Maneno ya Hayati Moringe Sokoine Mwaka 1 Kabla ya Kifo Chake

Maneno ya Hayati Moringe Sokoine Mwaka 1 Kabla ya Kifo Chake

jnuswe

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
1,270
Reaction score
549
"TUMERUHUSU Walanguzi na Wahujumu Uchumi kuongoza nchi. Wananchi wamefika mahali ambapo wanashindwa kutofautisha kati ya viongozi wa chama (CCM) na Serikali na Walanguzi na Wahujumu uchumi wa nchi."

Ilikuwa Machi 7, 1983 Dodoma.

Source: Raia Mwema

Maneno hayo yalisemwa na kiongozi mzalendo kabisa ambaye ameandika historia katika nchi hii ambayo ni vigumu kufutika vizazi hata vizazi,

Kipindi hicho walanguzi na wahujumu uchumi ni maneno yaliyotumika, kwa sasa tunaweza kusema Hayati Sokoine alikuwa anamanisha wezi au mafisadi kwa maneno yaliyozoeleka kwa sasa .


Swali la kujiuliza ni kwamba kumbe ufisadi ndani ya CCM na serikali ya CCM ni jadi yao miaka na miaka. Kama ni hivyo kwa nini tunaendelea kukipa chama hiki dhamana ya kuongoza nchi ?

Mimi nionavyo kwa sasa hali aliyokuwa akiikemea Sokoine kwa sasa ni mbaya kuliko wakati ule, Wako wapi viongozi wenye uzalendo wa kuweza kukemea mafisadi kutumia nguvu ya pesa kuingia madarakani na kisha baada ya hapo kuendelea kuliangamiza Taifa.


Kwa maneno hayo ya kiongozi wetu mpendwa nakiona kifo cha CCM kimekaribia , Watanzania tutafakari na kuchukua hatua .

Nawasilisha
 
Ngoja wake vijana was buku saba uone jinsi watakavyokitetea hicho chama kwa jazba na mapovu kuwatoka. ccm kilishaoza tangu siku nyingi, watu wengi walikuwa hawajafunuliwa na kuelewa hilo. Shukrani kwa CDM na elimu ya uraia sasa wengi wamefunguka macho. Kipindi cha kufanya msukumo was mwisho (final push) ni sasa. Tuhakikishe ccm hawashiki tena serikali 2015.
 
Waziri mkuu Sokoine wa wakati huo aliamua kuufia ukweli kama Kambona wa wakati ule
 
HAHAHAAAH CCM YA LEO IMEJAZA WATU WASIO MAKINI, WAADILIFU WALA WAUNGWANA.,......hao kina Moringe wangekuwa hai leo wangekuwa wanapata shida kujitambulisha kama wao pia ni wanaccm ambao ni chama kimoja na Nape na Mwigule Tindikali au Kinana mzee wa Tembo

1380687_684819801530123_1049973272_n.jpg
 
Sokoine is overrated.

He was driving this country towards being a police state.

People hardly mention that.
 
Kwenye hiyo picha kuna mengi ya kujifunza , Kinana anakuja ndita kula wali na maharage, hajui hayo ndo maisha halisi ya mtanzania ?
 
HAHAHAAAH CCM YA LEO IMEJAZA WATU WASIO MAKINI, WAADILIFU WALA WAUNGWANA.,......hao kina Moringe wangekuwa hai leo wangekuwa wanapata shida kujitambulisha kama wao pia ni wanaccm ambao ni chama kimoja na Nape na Mwigule Tindikali au Kinana mzee wa Tembo

1380687_684819801530123_1049973272_n.jpg

Huyu babu cjui alikua anakula vi nini wakati mezani ni ubwabwa na maharage..kajamaa uko nyuma kanacheekaa leo kanaionasiku kinana kesha fanya salivalization..
 
"TUMERUHUSU Walanguzi na Wahujumu Uchumi kuongoza nchi. Wananchi wamefika mahali ambapo wanashindwa kutofautisha kati ya viongozi wa chama (CCM) na Serikali na Walanguzi na Wahujumu uchumi wa nchi."

Ilikuwa Machi 7, 1983 Dodoma.

