Manji kujitoa Yanga?

Masatu

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2007
Posts
3,276
Reaction score
131
Kuna habari kuwa anaejiita mfadhili wa Yanga Yusuf Manji ambae pia ni mkurugenzi mtendaji wa Quality Group maji yamemfika shingoni na sasa anautema "ufadhili" wa klabu hiyo kongwa yenye historia ya migogoro isiyo kwisha.

Chanzo chetu ndani klabu hiyo kinatuhabarisha kuwa "mfadhili" amechoshwa na mwenendo wa kusua sua wa Yanga ktk ligi ya Vodacom sanjari na kunitumia mamilioni kununua wachezaji wanaoitwa wa kulipwa na kulipa mishahara minono kwa makocha na wachezaji.

Manji ambaye aliingia kwa mbwembwe na kuahidi kuifanya yanga kuwa "Arsenal" ya Tanzania anajiunga na mlolongo wa watu maarufu walijitahidi kutatua migogoro ya Yanga akiwemo Reginald Mengi,Yusuf Makamba ( akiwa mkuu wa mkoa Dar Es Salaam ) Sulemain Kuchaya ( aliyekuwa mshauri wa Rais Mkapa) Mbunge Azan Zungu nk.

Yanga ambayo imenyang'anywa ubingwa na yule Mnyama mkali Simba imeshafungwa mechi 3 ktk ligi inayoendelea. Na kutia chumvi ktk kidonda aliye kuwa kocha wao mkuu Razak Siwa amekiri mwenyewe kuwa yeye ni m-babaishaji na haiwezi kazi na kupelekea kurejeshwa Jack Chamangwana ambaye alikuwa akizurura mitaani Dar kama machinga bila kazi yeyote ya maana. Bado haijafahamika mara moja kama Jack ana mkataba wowote (let alone work permit kutoka immigration) au ni day worker mpaka atakapo kuja huyo mlima maparachichi kutoka Poland.

Tunachokuwa nafasi hii kuwakumbusha watani kuwa ile ni Yanga Sports Club neno Sports linajumuisha pia netball labda wajaribu bahati yao huko
 

Haya wana Kandambili tuliwa tabiria hili sana limewakuta...

Only on JF heh hey!
 
hilo ndo tatizo la soka letu lililolaaniwa la bongo...hasa hizi club zetu mbili kubwa..simba na yanga..yaaani kwa migogoro hazina wapinzani halafu kichekesho zaidi ni pale zinapopokezana migogoro...mwaka huu ikiwa ni wana msimbazi basi kwa jangwani kuna tulia likilipuka la jangwani basi msimbazi kwatulia...yaani sijui mpira utaendelea lini..halafu cha ajabu watu wengine wamezeeeka wanatakiwa kuwa wanawasimulia vitukuu na vilembwe vyao hadithi za miaka yao ya 47..lakini bado tuu wanangangania uongozi na madaraka without aibu...dohhh
 
yanga tuliwaambia kuwa lengo la manji halikuwa mpira..kwanza manji ni simba[na alipotaka kujiingiza kwenye mpira alitaka kuingilia simba,washauri wakamuambia kwa kuwa simba walikuwa ni kina MO..NI BORA ANGEINGILIA YANGA AMBAO kwa wakati ule walikuwa na shida na vile vile azingatie histororia ya yanga]..lengo lake kuu lilikuwa ni PUBLIC IMAGE BUILDING CAMPAGNE..especially hasa alivyokuwa akikabiliwa na kashfa mbalimbali....sasa kwa kuwa hisia za wananchi na magazeti hawaongelei tena kashfa za manji..hana haja tena na sabuni YANGA...

Poleni sana................
 
Tumeshapoa! I try 2 imagine sijui hata itakuwaje..... yaani hadi naogopa
 
ahaaaaaaaaaa
yaani mie sijui itakuwaje,kwani mkataba wake ulikwisha lini?
na vipi mishahara atawalipa nani?
na Simba wanacheza lini?
 
eeeeeeeee
tunaweza kupata iyo barua ya aliyoandika Manji kwa vyombo vya habari?na Mwenyekiti Madega anasemaje?
 
Timu zilizokuwa na msimamo Tanzania, zilikuwa timu za makampuni....
1) Pamba 2) Ushirika 3) Ndovu 4) RTC (mwanza, kigoma, kagera) 5) Mecco etc........yaani tangu mashirika hayo yaachane na michezo ligi ya bongo chovu tu.
Hao Simba/Yanga majina makubwa ila utumbo mtupu....kila siku kufarakana tuuu aaah, wanaboa.

Hivi kombe la taifa liliishia wapi? Linaloshirikisha kombaini za mikoa....Mzizima United, Kagera Eagles, Mwanza Heroes etc....labda hiyo itachangamsha mpira kidogo hapo nyumbani.

whatteva happened?
 
Manji kuondoka ilikuwa story ya kitambo mno!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…