Michael Mkwanzania
Member
- Jun 8, 2016
- 83
- 652
Maneno machache kwako wewe ambaye dunia bado inakuweka chini,
Hawakujui,
Watafanya kila liwezekanalo kukufanya ubaki ulipo,
Watalipa polisi wakuweka ndani bila wewe kufanya kosa,
Watakutishia,
Watabadilisha maneno waliosema na kutumia nguvu zao kukuhutumu,
Wataongea juu yako bila kukupa nafasi ya kujitetea,
Watakuona we muizi bila wewe kuiba,
Watakupandisha hasira' na kweli jamani hasira hasara, ila ukitulia jua kwamba yatapita,
Jua kwamba wapo wengi wasio na uwezo wala nguvu na wanatafuta kama wewe ambao kila siku haya mambo yanawatokea,
Jua kwamba haya mambo yamewekwa kukubakisha wewe ulipo,
Jua kwamba wapo ambao wameshapitia hayohayo na leo mambo ni tofauti,
Jua kwamba dunia inajua, mbingu zinajua, miti inaona, wanyama wapaao angani wanaona ukweli..
Jua kwamba kesho inakuja..
Mkwanzania.
Hawakujui,
Watafanya kila liwezekanalo kukufanya ubaki ulipo,
Watalipa polisi wakuweka ndani bila wewe kufanya kosa,
Watakutishia,
Watabadilisha maneno waliosema na kutumia nguvu zao kukuhutumu,
Wataongea juu yako bila kukupa nafasi ya kujitetea,
Watakuona we muizi bila wewe kuiba,
Watakupandisha hasira' na kweli jamani hasira hasara, ila ukitulia jua kwamba yatapita,
Jua kwamba wapo wengi wasio na uwezo wala nguvu na wanatafuta kama wewe ambao kila siku haya mambo yanawatokea,
Jua kwamba haya mambo yamewekwa kukubakisha wewe ulipo,
Jua kwamba wapo ambao wameshapitia hayohayo na leo mambo ni tofauti,
Jua kwamba dunia inajua, mbingu zinajua, miti inaona, wanyama wapaao angani wanaona ukweli..
Jua kwamba kesho inakuja..
Mkwanzania.