Mandonga apumzike ngumi kwa muda, kama atashiriki ahusike kama MC

Mandonga apumzike ngumi kwa muda, kama atashiriki ahusike kama MC

Peculiar

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2015
Posts
821
Reaction score
689
Kwanza nianze kumpongeza kwa anachokifanya,si kwamba nampongeza kwa kupigwa pigwa la,ila kwa kutumia fursa.waswahili wanasema "bahati haiji mara mbili" na "mungu akitaka kukupa hakuandikii barua"

Mandonga licha ya kupoteza kwa kupigwa kwa aibu katika mapambano yake.bado hajawahi kuonesha unyonge.hajawahi kuonesha kukata tamaa.niseme tu kwa kifupi "mandonga ANA UWEZO MKUBWA WA KUHIMILI AIBU NA DHARAU,Lau asingekua kua na uwezo huo basi angeshaacha ngumi kitambo kwa mtazamo wangu.wala asingependa hata kusikia akiongelewa maana hata yeye anajijua Hana anachofanya ulingoni,zaidi ya kujitia aibu.

Lakini kwa kuwa ameweza kuishinda hali hiyo basi kwa kuwa KIPAJI CHAKE NI KUONGEA na si masumbwi basi ANATUMIA MDOMO WAKE kuyabadilisha madhaifu yake ya ulingoni kuwa fursa nje ulingo.
HIKI NI KIPAJI KIKUBWA SANA,japo wengi wanaweza kuchukulia poa.

ACHA APIGE PESA
Ni wakati wake, namuombea tu asiwe kwenye mikono ya wahuni,akawa anaumia yeye halafu wanufaika wakubwa wakawa wengine.sitamani kuja kusikia mandonga akija kulalamika baadae kwamba 'ooh nilidhurumiwa' ooh Sina hela' na vitu kama hivyo.

Nasema hivi maana mandonga kajitoa sana,mandonga hapigani kwa ajili yake peke yake,wapo wengi nyuma yake ambao kama mwanaume anapambana kwa ajili yao. Na kwa jina lake,na ushawishi wake wa kwa wakati huu anastahili KULIPWA VIZURI.

MANDONGA NGUMI HAJUI!
Japo mimi siujui huu mchezo kiundani ila sioni tabu kusema mandonga sio bondia. Mwanzo nilikua nasema labda atabadilika kwenye mapambano yanayokuja,ila naona anazidi kuwa mzembe ulingoni
Hajilindi kabisa
Ngumi zake nyepesi
Miguu inalegea mapema sana
Hayuko makini na anachokifanya ulingoni, Yuko makini zaidi na kelele za nje ya ulingo.
NAHISI HATA (MWALIMU HANA).

NAMKUBALI SANA MANDONGA
Anatoa funzo kwamba riziki huja kwa njia yoyote,haupaswi kujisikia mnyonge na kujifichaficha unaposhindwa kwenye lolote. Kwa kuwa hamuibii mtu wala hamdhurumu mtu, acha apige maisha.

MWISHO NISEME
Bado Mandonga anahitajika sana, kuna matukio mengi yatamuhitaji kukusanya watu na kusherehesha.
Hivyo usalama wa afya ya akili na mwili wake ni muhimu vikalindwa kwa manufaa yake na ya anaowapambania nyuma yake.

Ushauri wangu, apumzike ngumi kwa muda, ila kwa kuwa ndio kazi yake basi kama atashiriki, ahusike kama MSHEREHESHAJI (MC) na si mpiganaji.

Ni mtazamo tu
 
Unaweza kunisahihisha mana tunatofautiana namna ya kufikiri,huwenda mtazamo wako ukawa bora zaidi pengine.
 
Aendelee kupambana ataiva tu na kuwa tishio asipokata tamaa
Ila kabla ya kurudi ajifue sana,kwa uwezo wake wa Sasa hawezi kosa chochote kinachohitajika katika kujifua.akiendelea kuingia kichwa kichwa hata hela anazopata hatozifurahia,sababu NGUMI NI MCHEZO HATARI SANA.kama unapigana kimandonga(kiutani utani) unajiweka katika hatari zaidi ya kutikiswa ubongo.
 
