Maofisa msitu wadaiwa kuchoma nyumba, familia yalala nje siku nne

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Familia ya watu sita wilayani Monduli, mkoani Arusha kwa siku nne imelala nje, baada ya nyumba zao kuchomwa moto na wanaodaiwa kuwa maofisa maliasili.

Watu hao wanaoishi Kata ya Monduli Juu wanadaiwa kuishi ndani ya hifadhi ya msitu wa jamii katika Kijiji cha Emairete.

Akizungumza na Mwananchi jana Januari 10, 2025 katika kijiji hicho, baba wa familia hiyo, Faraja Mephoroo amesema Januari 7, saa 12:00 asubuhi walifika watu aliodai aliwatambua kuwa wanafanya kazi kitengo cha maliasili walioambatana na mgambo na viongozi wa kijiji waliochoma nyumba zake tatu walizokuwa wakiishi na wake zake.

Akizungumza na Mwananchi ofisa maliasili Wilaya ya Monduli, Adili Mwanga amesema suala hilo liko ofisi ya kijiji ndio wanaoweza kutoa maelezo.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Emairete, Mboyo Kaiyai amesema wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya juhudi za mawasiliano ya kawaida ya kumhamisha mwananchi huyo kugonga mwamba.
 
Asogee tu hapo aiokoe familia na baridi, hakuna atakaemuonea huruma.
 
Watu wana roho mbaya sana.
 
Kitendo cha maafisa misitu na wanyama kufundishwa kwamba wanyama wana thamani kuliko binadam....kitendo cha wanajeshi kufundishwa kwamba wao sio binadam wa kawaida ......kitendo cha polis kufundishwa kwamba lazma utumie nguvu kila wakati...KITAKUJA KULETA BALAA ONE DAY...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…