Manyara: Kijana akutwa amejinyonga

Manyara: Kijana akutwa amejinyonga

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Kijana wa Kimasai rika la Morani, aliyejulikana kwa jina Sabaya Isaskar (31) mkazi wa Njaniodo, wilayani Kiteto mkoani Manyara amedaiwa kujinyonga hadi kufa kwa kutumia kamba ya manila.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Partimbo, Kimirei Mesiaya amethibitisha kutokea kwa kifo hicho leo Jumatatu Oktoba 23, 2023 akisema marehemu alikutwa porini juu ya mti ananing’inia na wasamaria wema waliokuwa wakipita kilometa 3 kutoka nyumbani kwake baada ya kujinyonga.

"Nilipokea taarifa ya mtu kujingonga porini na baadaye nikafuatilia na kubaini kifo hicho ambacho kwa kweli kinasikitisha sana, kwani aliyepoteza maisha hakuwa mgonjwa bali ameamua kuchukua maamuzi magumu ya kujiua," amesema Mesiaya.

Screenshot 2023-10-23 153210.png

Mwananchi
 
Huyu ni wa pili ndani ya siku mbili baada ya yule wa Ilula Iringa
 
Wamasai nao wana siteresi? Huwa nawaona kama vile wanaishi maisha huru sana na shuka zao matako nje nje bila kujali lo lote. Maisha hayana fundi ati!
 
Na wao mapenzi yameanza kuwatesa.Siku hizi washajua ladha zenye visimi.
 
HABARI Kijana mmoja rika la Morani wa kabila la Maasai, wilayami Kiteto mkoani Manyara aliyejulikana kwa jina la Sabaya Isaskar (31)mkazi wa Njaniodo, amekatisha maisha yake kwa kujinyonga hadi kufa akitumia kamba aina ya manila.

Kifo cha kijana huyu wa kifuaji Maasai kimevuta hisia kwa jamii huku ikielezwa kwa kabila la kimaasai mtu kujinyonga huwa ni nadra kwao.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Partimbo amethibitisha tukio la kijana huyo Morani wa Kimaasai kujinyonga, "Toka tulivyopata taarifa kuwa hili tukio limetokea tulipata mshtuko lakini niwashukuru walioshiriki toka mwanzo marehemu alipoonekana maeneo yale ya tukio hadi kumfikisha hospitalini"amesema Kimirei
 
Back
Top Bottom