Maneno kama haya ndiyo yananifanya nimdharau na kujiuliza kwanini yupo alipo sasa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
1. Naomba
2. Nadhani
3. Sijui
4. Jitahidini
5. Sikubaliani
6. Hela ipo
7. Nasikitika

Ukikutana na Mtu yoyote anasema Maneno haya tajwa hapa juu jua tu kuwa hana akili (Upeo mdogo ), Mvivu Mvivu hata katika Kuongea na Kutembea na yuko hapo aliko kwa bahati mbaya mno.
 
Tunatofautiana, wengine ustaarabu ni jadi yao na sio ujanja kuvunjiana heshima kwa kutumia lugha isiyo na staha

Hivyo ukiona mtu kafanya uteuzi wa maneno kabla ya kuzungumza ilhali ana uwezo wa kufanya atakalo, mheshimu

Sio kwamba ni mpuuzi, ila amejua ya kuwa dunia ni mapito na mkuu ni Mungu tu ila sie binadamu wote tutarejea mavumbini ama katika hali tuliyokuwa nayo awali

Hivyo sio vyema kumtusi Mamba kabla haujavuka mto
 
Wahuni unawaletea ustaarabu??!! Labda kama huwajui
 
Sijui,, ila nadhani hauko serious.. kwa kifupi sikubaliani na hoja zako.
 
Kizimkazi mkubwa wee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…