Timu ya Soka ya Getafe ya Spain imemsajili mshambuliaji Mason Greenwood kutoka Manchester United kwa mkopo kwa Msimu mmoja
Greenwood alisimamishwa Kucheza ligi Kuu ya Uingereza EPL tokea Januari 2022 kutokana na mashtaka mbalimbali yakiwemo jaribio la ubakaji na unyanyasaji wa kingono, ambapo mashtaka hayo yalifutwa mwezi Februari
Hivi karibuni Mashabiki wa ManU waligoma wakipinga Greewood kurejeshwa katika Kikosi kuitumikia timu hiyo, hivyo Uongozi wa timu ulikuwa unaangalia uwezekano wa kumtoa kwa mkopo, kumuuza au kuvunja mkataba