MMASSY
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 290
- 196
SURA YA NNE Ibara ya 39 kifungu kidogo cha 3 yaani ib 39.(3).Inatamka kuwa "Raia wa Jamhuri Muungano hatapelekwa katika nchi ya nje yoyote kujibu mashtaka au kufanyiwa mahojiano ya aina yoyote kinyume cha ridhaa yake".Kifungu hiki hakitakuwa na mantiki katika katiba yetu kwa sababu zifauatazo i. Katika rasimu hii ,ibara ya 12 inaeleza kuhusu sera ya mambo ya nje na mwelekeo wa sera za nje za taifa huku ikisisitiza Tanzania itakuwa mastari wa mbele kupambana na makosa ya kimataifa ya kijamii angalia ibara ya 12(g).
Kwa kuwa Tanzania imeridhia mikataba ya kimataifa kuhusiana na hakiza binadamu,za kisiasa na za kijamii,na kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa Umoja na taifa pamoja na vyombo vingine vya kimataifa,si vyema na wala haitakuwa busara kulinda raia wake kukamatwa,kuhojiwa na hata kujibu mashtaka nje ya nchi kwa kuwa kufanya hivi kutakuwa kunakikua mikataba hii ambayo taifa limeirdhia na kuidhinsha.Kwa mfano,Tanzania ni mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC iliyopo the Hague-Uholanzi.Ikitokea raia wake anatakiwa kushitakiwa katika mahakama hii kwa makosa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu,Katiba yetu itakuwa inamlinda na kwa hivyo itakuwa inakinzana na sheria za kimataifa na pia kama rasimu hii ikipita kama ilivyo,kutakuwa na kujikanyaga kwa katiba kwa kuwa Ibara za 12(g)na hii ya 39(3) kitu ambacho kisheria kinaleta utata mkubwa kimantiki na hata kiutekelezaji.
Ikumbukwe kuwa Watanzania ni sehemu muhimu ya jamii ya kimataifa na kwa hivyo nao wanatenda makosa kama raia wan chi nyinginezo,kwa hiyo,hakuna haja ya kuwawekea kinga kwa kuwa tutakuwa tunasaliti juhudi za dunia za kupambana na uhalifu.Kwa mfano katika tukio la kulipuliwa ubalozi wa Marekani hapa Tanzania mwaka 1998,Mtanzania mmoja tayari amefungwa kule Marekani kwa tukio hilo.Je kama tungekuwa na katiba inayotamka hili linalotamkwa katika rasimu hii hatuoni kama tungekuwa tunalinda uhalifu?.
Kuna biashara haramu zinafanyika kote ulimwenguni na Watanzania ni wahusika pia,je kama kifungu hiki kikipita si kitachochea biashara ya uhalifu ambayo Tanzania kupitia kuridhia mikataba mbalimbali ya dunia imesaini kukabiliana nayo kwa ushirikiano na nchi nyinginezo?
Sikubalianai na hoja kwamba makosa yaliyofanywa na Mtanzania akiwa nje ya nchi ama hapa nchini anatakiwa kushitakiwa tu hapa nchini kwa kuwa kutokana na wadhifa wake ama nguvu zake kwenye vyombo vya haki nchini anaweza kupendelewa.
Nashauri na kupendekeza kuwa kama Mtanzania amevunja sheria popote pale duniani akamatwe mara moja na kukabidhiwa katika vyombo vya ngazi husika mara moja nah ii itasaidia sana pia kuheshimiana na mataifa mengine duniani.Mikataba yote iliyoridhiwa na Tanzania ina nguvu kisheria na kwa hiyo kama rasimu hii ikipita na kuwa katiba tayari itakuwa inakizana kwa ukali sana na sheria za kimataifa na mikataba mbali mbali ya kimataifa.
Pia ni vizuri kuelewa kuwa sheria ni msumeno na kila mtu yuko chini ya sheria,rasimu kutamka kuwa raia wa Jamhuri hatapelekwa nchi nyingine pale anapofanya kosa kinyume na ridhaa yake,ni sawa na kusema kuwa raia yeyote katika Jamhuri anatakiwa atoe ridhaa yake ndio ashitakiwe kitu ambacho hakipo sehemu yoyote na wala katika mfumo wowote wa sheria duniani.