Mandonga asije kufa ulingoni....aache masihara
Kweli awe makini kuanzia kwenye kujifua mpaka ulingoni,MANENO NA TAMBO ZAKE ZIISHIE KWENYE MEDIA.ulingoni awe makini na kazi yake, kama anavoojiita 'mtu wa kazi'
 
Madhabiki wake wanasema wanademka naye hata kama atafia ulingoni
Hahaha! ni sawa,ila japo kufa ni kufa,ila Kuna kufa kishujaa na kufa kizembe.
Mandonga mzunguko wa pili tu miguu inapoteza nguvu,anaachia uso mpinzani ajibondee,HUO NI UZEMBE.
 
Hahaha! ni sawa,ila japo kufa ni kufa,ila Kuna kufa kishujaa na kufa kizembe.
Mandonga mzunguko wa pili tu miguu inapoteza nguvu,anaachia uso mpinzani ajibondee,HUO NI UZEMBE.
Mwenzako akipigwa anaingiza hela.

Anatafuta style ya kupigwa.

Umeona wapi chaputa ikamuacha mtu salama?
 
Kwanini asipewe kitengo Cha kupromote ngumi mfano labda kukiwa na mapambano yeye awe mstari wa mbele kutoa hamasa watu waende kutazama kiufupi awe kama hajimanara
 
Kwanini asipewe kitengo Cha kupromote ngumi mfano labda kukiwa na mapambano yeye awe mstari wa mbele kutoa hamasa watu waende kutazama kiufupi awe kama hajimanara
Hakika! na kwa ushawishi wake angepiga hela tu kama anavopiga manara.maana mandonga tayari ni brand kwenye ndondi.
 
Mwenzako akipigwa anaingiza hela.

Anatafuta style ya kupigwa.

Umeona wapi chaputa ikamuacha mtu salama?
Ni kweli anaingiza pesa,lakini anapigana mfululizo sana,halafu anapigwa,
Zile ngumi anazobondwa nazo kichwani mfululizo ni hatari kwa afya yake ya mwili na akili.
Ndio maana hata bodi ya ngumi wanasema hawayatambui,
 
Kwanza nianze kumpongeza kwa anachokifanya,si kwamba nampongeza kwa kupigwa pigwa la,ila kwa kutumia fursa.waswahili wanasema "bahati haiji mara mbili" na "mungu akitaka kukupa hakuandikii barua"

Mandonga licha ya kupoteza kwa kupigwa kwa aibu katika mapambano yake.bado hajawahi kuonesha unyonge.hajawahi kuonesha kukata tamaa.niseme tu kwa kifupi "mandonga ANA UWEZO MKUBWA WA KUHIMILI AIBU NA DHARAU,Lau asingekua kua na uwezo huo basi angeshaacha ngumi kitambo kwa mtazamo wangu.wala asingependa hata kusikia akiongelewa maana hata yeye anajijua Hana anachofanya ulingoni,zaidi ya kujitia aibu.
Lakini kwa kuwa ameweza kuishinda hali hiyo basi kwa kuwa KIPAJI CHAKE NI KUONGEA na si masumbwi basi ANATUMIA MDOMO WAKE kuyabadilisha madhaifu yake ya ulingoni kuwa fursa nje ulingo.
HIKI NI KIPAJI KIKUBWA SANA,japo wengi wanaweza kuchukulia poa.

ACHA APIGE PESA
ni wakati wake, namuombea tu asiwe kwenye mikono ya wahuni,akawa anaumia yeye halafu wanufaika wakubwa wakawa wengine.sitamani kuja kusikia mandonga akija kulalamika baadae kwamba 'ooh nilidhurumiwa' ooh Sina hela' na vitu kama hivyo.
Nasema hivi maana mandonga kajitoa sana,mandonga hapigani kwa ajili yake peke yake,wapo wengi nyuma yake ambao kama mwanaume anapambana kwa ajili yao.
Na kwa jina lake,na ushawishi wake wa kwa wakati huu anastahili KULIPWA VIZURI.

MANDONGA NGUMI HAJUI!
Japo mimi siujui huu mchezo kiundani ila sioni tabu kusema mandonga sio bondia.
Mwanzo nilikua nasema labda atabadilika kwenye mapambano yanayokuja,ila naona anazidi kuwa mzembe ulingoni
Hajilindi kabisa
Ngumi zake nyepesi
Miguu inalegea mapema sana
Hayuko makini na anachokifanya ulingoni, Yuko makini zaidi na kelele za nje ya ulingo.
NAHISI HATA (MWALIMU HANA).