Source: Raia Mwema

Maneno hayo yalisemwa na kiongozi mzalendo kabisa ambaye ameandika historia katika nchi hii ambayo ni vigumu kufutika vizazi hata vizazi,

Kipindi hicho walanguzi na wahujumu uchumi ni maneno yaliyotumika, kwa sasa tunaweza kusema Hayati Sokoine alikuwa anamanisha wezi au mafisadi kwa maneno yaliyozoeleka kwa sasa .


Swali la kujiuliza ni kwamba kumbe ufisadi ndani ya CCM na serikali ya CCM ni jadi yao miaka na miaka. Kama ni hivyo kwa nini tunaendelea kukipa chama hiki dhamana ya kuongoza nchi ?

Mimi nionavyo kwa sasa hali aliyokuwa akiikemea Sokoine kwa sasa ni mbaya kuliko wakati ule, Wako wapi viongozi wenye uzalendo wa kuweza kukemea mafisadi kutumia nguvu ya pesa kuingia madarakani na kisha baada ya hapo kuendelea kuliangamiza Taifa.


Kwa maneno hayo ya kiongozi wetu mpendwa nakiona kifo cha CCM kimekaribia , Watanzania tutafakari na kuchukua hatua .

Nawasilisha

Ndio maana Nyerere alisema watanzania tuna maadui watatu ujinga,umaskini na maradhi.. Mpaka haya yapungue kiwango cha zaidi ya asilimia 65 ndio tunaweza kubadilika kwa mfano sasa tunaenda vizuri ila kinachotuponza ni vijijini hawa maadui bado wapo asilimia mia na hamsini...
 
HAHAHAAAH CCM YA LEO IMEJAZA WATU WASIO MAKINI, WAADILIFU WALA WAUNGWANA.,......hao kina Moringe wangekuwa hai leo wangekuwa wanapata shida kujitambulisha kama wao pia ni wanaccm ambao ni chama kimoja na Nape na Mwigule Tindikali au Kinana mzee wa Tembo

1380687_684819801530123_1049973272_n.jpg

Hebu angalieni hao watu vizuri mniambie wanakifurahia hicho chakula au wanashangaa ni chakula cha namna gani wanachokula binadamu waliowatembelea! Angalieni kwa makini sana.
CCM kilikuwa chama cha Wakulima na Wafanya kazi. Ni Kina Sokoine walijua hilo na waliamini hivyo. Kilichowashangaza akina Sokoine na wenzake wachache walikuja kukukuta chama kimejaa manyang'au walanguzi na wahujumu uchumi.

Niambieni nafasi ya wakulima ipo wapi katika chama cha Mapinduzi. Niambeni nafasi ya Wafanyakazi ipo wapi katika Chama cha Mapinduzi. Wakiitisha harambee, ni wafanyakazi wangapi wanaalikwa na wakulima kuchangia?

Enzi za mwalimu kilikuwa chama chetu. Kiongozi alijibanisha kwa uwezo wake wa kifra kutatua matatizo ya wananchi. Leo hii viongozi wa kuteuliwa wanapatika kwa njia ya nani anamfahamu nani. Wakiambiwa Chama kimepoteza mwelekeo wanapiga kelele. Akina Kolimba wako wapi? Walisema Chama kimepoteza mwelekeo. Na sasa ni mbaya zaidi. Sijui kama Mwenyekiti wa Chama anajua kuwa manyang'au wabaya kabisa kuliko wale aliokemea Sokoine wamekita mizizi katika chama. Kama haamini anaimbie mkakati wa kuvua gamba ulienda wapi. Yeye aliyepiga kelele na mapovu yanamtoka ndo anashangaa wali maharage kuwa ni chakula cha Watanzania?
 
HAHAHAAAH CCM YA LEO IMEJAZA WATU WASIO MAKINI, WAADILIFU WALA WAUNGWANA.,......hao kina Moringe wangekuwa hai leo wangekuwa wanapata shida kujitambulisha kama wao pia ni wanaccm ambao ni chama kimoja na Nape na Mwigule Tindikali au Kinana mzee wa Tembo

1380687_684819801530123_1049973272_n.jpg


Hapa nadhani hakukuwa na access ya hotel, nadhani ni kijijini. Pia aliyepewa tenda ya kulisha hao wevi naye alichakachua akala pesa ya maini akapika maharagwe badala yake. Who cares?
 
Tuanomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iboreshe Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Vijana tuna hamu ya kuindosha CCM madarakani, maana nyinyi baba/mama/shangazi/wajomba zetu MLI/MMESHINDWA.

CDM mbona siwasikii mkiishinikiza NEC kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura??!.

Pia CDM fanyeni kampeini kubwa ya kuwaelimisha vijana wote nchini 18-40 years old wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Kama CDM mtafanikisha zoezi hili na > 80% ya vijana wakajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Na siku ya kupiga kura > 70% ya vijana tukapiga KURA. Huhitaji kuwa a rocket Scientist kujua kwamba HUO NDIYO UTAKUWA MWISHO WA CCM.

CHADEMA the Ball is in your Court. Msituangushe VIJANA wa NCHI hii tuliodhamiria kufanya MABADILIKO.
 
Hapa nadhani hakukuwa na access ya hotel, nadhani ni kijijini. Pia aliyepewa tenda ya kulisha hao wevi naye alichakachua akala pesa ya maini akapika maharagwe badala yake. Who cares?

Kijijini hakuna tenda hapo wana kijiji wamechangishwa na kikapikwa na kwa ajili ya watu wakubwa mzee wa operation bila ganzi na nape
 
Tuanomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iboreshe Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Vijana tuna hamu ya kuindosha CCM madarakani, maana nyinyi baba/mama/shangazi/wajomba zetu MLI/MMESHINDWA.

CDM mbona siwasikii mkiishinikiza NEC kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura??!.

Pia CDM fanyeni kampeini kubwa ya kuwaelimisha vijana wote nchini 18-40 years old wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Kama CDM mtafanikisha zoezi hili na > 80% ya vijana wakajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Na siku ya kupiga kura > 70% ya vijana tukapiga KURA. Huhitaji kuwa a rocket Scientist kujua kwamba HUO NDIYO UTAKUWA MWISHO WA CCM.


CHADEMA the Ball is in your Court. Msituangushe VIJANA wa NCHI hii tuliodhamiria kufanya MABADILIKO.

VIJANA POPOTE MLIPO ZIKENI CCM, TUPENI KULE
481682_500554979980091_2085213905_n.jpg
 
"TUMERUHUSU Walanguzi na Wahujumu Uchumi kuongoza nchi. Wananchi wamefika mahali ambapo wanashindwa kutofautisha kati ya viongozi wa chama (CCM) na Serikali na Walanguzi na Wahujumu uchumi wa nchi."

Ilikuwa Machi 7, 1983 Dodoma.

Source: Raia Mwema

Maneno hayo yalisemwa na kiongozi mzalendo kabisa ambaye ameandika historia katika nchi hii ambayo ni vigumu kufutika vizazi hata vizazi,

Kipindi hicho walanguzi na wahujumu uchumi ni maneno yaliyotumika, kwa sasa tunaweza kusema Hayati Sokoine alikuwa anamanisha wezi au mafisadi kwa maneno yaliyozoeleka kwa sasa .


Swali la kujiuliza ni kwamba kumbe ufisadi ndani ya CCM na serikali ya CCM ni jadi yao miaka na miaka. Kama ni hivyo kwa nini tunaendelea kukipa chama hiki dhamana ya kuongoza nchi ?

Mimi nionavyo kwa sasa hali aliyokuwa akiikemea Sokoine kwa sasa ni mbaya kuliko wakati ule, Wako wapi viongozi wenye uzalendo wa kuweza kukemea mafisadi kutumia nguvu ya pesa kuingia madarakani na kisha baada ya hapo kuendelea kuliangamiza Taifa.


Kwa maneno hayo ya kiongozi wetu mpendwa nakiona kifo cha CCM kimekaribia , Watanzania tutafakari na kuchukua hatua .

Nawasilisha

Ivi kipi kinachooza? Kiongoz ama chama?
 
sokoine hakustahili kuwa ccm , ilimbidi kwa sababu kulikuwa hakuna chama kingine .
 
Back
Top Bottom