Scholes/Owen Hargreaves, Michael Carrick/Ryan Giggs, Oliveira Anderson/Luis Nani, Carlos Tevez na Dimitar Berbatov
LONDON, Uingereza
KOCHA wa Liverpool, Rafael Benitez amepata ushindi wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu dhidi ya Manchester United, kwa bao la dakika za mwisho la Ryan Babel aliyetokea benchi.
Mechi hiyo iliyochezwa jana Uwanja wa Anfield na kuhudhuriwa na mashabiki 44,192 ilimalizika kwa wenyeji Liverpool kuibuka na ushindi wa mabao 2-1
Carlos Tevez aliwashitua Liverpool baada ya dakika tatu tangu filimbi ya kuanzisha pambano hilo ilipolia akimalizia wavuni pasi ya Dimitar Berbatov.
Makosa yaliyofanywa na kipa wa Manchester United, Edwin van der Sar ya kupangua ovyo dakika ya 26 yaliipatia Liverpool bao baada ya mpira huo kumgonga mguuni beki Wes Brown na kujaa wavuni.
Bao lililoifanya Liverpool iondoke na pointi zote tatu lilifungwa dakika ya 76 na Babel kwa shuti la mguu wa kulia ndani ya eneo la penelti baada ya kupata pasi ya Dirk Kuyt.
Vidic alitolewa nje dakika ya 89 baada ya kuoneshwa kadi ya pili ya njano kwa kumchezea rafu Xabi Alonso.
Huo ni ushindi wa kwanza kwa Benitez dhidi ya Manchester United tangu alipoanza kuifundisha Liverpool mwaka 2004 na ulipatikana bila Steven Gerrard na Fernando Torres ambao hawakuwemo katika kikosi kilichoanza mechi hiyo. line-up.
Liverpool: Jose Reina, Alvaro Arbeloa, Martin Skrtel, Jamie Carragher, Fabio Aurelio, Yossi Benayoun/Steven Gerrard, Xabi Alonso, Javier Mascherano/Sami Hyypia, Albert Riera/Ryan Babel, Dirk Kuyt na Robbie Keane.
Manchester: Edwin Van der Sar, Wes Brown, Rio Ferdinand, Nemanja Vidic, Patrick Evra, Wayne Rooney, Paul Scholes/Owen Hargreaves, Michael Carrick/Ryan Giggs, Oliveira Anderson/Luis Nani, Carlos Tevez na Dimitar Berbatov