moodykabwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2015
- 625
- 602
YANGA IKISHUSHWA DARAJA, BOSS WETU, MWENYEKITI WETU NA MPANGAJI WETU ATAWAJIBIKA NA HAWEZI KUKWEPA KIKOMBE HIKI :
Daniel Naftal Ngogo :
Dr Jonas Tiboroa alifukuzwa na bwana mkubwa Ukatibu mkuu wa Yanga kwasababu eti alisafiri kwenda Kwenye seminar nchini Ghana bila ruhusa ya bwana mkubwa mbali ya ukweli kuwa Seminar ilikuwa na manufaa ya timu bado bwana mkubwa hakujali lakini pia pamoja na weledi mkubwa na utendaji uliotukuka wa Dr Tiboroa (Mhadhiri mwandamizi toka Chuo Kikuu cha Dar es salaam) bado alifukuzwa!!
-Siku Chache baada ya Dr Tiboroa kufukuzwa tukaja kuambiwa Yanga walishindwa kushiriki kikao muhimu sana cha maandalizi ya hatua ya makundi ya michuano ya Shirikisho, kikao ambacho kilikuwa kinajadili mambo muhimu kwa manufaa ya timu kama vile Udhamini wa jezi, haki ya matangazo (TV rights) pamoja na kanuni mbali mbali za mashindano, tukaishia kuzuiliwa kuvaa hata jezi zetu tulizo Kwenda nazo na kwa huruma tukasaidiwa na TFF kupata jezi zinazocomply na mashindano bado tukiporudi home tukaanza ugomvi wa kijinga wa haki ya kurusha mechi zetu wakati mambo yote yaliamliwa na kupitishwa na kikao cha Shirikisho la mpira Afrika ambacho hatukushiriki kwa uzembe wetu wenyewe.
-Leo tena dirisha la Usajili limefungwa, Yanga hawajawasilisha usajili wao TFF, usajili unaofanywa kupitia mfumo wa kisasa kupitia online application system maarufu kama 'TMS' (Transfer Merging System) , kwa mujibu wa TFF Yanga walipo alikwa Kwenye seminar ya Mafunzo ya namna Transfer Merging System inavyofanya kazi hawakupeleka muwakilishi, yaani mpaka Toto Afrika, Lipuli, Majimaji waliona umuhimu wa Mafunzo hayo Yanga hawakuona umuhimu wa kushiriki, nimesikiliza utetezi toka kwa kaimu katibu mkuu wa Yanga Baraka Desderbit amesema wao hawakushiriki kwasababu yeye hakuwepo na Jerry Muro alikuwa amefungiwa kwahiyo walikosa mtu wa kumpeleka kule Kwenye Mafunzo... hili ndio sababu ya Yanga kushindwa kushiriki Mafunzo haya muhimu kwa timu:kwakweli nimesikitika Sana kusikia utetezi huu Moja ya utetezi dhaifu na wa kijinga kabisa kuwahi kutolewa na Katibu Mkuu wa timu kama Yanga.
*MY TAKE *
-Toka Dr Tiboroa anafukuzwa na Manji timu imepwaya Sana Kwenye eneo la utendaji (Ofisi ya katibu mkuu) inashindwa kufanya kazi zake kikamilifu hata zile ndogo za kawaida ambazo hata timu za Lipuli FC toka Iringa zinatuzidi.
-Kaimu katibu mkuu wa Yanga Baraka Desderbit, Muhasibu huyu kitaluma toka Quality group, kijana mwenzetu hana uwezo wa kuwa katibu mkuu wa Yanga matukio haya yanayotokea Sasa ni ushahidi tosha kuwa boss wetu wa Secretarieti hatoshi, ni kweli wenda alikuwa Muhasibu mzuri pale Quality Group lakini Kuna utofauti mkubwa Kati ya kuendesha timu na kuwa Muhasibu wa kampuni binafsi.
-Washabiki wa Yanga tupunguze kumpigia makofi Manji kwa kila kitu anachosema tumfundishe kumkatalia na kusema hili sawa Lakin hili hapana bila hivyo atatupeleka shimoni.
