Maneno ya katibu Mkuu wa BAVICHA yanaelezea uelewa mdogo walionao vijana. Ni CCM pekee ndio itakomboa vijana wa nchi hii

Maneno ya katibu Mkuu wa BAVICHA yanaelezea uelewa mdogo walionao vijana. Ni CCM pekee ndio itakomboa vijana wa nchi hii

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Katibu Mkuu wa BAVICHA amenukuliwa akisema CCM inawafanya watanzania ni maskani lakini wao wakifaidika sana. Maneno hayo yanafanya nijiulize sana juu ya uelewa wa vijana hao wa CHADEMA na mambo yafuatayo nimefahamu:

Kwanza, Vijana hao wamemeza sumu mbaya ya kujilemaza kifikra. Taifa lolote lenye maendeleo vijana wake wana fikra na mitazamo mikubwa lakini hili limekosekana kwa vijana wa CHADEMA na wanalemaa .

Pili, CHADEMA inakiri kupitia BAVICHA kuwa kama Chama hakuna uwezo wa kuwakomboa vijana ndio maana UVCCM hawalalamiki kwa kuwa kina agenda kubwa za kuwavusha vijana kama vijana kupewa mafunzo mbalimbali.

Tatu, BAVICHA inashindwa kuliambia Taifa mpango ulionao kwa vijana hususani kwenye suala la ajira na badala yake inaliaminisha Taifa kuwa suala la ajira ni la wachace.

Nne, BAVICHA inaonesha ni kikundi kinachojali maslahi yao binafsi na sio maslahi ya Umma ndio maana hoja ya katibu Mkuu wa BAVICHA imeelekea ni kwa namna gani CHADEMA itanufaika na sio namna gani Taifa litanufaika.

BAVICHA imetambua mchango wa CCM kwa watu wake ,hili ni jambo zuri kwa kuwa sera za CCM ni bora kwa watu wote.

BAVICHA imetambua jukumu la pamoja la kujenga uchumi ambao ni shirikishi linalofanywa na CCM.
 
Back
Top Bottom