Manyara: Mchimba madini mbaroni kwa tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi

Manyara: Mchimba madini mbaroni kwa tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Mchimbaji wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Erick Peter (36) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi wa shule ya sekondari Tanzanite wa kidato cha nne.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Manyara, Benjamin Kuzaga akizungumza leo Jumanne, Septemba 6, 2022 amesema Erick anashikiliwa kwa tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi wa shule ya sekondari Tanzanite ya mji mdogo wa Mirerani.

Kamanda Kuzaga amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa Septemba 1, 2022 akiwa mtaa wa Msikitini mji mdogo wa Mirerani.

"Tulimkamata mtuhumiwa huyo akiwa nyumbani kwa baba wa mwanafunzi huyo na kulazwa mahabusu kituo cha polisi Mirerani na tunatarajia kumfikisha mahakamani uchunguzi ukikamilika," amesema Kuzaga.

Baba wa mwanafunzi huyo, Shabani Khamisi ameiomba Serikali kuhakikisha mtuhumiwa huyo Erick afikishwe mahakamani ili kujibu shtaka hilo linalomkabiki.

"Huyu why not amempa mimba mtoto wangu kisha anaita wazee ili anilipe fedha na kumaliza juu juu, hili jambo nami sijakubali itabidi aende mahakamani akashtakiwe huko," amesema Khamisi.

Amesema lengo lake ni kuhakikisha mtuhumiwa huyo anahukumiwa kwenda jela miaka 30 kwa kumpa mimba mtoto wake ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha nne anayetarajia kufanya mtihani Novemba 2022.

MWANANCHI
 
Sasa form four mbona anazaa na anaendelea na shule …. Mzee ajatumia busara maana kijana hakuwa na nia mbaya kwani angekimbia wangempata Wap ?
 
Yani unatia mimba bado upo tu na bado unaenda kwa baba mzazi wa binti

Kama ni mimi kitendo cha kuniamb haoni siku zake tayari nishadandia lori mda huohuo uelekeo usiojulikana hata ruvuma vijijini huko nikajifiche halafu wazee wangu nawaachia wali solve Hilo
 
Wazee wengine wase..nge tu!! baada ya miaka 2 au mitatu mbele kutakuwa na mgogoro wa chuki kati ya binti na baba yake.
 
Mazikini jamaa anaenda Mangola hivi hivi kalime vitunguu sema mzee wangu umemkosea mjukuu
 
Sheria zetu linapokuja suala la ujauzito kwa watoto wa shule ziangaliwe upya.

Huwezi kumpeleka mtu jela miaka thelathini kwasababu ya ujauzito.

Ingekuwa kubakwa sawa, lakini kwa makubaliano yao binafsi ni uonevu tu
 
Mzee akili kisoda kweri.asa akienda jela yeye anapata faida gani.huyo mjukuu anabaki kama yatima .binti nae anabaki na stress tu.
 
Back
Top Bottom