Manji ajaribu kujisafisha Kashfa ya Kagoda; ajichongea!


Sorry Mkubwa... Wizi ni wizi tu uwe wa siku zilizopita au wa leo?? Madhara yake kwa Taifa hili ni yale yale... Mimi naamini kabisa Wizi uliofanywa miaka iliyopita bado unatugharimu hadi leo!!! Na labda utaendelea kutugharimu kwa miaka mingi ijayo!!! Mimi binafsi sioni ubaya wa kuendelea kujadili hilo. "IF YOU DON'T KNOW YOUR PAST..... YOU DON'T KNOW YOUR FUTURE..."
 
Yale yale ya kufungua akaunti siku ya mwaka mpya.kumbe huyu msemakweli ni msanii tu aliyetumwa na wasanii wenzie kuudanganya umma.

Ajaribu njia nyingine, hii imebuma-shame on you manji & your group.
 

Umeongea upupu mwingine juu ya upupu wako wa awali! Naona hata hujui unachoongea hapa, ndio maana unaishia kusahihisha lugha. We umesema kampuni inaweza kuwepo kabla ya incorporation! Tumekwambia kama ilikuwepo basi haikuwa Kagoda Agriculture Ltd, na hivyo Manji hasinge weza kopa fedha kwa Kagoda Agriculture Ltd maana haikuwepo! Hata kwenye mkataba kusinge onekana neno Kagoda Agriculture Ltd.

Hamna sheria yoyote unaijuwa wewe unaishi kwa kubahatisha na kuongea lolote ili mradi mkono uende kinywani. Kama anayehusika na huo mkopo ni mtu binafsi na si kagoda Agriculture Ltd basi Mkataba ulipaswa kuonyesha kuwa Quality Finance Corporation Ltd wamekopa fedha kutoka kwa huyo mtu binafsi na si kwa Kagoda Agriculture Ltd, na kwa mantiki hayo unaongea kitu kile kile ambacho Invisible amekianisha hapo juu " Iweje Quality Finance Corporation Ltd" wakopeshwe fedha na "Kagoda Agriculture Ltd" wakati haijasajiliwa?!

Nyie vibaraka wa Mafisadi tatizo lenu elimu ya kuunga unga hata hamjui mnachoongea, mwisho wake mnakimbilia vioja na viroja badala ya hoja.
 

Hicho kifungu kimewekwa kwa ajili ya 'promoters' wa kampuni. Kuna nyakati 'promoters' wanalazimika kuingia mikataba (kwa mfano rental ya jengo, nk) kabla kampuni haijaanzishwa (sajiliwa). Kwa kifungu hicho, huyo promoter aliyeingia huo mkataba ndio personally anakuwa liable (kwa sababu kampuni anayodai kuirepresent kimsingi inakuwa hai exist). So hapo haina maana kwamba kampuni tajwa imeingia kwenye makataba huo. Hata hivyo katika mkataba huo promoter hawezi kuweka jina la kampuni ambayo haipo (kama ilivyo kwa Kagoda na QFCL) kwa sababu mkataba utakuwa void/voidable.
 

SMU! Good, unafahamu unacho ongea.

Kuna watu humu kazi yao kuongea lolote hata kama kitu hakijui anajifanya anakijuwa.
 
Reactions: SMU

hapa Hiyo quality finance wanaweza kushitakiwa kwa money laundering, kwani kilicho fanyika hpo ni kutaka kutakasa fedha chafu, kwa kuziingiza katiksa system na baadae kufuta nyayo za chanzo za hizo fedha. hivi kile kitengo chetu cha money laundering kipo?
 
z Kuendelea nako kuvumbua uwizi mpya wakati ule wa zamani haujashughulikiwa nalo ni tatozo. Hivyo sioni hoja yoyote ya msingi hapo.
 
Je hizo pesa ziliingizwa lini kwenye account ya kagoda? na account ilifunguliwa lini? je waliwezaje kufungua account bila vielelezo vya kampuni?
 
Hiki kitengo kipo lakini kumbuka lazima kiwe chini ya mtu aliyeteuliwa na Kikwete kwa maslahi ya Kikwete ,maswahiba wake na/au Chama
 



Hapa swali gumu ambalo naliona hapa ni kuwa inaonekana BoT walikopesha fedha Kampuni hewa hiyo ya Kagoda Agriculture Ltd, yamkini walipata mkopo kabla ya usajili. Maadamu waliamishia fedha zao kama mkopo kwa QFC(ltd) kabla ya kusajiliwa basi walizipata kabla ya kusajiliwa.