Ni vizuri tukatazama vizuri sehemu hii na kuondoa kifungu hiki kwa kuwa hakina maslahi kwa taifa wala dunia na badala yake kimejaa maslahi binafsi ya washukiwa wa uhalifu na kukinzana na sheria zetu zenyewe na hata sheria za kimataifa.
Nitaendelea kuweka uchambuzi kadiri ninavyomaliza.Kimsingi ninazungumzia kwanza yale yanayohitaji marekebisho japo nimeikubali rasimu hii kwa 95%
Karibuni
Kwa kuwa Tanzania imeridhia mikataba ya kimataifa kuhusiana na hakiza binadamu,za kisiasa na za kijamii,na kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa Umoja na taifa pamoja na vyombo vingine vya kimataifa,si vyema na wala haitakuwa busara kulinda raia wake kukamatwa,kuhojiwa na hata kujibu mashtaka nje ya nchi kwa kuwa kufanya hivi kutakuwa kunakikua mikataba hii ambayo taifa limeirdhia na kuidhinsha.Kwa mfano,Tanzania ni mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC iliyopo the Hague-Uholanzi.Ikitokea raia wake anatakiwa kushitakiwa katika mahakama hii kwa makosa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu,Katiba yetu itakuwa inamlinda na kwa hivyo itakuwa inakinzana na sheria za kimataifa na pia kama rasimu hii ikipita kama ilivyo,kutakuwa na kujikanyaga kwa katiba kwa kuwa Ibara za 12(g)na hii ya 39(3) kitu ambacho kisheria kinaleta utata mkubwa kimantiki na hata kiutekelezaji.
Ikumbukwe kuwa Watanzania ni sehemu muhimu ya jamii ya kimataifa na kwa hivyo nao wanatenda makosa kama raia wan chi nyinginezo,kwa hiyo,hakuna haja ya kuwawekea kinga kwa kuwa tutakuwa tunasaliti juhudi za dunia za kupambana na uhalifu.Kwa mfano katika tukio la kulipuliwa ubalozi wa Marekani hapa Tanzania mwaka 1998,Mtanzania mmoja tayari amefungwa kule Marekani kwa tukio hilo.Je kama tungekuwa na katiba inayotamka hili linalotamkwa katika rasimu hii hatuoni kama tungekuwa tunalinda uhalifu?.
Kuna biashara haramu zinafanyika kote ulimwenguni na Watanzania ni wahusika pia,je kama kifungu hiki kikipita si kitachochea biashara ya uhalifu ambayo Tanzania kupitia kuridhia mikataba mbalimbali ya dunia imesaini kukabiliana nayo kwa ushirikiano na nchi nyinginezo?
Sikubalianai na hoja kwamba makosa yaliyofanywa na Mtanzania akiwa nje ya nchi ama hapa nchini anatakiwa kushitakiwa tu hapa nchini kwa kuwa kutokana na wadhifa wake ama nguvu zake kwenye vyombo vya haki nchini anaweza kupendelewa.
Nashauri na kupendekeza kuwa kama Mtanzania amevunja sheria popote pale duniani akamatwe mara moja na kukabidhiwa katika vyombo vya ngazi husika mara moja nah ii itasaidia sana pia kuheshimiana na mataifa mengine duniani.Mikataba yote iliyoridhiwa na Tanzania ina nguvu kisheria na kwa hiyo kama rasimu hii ikipita na kuwa katiba tayari itakuwa inakizana kwa ukali sana na sheria za kimataifa na mikataba mbali mbali ya kimataifa.
Pia ni vizuri kuelewa kuwa sheria ni msumeno na kila mtu yuko chini ya sheria,rasimu kutamka kuwa raia wa Jamhuri hatapelekwa nchi nyingine pale anapofanya kosa kinyume na ridhaa yake,ni sawa na kusema kuwa raia yeyote katika Jamhuri anatakiwa atoe ridhaa yake ndio ashitakiwe kitu ambacho hakipo sehemu yoyote na wala katika mfumo wowote wa sheria duniani.
Ni vizuri tukatazama vizuri sehemu hii na kuondoa kifungu hiki kwa kuwa hakina maslahi kwa taifa wala dunia na badala yake kimejaa maslahi binafsi ya washukiwa wa uhalifu na kukinzana na sheria zetu zenyewe na hata sheria za kimataifa.
Nitaendelea kuweka uchambuzi kadiri ninavyomaliza.Kimsingi ninazungumzia kwanza yale yanayohitaji marekebisho japo nimeikubali rasimu hii kwa 95%
Karibuni