-Mwisho boss wetu mkubwa tuliye mkodisha timu anapaswa kujua Yanga ni timu yenye umasikini mkubwa wa fedha lakini yenye utajili mkubwa Sana wa Mashabiki na wapenzi.. Kwa hiyo pesa sio kila kitu Kwenye timu, timu pia zinahitaji uongozi bora na Manji sio kiongozi bora wa timu bali ni mfadhiri bora hivyo anapaswa kupata katibu bora kama Dr Tiboroa,
Daniel Naftal Ngogo
Shabiki na mwanachama wa Yanga
Daniel Naftal Ngogo :
Dr Jonas Tiboroa alifukuzwa na bwana mkubwa Ukatibu mkuu wa Yanga kwasababu eti alisafiri kwenda Kwenye seminar nchini Ghana bila ruhusa ya bwana mkubwa mbali ya ukweli kuwa Seminar ilikuwa na manufaa ya timu bado bwana mkubwa hakujali lakini pia pamoja na weledi mkubwa na utendaji uliotukuka wa Dr Tiboroa (Mhadhiri mwandamizi toka Chuo Kikuu cha Dar es salaam) bado alifukuzwa!!
-Siku Chache baada ya Dr Tiboroa kufukuzwa tukaja kuambiwa Yanga walishindwa kushiriki kikao muhimu sana cha maandalizi ya hatua ya makundi ya michuano ya Shirikisho, kikao ambacho kilikuwa kinajadili mambo muhimu kwa manufaa ya timu kama vile Udhamini wa jezi, haki ya matangazo (TV rights) pamoja na kanuni mbali mbali za mashindano, tukaishia kuzuiliwa kuvaa hata jezi zetu tulizo Kwenda nazo na kwa huruma tukasaidiwa na TFF kupata jezi zinazocomply na mashindano bado tukiporudi home tukaanza ugomvi wa kijinga wa haki ya kurusha mechi zetu wakati mambo yote yaliamliwa na kupitishwa na kikao cha Shirikisho la mpira Afrika ambacho hatukushiriki kwa uzembe wetu wenyewe.
-Leo tena dirisha la Usajili limefungwa, Yanga hawajawasilisha usajili wao TFF, usajili unaofanywa kupitia mfumo wa kisasa kupitia online application system maarufu kama 'TMS' (Transfer Merging System) , kwa mujibu wa TFF Yanga walipo alikwa Kwenye seminar ya Mafunzo ya namna Transfer Merging System inavyofanya kazi hawakupeleka muwakilishi, yaani mpaka Toto Afrika, Lipuli, Majimaji waliona umuhimu wa Mafunzo hayo Yanga hawakuona umuhimu wa kushiriki, nimesikiliza utetezi toka kwa kaimu katibu mkuu wa Yanga Baraka Desderbit amesema wao hawakushiriki kwasababu yeye hakuwepo na Jerry Muro alikuwa amefungiwa kwahiyo walikosa mtu wa kumpeleka kule Kwenye Mafunzo... hili ndio sababu ya Yanga kushindwa kushiriki Mafunzo haya muhimu kwa timu:kwakweli nimesikitika Sana kusikia utetezi huu Moja ya utetezi dhaifu na wa kijinga kabisa kuwahi kutolewa na Katibu Mkuu wa timu kama Yanga.
*MY TAKE *
-Toka Dr Tiboroa anafukuzwa na Manji timu imepwaya Sana Kwenye eneo la utendaji (Ofisi ya katibu mkuu) inashindwa kufanya kazi zake kikamilifu hata zile ndogo za kawaida ambazo hata timu za Lipuli FC toka Iringa zinatuzidi.
-Kaimu katibu mkuu wa Yanga Baraka Desderbit, Muhasibu huyu kitaluma toka Quality group, kijana mwenzetu hana uwezo wa kuwa katibu mkuu wa Yanga matukio haya yanayotokea Sasa ni ushahidi tosha kuwa boss wetu wa Secretarieti hatoshi, ni kweli wenda alikuwa Muhasibu mzuri pale Quality Group lakini Kuna utofauti mkubwa Kati ya kuendesha timu na kuwa Muhasibu wa kampuni binafsi.
-Washabiki wa Yanga tupunguze kumpigia makofi Manji kwa kila kitu anachosema tumfundishe kumkatalia na kusema hili sawa Lakin hili hapana bila hivyo atatupeleka shimoni.
-Mwisho boss wetu mkubwa tuliye mkodisha timu anapaswa kujua Yanga ni timu yenye umasikini mkubwa wa fedha lakini yenye utajili mkubwa Sana wa Mashabiki na wapenzi.. Kwa hiyo pesa sio kila kitu Kwenye timu, timu pia zinahitaji uongozi bora na Manji sio kiongozi bora wa timu bali ni mfadhiri bora hivyo anapaswa kupata katibu bora kama Dr Tiboroa,
Daniel Naftal Ngogo
Shabiki na mwanachama wa Yanga