Labda ndio maana CCM iliamua kumpoteza Balali! Ila bado Manji ana kesi ya kujibu na hao wenzake pia hata BoT waliotoa fedha wanatakiwa kukamatwa wahusika wote, hata kama Balali hayupo lakini wasaidizi wake wote waliopitisha fedha wakamatwe, nadhani hata Mkapa anapwa kukamatwa.
 
Reactions: SMU
halafu Manjiii na akili zake zote za biashara anataka kutuaminisha kampuni ambayo haina historia yoyote na hao wakurugenzi wake? wanaweza kumkopesha fedha nyingi hizo? kama sio fedha za wizi? " rejea sheria ya buyer be aware" na hiyo kampuni kagoda sio kampuni ya kukopesha, walau ingekuwa kagoda kamkopesha manjii mahindi basi angala tungesema madhumuni na biashara yenyewe vinashabihiana. na je wao manjjiii walitoa dhamana gani? na zilisajiliwa kisheria kama dhamana! maana hela zinazo ongelewa hapa si mchezo!
 

Hiki kitengo kipo lakini kumbuka lazima kiwe chini ya mtu aliyeteuliwa na Kikwete kwa maslahi ya Kikwete ,maswahiba wake na/au Chama

Kama hawajabadilisha nadhani kipo chini ya wizara ya fedha! Toka mwanzo sijui kwanini hawaku wafungulia Manji na wenzake kesi chini ya hii sheria?

Lakini Wakuu mi nachanganyikiwa hapa; Mi nilijuwa kuwa Manji na wenzake hawakushtakiwa kwa sababu Rais alitoa sharti tokea mwanzo kuwa wanarudisha fedha hawata shtakiwa! na hivyo Manji na kagoda waliangukia katika msamaa huo, si kuwa hawakushtakiwa kwa sababu hawakumjuwa mwenyewe Kagoda! au mimi ndio nachanganya?

Hii kauli ya Kikwete tunaiweka wapi? Maana aliitoa mchana kweupe mbele ya Watanzania! au ndio Kigeugeu?
 
hyo document ya kwanza anakubali kua QF ilipokea hela kutka kagoda,
so kagoda kweli ilikwapua hizo hela.
sasaje, manji atajitenga vipi na kagoda??
 
na inasemekana huyu jamaa anataka kuingia tena kwenye ufukwe wa coco beach, manispaa ya kinondoni wanataka kumpoka yule mwafrika na kumpa manji, kwa madai ya kuwa huyu mtu mweusi alipi kodi ikiwa analipa. sasa wanataka fukwe zote zimilikiwe na mashombishombi!
 
1.tika taarifa yake kwa vyombo vya habari, kipengele cha 5 na 6 anamlenga mtu badala ya kuonesha kua yanayosemwa sio kweli.
2. taarifa hyo pia anakiri kurudisha fedha serikalini. swali;kwa nini arudishe serikalini wakati alikopeshwa na kagoda??
3. hyo document ya kwanza anakubali kua QF ilipokea hela kutka kagoda, so kagoda kweli ikwapua hizo hela.
saje, manji atajitenga vipi na kagoda??
4.Nadai kua alikopeshwa na kagoda siku ya tarehe 12-9-2005, lakini huku chini baadae anaonesha kagoda ilisajiliwa 29-9-2005, huu ni utata mtupu.
 
The only reason these fools are still playing with the system, is because the president is behind all this..I mean Msemakweli has more evidence than Osman Rashid and his people?...DPP?. The president has placed incompetent and corrupt people everywhere to cover his back... Ngelejas, Shimbos, Osmans, Mkullos, Simbas, Jairos, Maiges, Nchimbis etc
 


Lousy docs lakini jamaa ndo wamepigia bilioni 30 duh! Bongo kweli "tambalaleee" Nchi kama vile haina wenyewe.
 

Kama msemakweli as an individual anaweza ku-collect concrete evidence za wizi mkubwa kiasi hicho, sasa sijui kina Hosea, UWT na wengineo kazi yao ni nini? Kuna uwajibikaji kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…