Nyakati
Ni nafasi ya kipekee kwake,
Tantalila zimempa ulaji, hii ni bahati kwake, na bahati haiji Mara mbili huu ni wakati wa yeye kuwa na kitu ambacho hakuwa nacho (kama ana afford lakini)
Kapata mtaji, ni fursa ya kipekee kudili na mishe zingine, kwani ngumi kwake ni kitu anacholazimisha ila hana kipaji.
Watanzania hawachelewi kusahau maana ni kama wanapiga ngoma, ikivuma sana hupasuka, na ndipo tutakapokusahau (msahau mandonga)
1.Pierre liquid
Huyu alitrend na kukick vilivyo, wenye habari zake watakuwa wanajua.na kulamba dili fulani kwenye vinywaji vikali
2.Mzee Mpili
Huyu alikuja kimasihara watu wakamwamini kiasi Cha kula shavu kwa maboss wepesi wa kutumia kick
GSM ila mechi ya kigoma ilimzima, watanzania wakampuuza,
Kabaki akilazimisha umaarufu.
3.Dereva wa bus (New force)
Huyu yeye naye alikimbiza kunako social media na mtindo wake wa kuongea na abiria akitumia Mic, Sina uhakika kama alilamba dili lolote, ila Kuna watu wametumia sauti yake bila ridhaa yake na huwenda akalipwa mpunga mrefu tu.
Hawa ni wachache Kati ya wale ambao umaarufu wao umekuja
automatic.
My advice kwa Karim Mandonga,
Huu ni wakati ambao atazungukwa na makundi makubwa ya watu, kana vile, watakao taka awape pesa fulani ili wambrand kumbe ni matapeli.
Ndugu wengi wasiojulikana wakilazimisha udugu wa lazima.
Washikaji wadau, wacheza boxer wenzie na wote wenye kumjaza kichwa mchizi kusudi tu awanunulie pombe na mizinga,
Bila kusahau wafanyabiashara ambao ni wajanja wa mjini , yaani wakiiona tu sura yake basi suruali anazonunua elfu kumi ataambiwa laki moja.
Umaarufu mzigo haswa ukikupata ukubwani.