NAMKUBALI SANA MANDONGA
Anatoa funzo kwamba riziki huja kwa njia yoyote,haupaswi kujisikia mnyonge na kujifichaficha unaposhindwa kwenye lolote.
Kwa kuwa hamuibii mtu wala hamdhurumu mtu,acha apige maisha.

MWISHO NISEME
Bado Mandonga anahitajika sana, kuna matukio mengi yatamuhitaji kukusanya watu na kusherehesha.
Hivyo usalama wa afya ya akili na mwili wake ni muhimu vikalindwa kwa manufaa yake na ya anaowapambania nyuma yake.

Ushauri wangu, apumzike ngumi kwa muda, ila kwa kuwa ndio kazi yake basi kama atashiriki, ahusike kama MSHEREHESHAJI (MC) na si mpiganaji.

Ni mtazamo tu
Alieshinda round 4 za mwanzo aache ngumi? Shida hapa makocha wa Mandonga wabadilike au atafutiwe kocha hawamtendei haki, zile round mbili za mwisho Mandonga alitakiwa asiwe na papara alipaswa adefence tu
 
mandonga si bondia bani ni 'comedian', akiendelea kuleta comedy zake ulingoni ipo siku atauliwa ulingoni!
 
Nilichojifunza kupitia Mandonga na uwepo wake kwa wakati huu mfupi

ni kwamba kumbe Si mpira wa miguu tu hata BOXING inaweza kupata watazamaji

Boxing imeanza fatiliwa kwa haraka sana kupitia mandonga,si kwamba ilikua haifatiliwi

ila mandoga ame "ADD VALUE" ya boxing,Tanzania michezo ni mingi inakosa tu watu

sahihi wa kuifikisha mbali,yani mandonga n kama Marketing Manager anatoa promo

za kutosha kiasi kwamba unashawishika kuangalia pambano lake,we need 10 Mandonga ktk michezo yetu yote hapa Tanzania,tutafika mbali sana.

Napenda Spirit ya Mandonga, mwenyewe anakwambia ''ukinipiga kama nimekupiga,Niki kupiga nimekupiga tu'' Huyo ndio mandonga sasa,spirit of wining wining..
 
Ni kweli anaingiza pesa,lakini anapigana mfululizo sana,halafu anapigwa,
Zile ngumi anazobondwa nazo kichwani mfululizo ni hatari kwa afya yake ya mwili na akili.
Ndio maana hata bodi ya ngumi wanasema hawayatambui,
Kaamua kufa.

Sisi kazi yetu ni kumshabikia tu.

Kama.hashauriki ni jambo la kujiandaa kwa msiba au kumchangia matibabu
 
Nilichojifunza kupitia Mandonga na uwepo wake kwa wakati huu mfupi

ni kwamba kumbe Si mpira wa miguu tu hata BOXING inaweza kupata watazamaji

Boxing imeanza fatiliwa kwa haraka sana kupitia mandonga,si kwamba ilikua haifatiliwi

ila mandoga ame "ADD VALUE" ya boxing,Tanzania michezo ni mingi inakosa tu watu

sahihi wa kuifikisha mbali,yani mandonga n kama Marketing Manager anatoa promo

za kutosha kiasi kwamba unashawishika kuangalia pambano lake,we need 10 Mandonga ktk michezo yetu yote hapa Tanzania,tutafika mbali sana.

Napenda Spirit ya Mandonga, mwenyewe anakwambia ''ukinipiga kama nimekupiga,Niki kupiga nimekupiga tu'' Huyo ndio mandonga sasa,spirit of wining wining..
Nakubaliana nawewe 100%.
Ndio mana nasema aendelee kutumika kwa namna nyingine kwa kipindi ambacho anajitibia,anajipumzisha na kujiandaa.
Na itakua vema sana kama atakua na watu sahihi nyuma yake wanaojali kazi yake katika kugawana maslahi.
Maana mjini wanaokula sana au zaidi ya anayeumia na kuvuja jasho ni wengi mno.
 
IMG_7985.jpg

Eeeeh eeeh eeeh eeeeeeeeeeeeeeeh
Eeeee eeeee eeee eeeee eeeeeeeeeeh[emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom