Maneno na Kauli tunazoambizana tukiwa na hasira; zinafichua yaliyo moyoni!

bahati mbaya ugomvi mwingine huzuka sehemu ambayo haikupi wasaa wa kutafakari; kwenye kadamnasi ya watu...........usiku wa manane!

Nyote wa wawili mmenena mambo muhimu sana lakini tunahitaji kusaidia njia za haraka za kudhibiti hizi hasira

Wasaa upo sana MJ..tatizo ni utayari wa watu kuutumia.
Kunyamaza is the best thing you can do badala ya kuanza kurusha maneno.
Kama ni kwenye kadamnasi we nyamaza ikiwezekana simama ondoka eneo hilo...waliokuzunguka wanaweza kukuona zoba/mwoga but it's better and safer that way on the long run. Kama mko nyumbani/chumbani geukia TV yako..hama chumba...toka nje yani kwa vyovyote vile epuka kureact wakati hasira imekufika machoni.

Binafsi kama sitaki kuondoka nilipo hua namwambia kabisa mtu aliyenikasirisha asiniongeleshe.
Na mimi sitaongea mpaka ntakapohisi nafuu...kwamba sasa naweza ongea na hata kama ni kumsema huyo mtu ntafanya hivyo reasonably. Ntasema yale nnayohitaji ayasikie though yanaweza kumuuma nia yangu haitakua kumuumiza bali kumfanya ajifunze/elewe ubaya wa kilichotokea kabla. And yes....watu wa aina hii hua tunaonekana tuna kiburi ila ni kwa faida ya wote!!!
 

Vipi anayeyasema hayo akiwa amelewa chakari. Mfano anamwambia mkewe kwa lafudhi ya kilevi: Weeh kenge leta chakula haraka hapa?
 
Kila anayekutukana aidha kwa sababu ya hasira au ulevi, fahamu fika kuwa alishapanga kukutendea hivyo kitambo, ila hasira na ulevi ni "catalyst" tu!
 
Wasiogombana ni rahisi kutengana ama kusalitiana. Binadamu tumeumbwa na madhaifu yetu na ugomvi ni sehemu ya kuweka wazi lililo moyoni. Kwa walio wengi baada ya ugomvi huwa amani inatawala tofauti na kuwekeana vinyongo.
 

Lizzy nmevutiwa sana na unavyojaribu ku manage hisia hasi za hasira nk kabala ya kuusema moyo wako! Ninaamini kuwa kuusema kilichoko moyoni baada ya ushindi wa negative emotions hicho utakachosema kitakuwa ni upendo, utakacho tenda kitakuwa ni upendo na utakachowaza ni upendo kwani umeshinda chuki, hasira, kinyongo nk! Kuusema Moyo wako wakati kama huu ni dhibitisho la Ujasiri usio kuwa na hasira, chuki kinyongo na kadhali hivyo .. Ni Ustaarabu na Upendo mkuu wa kijasiri toka moyoni!!

Niongezee jmabo moja, nitaonekanaje na watu wengine wakati ninapokuwa kwenye kipindi cha mpito huku nikisubiria kuzimiliki hisia zangu kabla ya kujieleleza? Umesema waweza kuonekana zoba, mwoga, myonge na dhaifu! Kweli huo ni mtizamo wa watu wengi lakini ..ni mtizamo uliopotoka! Na hatupaswi kuuamini wala kuutilia maanani!! Ufahamu na uelewa wangu vilinipatia sababu ya kuchukua hatua nilizochukua ... Jua kuwa niliamua kabla ..kuwa nitafanya hivyo kama sehemu ya tabia ya maisha yangu na sio kuwa nakurupuka ...Kwa kuwa naamini huo ni ushindi na hiyo show lazima niifanye!! Kwa kuwa kanuni zinasema SHINDA Hisia hasi alafu sema uanchotaka kusema toka moyoni, Shinda hisia hasi fanya uanchotaka kufanya naukifanye toka moyoni. Kwani bila hisia hasi utakachosema , waza na kutenda kitakuwa SIO KOSA! Hata kama kitamuumiza Mtu ..Hayo yatakuwa sio maumivu mabaya ..Ni Maumivu ya kujenga na kuimarisha UPENDO kwenye MIOYO ya watu wakweli na Wapendanao!!
 
Binafsi kama sitaki kuondoka nilipo hua namwambia kabisa mtu aliyenikasirisha asiniongeleshe.
Na mimi sitaongea mpaka ntakapohisi nafuu...

Hatua hiyo inaweza kutafsiriwa na upande wa pili kama kulikwepa tatizo na huenda mara ya pili mwenzio asikubali kwa madai kuwa ulizidharau hisia zake !
 
Kuna neno niliambiwa sitalisahau kamwe eti nan....uli.... Dah ngoja niache tu
 

AJ unayosema ni kweli kabisa...muhimu ni watu waache kuwaza ntaonekanaje/ntachukuliwaje/ntaelewekaje hata kwenye mambo ambayo ni binafsi sana na hayawahusu hao anaofikiria watamwonaje. Kwa kukurupuka na kurusha maneno/makonde ukiwa na hasira utawafurahisha watazamaji ila hasara itakua juu yako pale utakapogundua na kujutia uliyofanya ukiwa umegubikwa na hasira!!
 
Hatua hiyo inaweza kutafsiriwa na upande wa pili kama kulikwepa tatizo na huenda mara ya pili mwenzio asikubali kwa madai kuwa ulizidharau hisia zake !

MJ kukwepa tatizo ni pale unapoliignore moja kwa moja as if halipo...
Kitendo cha kuliacha tatizo kwa muda na kulirudia baada ya akili kutulia sio sawa na kuliignore moja kwa moja. Na mtu akitafsiri ukimya wangu wa muda hivyo basi hana jipya zaidi ya kutaka kuongeza/kuza tatizo!

Alafu swala la hisia zake...je ni bora uanze kupiga kelele ukiwa na hasira na kumtupia maneno mabaya usiyomaanisha??Kwa kufanya hivyo utakua umezijali hisia zake??SIDHANI!!! Kama wewe ndie uliyekasirishwa una haki ya kupata muda wa kutuliza akili yako mpaka utakapokua tayari kukabiliana na tatizo lililopo...na kama wewe ndie mwenye hasira mwombe/mwache atulie kwanza vile vile. Itawafaidisha wote mwisho wa siku.
 
Hatua hiyo inaweza kutafsiriwa na upande wa pili kama kulikwepa tatizo na huenda mara ya pili mwenzio asikubali kwa madai kuwa ulizidharau hisia zake !

MJ .. Ni kweli ..Mara nyingi inachuliwa kama dharau, kiburi na kutokujali ... (haha haha) ..Si kweli ... wala mtu usije kukubali kuingia kwnye huo mtego! Unajua mara nyingi mtu kama anakutukana ..anachotaka pale ni reaction yako ...usiporeact kwa hisia za hasira, chuki nk ... Lazima inabidi areact yeye... na kuumia yeye ...sasa anapokuambia .. unakiburi nk ..ni kama anakuomba ... Uchemke ..ili maumivu yahamie kwako ...HIYO HAIKUBALIKI!! lol
 
Mi nashukuru hasira zikizidi huwa siongei neno lolote, nakuwa kama bubu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…